Nav bar

Jumamosi, 21 Novemba 2020

WIZARA YAFANYA UKAGUZI WA UKARABATI WA BWAWA LA MAJI KWA AJILI YA MATUMIZI YA MIFUGO NA BINADAMU

 

Mhandisi kutoka Kampuni ya ZECO, Emmanuel Rodrick (kushoto) akitoa maelezo kwa Mhandisi kutoka WMUV, Masanga Makoje (mwenye flana ya njano) jinsi maji yaliyotokana na mvua kubwa, yalivyobomoa ukingo uliokarabatiwa na hatua zitakazochukuliwa kurekebisha hali hiyo ili maji yajae. Bwawa hilo lipo katika kijiji cha Narakauo, wilayani Simanjiro, mkoani Manyara. (16.11.2020)

Mhandisi Masanga Makoje (kulia) akiwa na Mhandisi wa Kampuni ya ZECO, Emmanuel Rodrick wakikagua ukarabati wa bwawa la maji kwa ajili ya matumizi ya Mifugo na Binadamu katika kijiji cha Narakauo, wilayani Simanjiro, mkoani Manyara. (16.11.2020)

Mhandisi kutoka WMUV, Masanga Makoje (mwenye flana ya njano kushoto) akitoa maelezo ya ushauri kwa Mhandisi wa Kampuni ya ZECO, Emmanuel Rodrick kuhusu ukarabati wa bwawa la maji kwa ajili ya matumizi ya Mifugo na Binadamu unaoendelea kufanyika katika bwawa hilo kwenye kijiji cha Narakauo, wilayani Simanjiro, mkoani Manyara. (16.11.2020)

Bwawa la maji kwa ajili ya matumizi ya Mifugo na Binadamu ambalo linakarabatiwa baada ya udongo uliokuwa unatumika kama kingo za kuzuia maji kusombwa kufuatia mvua kubwa iliyonyeesha katika kijiji cha Narakauo, wilayani Simanjiro, mkoani Manyara. (16.11.2020)

Picha ya pamoja ya viongozi wa kijiji cha Narakauo, Mhandisi kutoka WMUV, Masanga Makoje (wa nne kutoka kulia) na Mhandisi wa Kampuni ya ZECO, Emmanuel Rodrick (wa pili kutoka kushoto) baada ya kufanya ukaguzi kwa pamoja kuona maendeleo ya ukarabati wa bwawa la maji kwa ajili ya matumizi ya Mifugo na Binadamu katika kijiji cha Narakauo, wilayani Simanjiro, mkoani Manyara. (16.11.2020)


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni