Nav bar

Jumanne, 11 Januari 2022

UFUGAJI KIBIASHARA NI JIBU LA UHABA WA AJIRA KWA VIJANA - ULEGA

Ufugaji wa kibiashara  unaofanywa na baadhi ya vijana katika Sekta ya mifugo na Uvuvi ni jibu la changamoto ya uhaba wa  ajira iliyokumba  vijana wengi hapa nchini.

Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri  wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega 15.12.2021 wakati akiongea na Viongozi wa Kituo cha Utafiti  Kongwa  (TALIRI), Agricultural Sector Support Trust Fund (PASS ) na  Kituo cha Ubunifu wa Kilimobiashara ( AIC.) Kwa lengo la kukagua shughuli zinazofanywa na taasisi hizo.

Mhe. Ulega alisema kuwa vijana wengi wakiingia katika kujiajiri kwa kufanya ujasiriamali wa shughuli za Ufugaji ,Kilimo na Uvuvi itakuwa ni jibu kwa tatizo la ajira hapa nchini. 

"Vijana wengi baada ya kuhitimu Masomo yao hawakupata ajira na matokeo yake wengi wamebaki wakikaa majumbani kwa wazazi bila shughuli ya kufanya wengine wamekuwa vijiweni bila shughuli ya  kufanya kwa  vijana kama taifa tegemeo la kesho", alisema

Vijana ambao wameteuliwa kupata mafunzo katika taasisi ya AIC wanaopata mafunzo ya ujasiriamali wa unenepeshaji wa mbuzi watakuwa wamejiajiri na kupunguza pengo la ajira la  vijana ambao hawajaajiriwa hapa nchini.

Aidha,  aliwataka AIC kupanua wigo wa shughuli ya kunenepesha  na kuanza kuchinja na kuuza nyama ya mbuzi yaani usindikaji ili kuongeza thamani ya bei ya Mbuzi.

Aliongeza kwa kuwataka AIC kwa kushirikana na  TALIRI kupanua shughuli hizi kwa kuongeza uwekezaji katika kituo cha unenepeshaji  na kuchoma  nyama kitaalam, kusindika ngozi na shughuli nyingine za kuvutia wananchi wasafiri kupita na kujipatia huduma mbali mbali ikiwemo nyama safi na bora.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa kituo cha ubunifu wa Kilimobiashara (AIC), Bw.Tamim Amijee amesema kituo chao kwa kushirikiana na TALIRI, kituo atamizi cha kilimo biashara cha vijana cha PASS-AIC na TALIRI farm, kilianzishwa mwaka 2019 kwa lengo la kuwawezesha vijana katika sekta ya Mifugo na Kilimo kuweza kuanzisha kuendesha na kumiliki biashara binafsi huku wakipata uzoefu na ushuri wa ufugaji wa kisasa. 

Mkurugenzi huyo amezungumzia changamoto wanazo kabiliana nazo ni uhaba wa ardhi, mitaji midogo na magonjwa ambayo yamekuwa yakirudisha nyuma maendeleo ya  kituo hicho.

Hivyo ameiomba serikali kuangalia suala hilo ili vijana wapate mikopo ya riba nafuu na maeneo ya kufanyia kazi ambayo wanamiliki.


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.Abdallah Ulega akiongea na vyombo vya Habari baada ya kutembelea Mabanda na ofisi zinazotumika kufundishia vijana wajasiria mali wanaojifunza Ufugaji wa Mbuzi kibiashara kwa kuwanenepesha na wakifikia uzito wa kuuza wanawauza na kujipatia kipato chenye faida, ambapo Mhe. Naibu Waziri alisema njia hii ya kujiajiri katika ujasiria mali wa Ufugaji wa kibiashara ndio jibu la kuondoa changamoto ya ajira kwa vijana wetu hapa nchini. Hayo aliyasema katika kituo cha utafiti wa Mifugo TALIRI  Wilayani Kongwa. (15.12.2021). 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni