Nav bar

Jumanne, 11 Januari 2022

MKUTANO WA KUPITIA NA KUTHIBITISHA MPANGO KABAMBE WA UVUVI.

Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah(Mgeni rasmi) akiongea wakati akifungua Mkutano wa Wadau wa Kupitia na Kuthibitisha Mpango Kabambe wa Uvuvi unaofanyika kwa siku mbili jijini Dodoma kuanzia Disemba 20- 21, 2021.Ambapo aliwataka Washiriki wa Mkutano huo kutumia fursa hiyo kupitia kwa makini kipengere kwa kipengere na hatimaye kuthibitisha rasimu ya Mpango huo wa Mwaka 2021. 

Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (kushoto) akijadiliana jambo na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO), Prof. Yunus Mgaya muda mfupi baada ya kufungua Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Mpango Kabambe wa Uvuvi unaofanyika kwa siku mbili jijini Dodoma kuanzia Disemba 20-21, 2021. 

 

Mkurugenzi wa Idara ya Uvuvi, Bw. Magese Bulayi akitoa neno fupi kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi kufungua Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Mpango Kabambe wa Uvuvi unaofanyika kwa siku mbili jijini Dodoma kuanzia Disemba 20-21, 2021. 

 


Mwakilishi kutoka Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO), Dkt. Oliver Mkumbo akitoa maelezo mafupi kuhusu ushiriki wa FAO katika kuandaa Mpango Kabambe wa Uvuvi katika Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Mpango huo unaofanyika kwa siku mbili jijini Dodoma kuanzia Disemba 20-21/2021

  

Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Wadau wa Sekta ya Uvuvi wanaoshiriki Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Mpango Kabambe wa Uvuvi unaofanyika kwa siku mbili jijini Dodoma kuanzia Disemba 20-21, 2021. 

 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni