Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2018

WAZIRI LUHAGA MPINA AMEWATAKA WAWEKEZAJI WA VIWANDA VYA KUCHINJA PUNDA NCHINI KUPANDISHA BEI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina   amewataka wawekezaji wa viwanda vya kuchinja Punda nchini kupandisha bei ya kununua wanyama hao badala ya shilingi laki mbili ya sasa kwa punda mmoja ili kudhibiti utoroshaji wa   mifugo   nje ya nchi ambapo inakadiriwa kuwa   zaidi ya   mifugo elfu kumi inatoroshwa   mipakani kwa siku kwenda nje ya nchi inakonunuliwa kwa bei ya juu. Akizungumza   leo   baada ya kufanya ziara ya kushitukiza katika Kiwanda   cha Punda   cha Hua Cheng Limited kilichopo nje kidogo ya mji wa Dodoma   alichokifungua   hivi karibuni, Waziri Mpina alisema bei hiyo   haiendani na gharama halisi ya   ufugaji wa Punda hali inayowafanya wafugaji kuwatorosha   mifugo na   kulikosesha taifa mapato makubwa. Alisema ili punda aweze kufikia hatua ya kuchinjwa inachukua kiasi cha miaka   miwili ambapo   gharama zake za ufugaji   zinakuwa   juu ukilinganisha na bei ya s...

WAZIRI MPINA AKABIDHIWA HATI YA KIWANDA CHA NYAMA SHINYANGA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina mwenye (suti miwani) akishuhudia utiaji saini wa hati ya makabidhiano ya Kiwanda cha nyama cha Shinyanga. Hati hiyo zilisainiwa na Mkurugenzi wa Ubinafsishaji   na Ufuatiliaji Jones   Mwalemba(aliyekaa upande wa kushoto)   kutoka Hazina kwa upande wa Serikali na Balozi   Fouad Mustafa (aliyeinama upande wa kulia)   kwa upande wa Kampuni ya Albwardy Investment Group aliyemwakilisha   mmiliki wa Kampuni hiyo bwana Ali Saeed Juma Albwardy. Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina (aliyekaa mwenye miwani) akishuhudia ubadilishanaji wa hati ya makabidhiano ya Kiwanda cha nyama cha Shinyanga.Kushoto ni Mkurugenzi wa Ubinafsishaji   na Ufuatiliaji Jones   Mwalemba   kutoka Hazina aliyeiwakilisha Serikali na kulia ni Balozi   Fouad