UTARATIBU WA KUPATA HUDUMA IDARA YA UKUZAJI VIUMBE KWENYE MAJI
IDARA YA UKUZAJI VIUMBE KWENYE MAJI Idara ya Ukuzaji Viumbe kwenye Maji ina jukumu la kuratibu mazingira rafiki ya uwekezaji kwa kutoa miongozo mbalimbali kutegemea na aina za uwekezaji. Taratibu za uwekezaji zitafuata miongozo na taratibu zilizopo kulingana na viwango vilivyopo nchini na kimataifa pamoja na kuzingatia hifadhi ya mazingira na uendelezaji wa rasilimali za uvuvi (Fisheries Investment Guidelines and The Environmental management Act). 1.0 Mchango wa Idara ya Ukuzaji Viumbe kwenye Maji katika uwekezaji Idara ina wajibu wa kutoa ushauri juu ya mambo mbalimbali katika uwekezaji ambayo ni pamoja na; Taratibu za kufuata kabla ya uwekezaji; Sheria zilizopo; Eneo linalofaa kwa uwekezaji; Aina ya viumbe wanaofaa kufugwa/kulimwa kwa kufuata kanuni za .uvuvi na "FAO code of conduct for transfer of species" (1988); na Teknolojia sahihi ambazo hazina athari kwa mazingira, zinazofaa kiuchumi na zinazokubalika katika...