Nav bar

Alhamisi, 22 Septemba 2022

SEKTA YA MIFUGO YAWASILISHA MPANGO WA MABADILIKO YA KAMPUNI YA RANCHI ZA TAIFA (NARCO)

 

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb) akizungumza wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge, Kilimo, Mifugo na Maji wakati wa kuwasilishwa kwa mpango wa mabadiliko ya Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) katika viwanja vya bunge jijini Dodoma, ambapo Naibu Waziri Ulega amesema wizara itahakikisha NARCO inakuja na mabadiliko makubwa katika kukuza Sekta ya Mifugo nchini. (20.09.2022)

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Bw. Tixon Nzunda, akizungumza wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge, Kilimo, Mifugo na Maji wakati wa kuwasilishwa kwa mpango wa mabadiliko ya Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) katika viwanja vya bunge jijini Dodoma, ambapo amesema wizara itahakikisha inawapima viongozi mbalimbali wa wizara katika kufikia matokeo chanya ya kuifanya NARCO kuwa ya kisasa zaidi. (20.09.2022)


Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) Prof. Peter Msoffe akiwasilisha mpango wa mabadiliko ya NARCO kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge, Kilimo, Mifugo na Maji katika viwanja vya bunge jijini Dodoma, ambapo amesema mpango huo utakuwa na wigo mkubwa wa kuwanufaisha wananchi katika kukua kiuchumi kupitia Sekta ya Mifugo nchini. (20.09.2022)


Kaimu Mwenyekiti Kamati ya Kudumu ya Bunge, Kilimo, Mifugo na Maji Mhe. Yustina Rahhi (Mb), akizungumza baada ya kuwasilishwa kwa mpango wa mabadiliko ya Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) kwa wajumbe wa kamati hiyo katika viwanja vya bunge jijini Dodoma, ambapo ameipongeza Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na NARCO namna walivyoandaa mpango huo ambao unaonesha dira katika kukuza Sekta ya Mifugo nchini. (20.09.2022)

Wakurugenzi kutoka idara mbalimbali za Sekta ya Mifugo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge, Kilimo, Mifugo na Maji wakati wa kuwasilishwa kwa mpango wa mabadiliko ya Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) katika viwanja vya bunge jijini Dodoma. (20.09.2022)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni