Nav bar

Jumapili, 30 Machi 2025

KAMATI YA BUNGE YARIDHIA UPUMZISHWAJI WA SHUGHULI ZA UVUVI ZIWA TANGANYIKA

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imeridhia Upumzishwaji wa shughuli za uvuvi kwa ziwa Tanganyika uendelee kulingana na manufaa yanayopatikana kutokana na takwimu zinavyoeleza.

Akizungumza wakati wa Semina kuhusu upumzishwaji wa shughuli wa Ziwa Tanganyika kwa mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi uliopo Bungeni jijini Dodoma Machi 28, 2025  Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe.  Deodatus Mwanyika amesema wizara iendelee kufanya utafiti katika ukanda wote wa ziwa Tanganyika ili kubaini changamoto na kuzitatua.

Aidha Mhe. Mwanyika ameipongeza Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kuendele kulinda rasilimali za Taifa kwa manufaa ya Wananchi wake, vilevile amesisitiza kuwa udhibiti wa uvuvi haramu lishughulikiwe kwa nguvu kubwa.

Kwa upande wake Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji ameielekeza kikosi cha kuzuia uvuvi Haramu kuelekea ziwa Tanganyika na kuondoa Nyavu zote zinazotumika kwenye uvuvi Haramu (Gillnet) ili kuendelea kulinda Rasilimali za nchi yetu.

Aidha Mhe. Kijaji ameongeza kuwa Serikali itaendelea kutoa elimu kuhusu manufaa yanayopatikana baada ya zoezi la upumzishwaji wa shughuli za uvuvi ziwa Tanganyika kwa wavuvi pamoja na jamii kwa ujumla ili kuondoa taharuki wakati wa zoezi hilo.

Naye Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Edwin Mhede amesema Upumzishwaji wa shughuli za uvuvi katika Ziwa ulilenga kurejesha mifumo ya ikolojia kwa kuruhusu idadi ya samaki kuongezeka na hivyo kuimarisha usalama wa chakula, kuongeza kipato cha wavuvi na kukuza mchango wa sekta ya uvuvi kwenye pato taifa.

Aidha, Dkt. Mhede ameongeza kuwa katika kipindi cha mwaka 2024, jumla ya tani 85,180.11 zenye thamani ya shilingi bilioni 567.9 za samaki aina ya dagaa, migebuka, kuhe, ngege na wengineo zilivunwa kabla ya kupumzishwa kwa ziwa, baada ya kupumzishwa kwa ziwa uzalishaji wa mazao ya uvuvi yaliongezeka kwa kiasi cha tani 89,138   zenye  thamani ya shilingi bilioni 742.45 zilizovunwa mwaka 2024.

Sambamba na hayo upumzishwaji wa ziwa Tanganyika  ulifanyika Mei 15, 2024 hadi Agosti 15, 2024 na kwa mwaka huu unatarajiwa kufanyia Mei 15, 2025 hadi Agosti 15, 2025.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo Mhe. Deodatus Mwanyika akihitimisha Semina ya Wabunge  kuhusu upumzishwaji wa Ziwa Tanganyika, semina iliyofanyika Bungeni Jijini Dodoma Machi 28, 2025.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akizungumza na wajumbe wa kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo wakati na Wabunge  wanaotoka ukanda wa Ziwa Tanganyika wakati wa semina kuhusu Mpango wa Serikali wa  upumzishwaji wa Ziwa Tanganyika, semina iliyofanyika Bungeni Jijini Dodoma Machi 28, 2025.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi(Uvuvi) Dkt. Edwin Mhede akitoa semina kwa Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo  na Baadhi ya Wabunge wanaotoka Ukanda wa Ziwa Tanganyika kuhusu mpango wa Serikali wa kupumzisha Ziwa hilo, Semina hiyo iliyofanyika Machi 28, 2025 Bungeni Jijini Dodoma.

Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo wakifuatilia Semina iliyokuwa ikitolewa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuhusu mpango wa Serikali wa Kupumzisha Ziwa Tanganyika, Semina iliyofanyika Machi 28, 2025 Bungeni Jijini Dodoma.











Ijumaa, 28 Machi 2025

KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA BAJETI YA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI 2024/2025

Na Hamis Hussein, MLF Dodoma.

⬛️ Yaahidi Kuisemea Wizaya hiyo kuongezewa Fedha

Kamati ya Kudumu ya Viwanda,Biashara, Kilimo na Mifugo, chini ya Kaimu Mwenyekiti wake Mhe. Dkt. Medadi Kalemani Machi 27, 2025 imepokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa Bajeti ya Wizara ya  Mifugo na Uvuvi katika mwaka wa fedha 2024- 2025 na kuridhia mpango na bajeti ya mwaka fedha 2025- 2026.

Akizungumza kwenye kikao hicho Kaimu Mwenyekiti wa Kamati Mhe. Dkt. Medadi Kalemani ameipongeza Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambayo licha ya kuwa na bajeti ndogo lakini imeweza kutekeleza miradi ya kimkakati.

" Wizara hii  huwa haipati bajeti kubwa sana ukilinganisha na Wizara zingine lakini imeweza kutekeleza miradi ya kimkakati ambayo inaenda kuleta tija kwa wananchi, hivyo Mhe. Waziri na watumishi wote wa Wizara sisi kamati tutaendelea kuishauri serikali ili iongeze bajeti kwenye sekta hii ya mifugo na uvuvi kwani inatoa utajiri kwa wananchi, lakini pia mtuombee na sisi turudi ili tuendelee kuwasemea  watanzania" alisema Mhe.Dkt. Kalemani.

Aidha kamati hiyo iliiagiza Wizara kuweka mazingira yatakayowafanya wananchi wanaojihusisha na mnyonyoro wa thamani katika sekta za mifugo na Uvuvi waweze kunufaika na kuthaminiwa ili kuonesha umuhimu wa sekta za Mifugo na Uvuvi.

Kwa upande wake Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji alisema kuwa Wizara hiyo imeendelea kufanya vizuri na kuanza kuonekana ya thamani kwa jamii kutokana na usimamizi na ushauri mzuri unaotolewa na kamati ya kudumu ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo hivyo Wizara itaendelea kutekeleza miradi yakuinua kipato cha mwananchi mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

" Mhe. Mwenyekiti Wizara yetu inafanya vizuri kwa sasa na inaoneka kukua hii nikutokana na Ushauri na maelekezo ya kamati yako, hivyo tutaendelea kufanya kazi kwa weledi kuzikuza sekta hizi, hilo ndilo lengo letu." Alisema Mhe. Dkt. Kiaji.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe amesema Wizara hiyo itaendelea kutekeleza miradi kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo wa kitaifa na kimataifa na kuwa kama watendaji wa Wizara hiyo wataendelea kukamilisha miradi inayoendelea kutekelezwa ili ianze kutoa matunda kwa watanzania.

Katika mwaka 2024/2025, Wizara ya Mifugo na Uvuvi iliidhinishiwa jumla ya Shilingi Bilioni 460.3 kwa ajili ya kutekeleza majukumu yake, ambapo hadi kufikia Februari 28, 2025, jumla ya Shilingi  Bilioni 40.3 zimepokelewa  kwa ajili ya matumizi ya kawaida, sawa na asilimia 41.48 ya bajeti iliyotengwa,  Shilingi Bilioni 25.5 sawa na asilimia 56.88 ni kwa ajili ya Mishahara (PE) na Shilingi Bilioni 14.8 sawa na asilimia 28.29 ni kwa ajili ya Matumizi Mengineyo (OC).

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo na Wataalam wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa fedha 2024/2025 kwenye  Kikao  kilichofanyika Machi 27, 2025 Bungeni Jijini Dodoma
Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo Mhe. Dkt. Medadi Kalemani akizungumza na Wajumbe wa kamati hiyo na Wataalam wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa kupokea taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa fedha 2024/2025, Kikao hicho kilichofanyika Leo Machi 27, 2025 Bungeni Jijini Dodoma

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo na Wataalam wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa fedha 2024/2025 kwenye  Kikao  kilichofanyika Machi 27, 2025 Bungeni Jijini Dodoma
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe akifafanua Jambo mbele ya Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo wakati wa kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa fedha 2024/2025 kwenye  Kikao  kilichofanyika Machi 27, 2025 Bungeni Jijini Dodoma

Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Bishara, Kilimo na Mifugo Wakismikiliza Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji(aliyesimama) wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa bajeti ya Mwaka wa fedha 2024/2025 na mpango wa bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026 kwenye kikao cha Kamati ya Bunge kilichofanyika Machi 27, 2025 Bungeni, Jijini Dodoma.








Jumatano, 26 Machi 2025

DKT. KIJAJI AWATAKA WATUMISHI WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI KUWA WAZALENDO

Na. Stanley Brayton

◼️Ataka watumishi kuwatumikia vyema wananchi

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, amewataka watumishi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuwa na utumishi wa kizalendo uliotukuka kwa Watanzania ili kuweza kusongambele katika Sekta hizo mbili.

Akizungumza na watumishi wa Wizara hiyo leo Machi 26, 2025 katika Kikao chake na watumishi hao, kilicho jumuisha Wakuu wa Idara, Vitengo na Taasisi za Wizara, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara katika Mji wa Kiserikali Mtumba, Dkt. Kijaji amesema anafurahishwa sana na utendaji mzuri wa watumishi wa Wizara hiyo huku akiwapongeza kwa kazi nzuri wanazozifanya katika kuendeleza sekta za mifugo na uvuvi.

"wizara inaonekana jinsi inavyofanya kazi  na inaendelea kufanya kazi vyema kwani tangu tuanze kuzunguka na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, tulikopita kwenye Miradi yetu yote walitupongeza na kusema tumefanya vizuri" amesema Dkt. Kijaji.

Aidha, Dkt. Kijaji amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na kumteua kuwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi.

Vilevile, Dkt. Kijaji amesema matarajio na matumaini ni makubwa katika Sekta  za Mifugo na Uvuvi kwa sababu Mheshimiwa Rais tangu aingie madarakani ameamua kuzipa kipaumbele Sekta za uzalishaji ikiwemo Sekta hizi mbili, ambazo ndio Sekta zinazogusa maisha ya kawaida ya Watanzania na hakuna nyumba utakayokwenda ukakosa Mifugo au mvuvi, kila siku ya mungu Sekta hizi mbili lazima ziguswe, na ni Sekta zinazogusa watu wa chini kabisa.

Aidja, Dkt. Kijaji amewaelekeza Watendaji wa  Wizara kuhakikisha wanasimamia maeneo yote ya Mifugo na Malisho na kuainisha maeneo hayo pamoja na kuwaita wafugaji kuwaelewesha umuhimu wa kumiliki ardhi na malisho.

Halikadhalika, Dkt. Kijaji watendaji wa wizara kuanza zoezi ra kuwarasimisha wavuvi wote nchi na kuwatambua wapo wangapi na wanafanya nini, ikiwa ni pamoja na kujua kuwa kuna vyombo vingapi vya uvuvi nchini.

"Wakuzaji Viumbe Maji tuwe na tathimini ya maji yote na kuamua kufanya kazi ipasavyo ili ndani ya miaka 5 ijayo pato kubwa la nchi hii litokane na uchumi  Buluu, na hilo linawezekana." amesema Dkt. Kijaji

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, akitoa maelekezo  kwa watumishi wa Wizara hiyo, katika Kikao chake na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe, akizungumza na watumishi wa Wizara hiyo, katika Kikao cha Waziri  wa Mifugo na Uvuvi na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Edwin Mhede, akijibu hoja za watumishi mbalimbali na kuzitolea maelezo hoja hizo, katika Kikao cha Waziri wa Mifugo na Uvuvi na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Ndg. Abdul  Mhinte, akijibu hoja za watumishi mbalimbali na kuzitolea maelezo hoja hizo, katika Kikao cha Waziri  wa Mifugo na Uvuvi na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma.

Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Mhina, akiahidi mambo mazuri kiutendaji kwa watumishi wote wa Wizara, katika Kikao cha Waziri  wa Mifugo na Uvuvi na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (katikati), akisikiliza na kuandika hoja mbalimbali za Watumishi wa Wizara hiyo, katika Kikao chake na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma, wa pili kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe, wa kwanza kushoto ni Naibu Katibu Mkuu (Mifugo), Ndg. Abdul Mhinte, wa pili kulia ni Naibu Katibu Mkuu (Uvuvi), Dkt. Edwin Mhede, na wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Dkt. Charles Mhina.

Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Utafiti na Mafunzo ya Uvuvi, Bi. Emelda Adam, akimuomba Waziri wa Mifugo na Uvuvi (hayupo pichani), kuwajengea watumishi wa Wizara uwezo ili waweze kupata Maarifa zaidi kutokana na Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia, katika Kikao cha Waziri  wa Mifugo na Uvuvi na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma.

Mteknolojia wa Samaki Mwandamizi Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bw. Masui Munda, akimuomba Waziri wa Mifugo na Uvuvi (hayupo pichani), kufanyike uchunguzi yakinifu ili kujua mchango wa Sekta ya Uvuvi kwa wavuvi na jamii nzima na kujua Maendeleo yake halisi, katika Kikao cha Waziri  wa Mifugo na Uvuvi na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma.

Afisa Mifugo Mkuu, Bw. Emmanuel Kato, akimuomba Waziri wa Mifugo na Uvuvi (hayupo pichani), kuangalia kwa kina swala la Miradi iliyosimama ili kuweza kuendeleza, katika Kikao cha Waziri  wa Mifugo na Uvuvi na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma.

Afisa Uvuvi Mkuu, Bw. Nallianiel Mboje, akimuomba Waziri wa Mifugo na Uvuvi (hayupo pichani), kuongeza Watendaji katikati Sekta ya Uvuvi pamoja na kuongeza vitendea kazi vya kuzuia Uvuvi haramu, katika Kikao cha Waziri  wa Mifugo na Uvuvi na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma.

Afisa Mifugo Mkuu, Bw. Mussa Mrindoko, akimuomba Waziri wa Mifugo na Uvuvi (hayupo pichani), kuboresha machinjio ya Mifugo ili iendane na machinjio ya kisasa yenye vifaa vya kisasa, katika Kikao cha Waziri  wa Mifugo na Uvuvi na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma.

Picha ni watumishi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, wakimsikiliza  Waziri wa Mifugo na Uvuvi (hayupo pichani), akitoa maelekezo kwa watumishi hao, katika Kikao cha Waziri  wa Mifugo na Uvuvi na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (mstari wa mbele katikati), akiwa kwenye picha ya pamoja na Watumishi  wa Wizara hiyo, baada ya Kikao chake na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma, wa pili kushoto mstari wa mbele ni Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe, wa kwanza kushoto mstari wa kwanza ni Naibu Katibu Mkuu (Mifugo), Ndg. Abdul Mhinte, wa pili kulia mstari wa mbele ni Naibu Katibu Mkuu (Uvuvi), Dkt. Edwin Mhede, na wa kwanza kulia .stari  wa mbele ni Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Dkt. Charles Mhina.















Jumatatu, 17 Machi 2025

 SERIKALI YATAMBULISHA MRADI MPYA WA KIMAGEUZI KATIKA TASNIA YA MAZIWA 

Na. Stanley Brayton

Serikali imeendelea kufanya juhudi za kuimarisha na kuweka mikakati  bora ya kukuza Tasnia ya Maziwa kwa kutambulisha Mradi mpya wa Kimageuzi  wa Tasnia hiyo.

Akizungumza katika  Warsha hiyo ya  kutambulisha  Mradi wa Kimageuzi wa Tasnia ya Maziwa iliyofanyika leo Machi 17, 2025 mkoani Dodoma katika Ukumbi  wa Hoteli ya Rafiki, Katibu Mkuu Wizara  ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe, amesema Mradi huu utagharimu kiasi cha Dola 174.36 za Kimarekani na ni muhimu sana kwa watanzania wengi.

"tunamshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia kuwepo kwa Mradi huu ambao utasaidia kunyanyua uchumi wa Watanzania na nchi kiujumla" amesema Prof. Shemdoe 

Aidha, Prof. Shemdoe ameelekeza kuwa Mradi huo uzingatie thamani ya fedha, muda pamoja na matokeo  chanya yanayolenga kuwanufaisha vijana, wakina mama pamoja na makundi maalum 

Vilevile, Prof. Shemdoe ameeleza kuwa Mradi huo ni Muunganiko wa Tanzania Bara na Visiwani unaotarajiwa kufika katika Mikoa 10 na Wilaya 28.

Prof. Shemdoe amewashukuru wadau wa maendeleo pamoja na wadhamini ambao ni IFAD, OPEC Fund, AFD, Irish League of Credit Union's Foundation (ILCUF), HEIFER, International Tanzania (HI), Tanzania Agricultural Development Bank (TADB) na FAO.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo - Zanzibar, Ndg. Ali Khamis Juma, amesema Mradi huo unategemewa kuinua kipato na maisha ya Mtanzania hususani kwa wafugaji kwani Seerikali imejipanga kushirikiana na wafugaji wadogo na kuwasaidia kukua katika tasnia ya Maziwa.

Pia, Mkurugenzi wa Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Ndg. Stephen Michael, amesema Maziwa yanachangia kwa asilimia kubwa pato la Taifa, japo kunahitajika kuhakikisha upatikanaji wa Maziwa unatakiwa kuwekewa Mazingira mazuri ikiwemo kuboresha Malisho na upatikanaji wa maji, Huduma za Ugani, Tafiti, mafunzo na Masoko kwa ajili ya wafugaji.

Naye, Msajili wa Bodi ya Maziwa Tanzania, Prof. George Msalya amesema Tasnia ya Maziwa ina changamoto nyingi zikiwemo Uzalishaji mdogo wa Maziwa, Masoko na ukusanyaji wa Maziwa ambao unachangiwa sana na mabadiriko ya hali ya hewa, kwa hiyo Mradi huu utaenda fanya Mageuzi makubwa kitasnia.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe, akihutubia wadau wa Tasnia ya Maziwa, ni katika Warsha ya kutambulisha Mradi wa Mageuzi wa Tasnia ya Maziwa na Mabadiriko ya Tabia ya nchi, kilichofanyika katika Ukumbi wa Rafiki Hoteli, Machi 17, 2025, Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo, Ndg. Ali Khamis Juma, akielezea hali ya Tasnia ya Maziwa Zanzibar, ni katika Warsha ya kutambulisha Mradi wa Mageuzi wa Tasnia ya Maziwa  na Mabadiriko ya Tabia ya nchi, kilichofanyika katika Ukumbi wa Rafiki Hoteli, Machi 17, 2025, Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo  na Uvuvi (Mifugo), Ndg. Abdul Mhinte, akizungumza na wadau wa Tasnia ya Maziwa, ni katika Warsha ya kutambulisha Mradi wa Mageuzi wa Tasnia ya Maziwa  na Mabadiriko ya Tabia ya nchi, kilichofanyika katika Ukumbi wa Rafiki Hoteli, Machi 17, 2025, Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo  na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Edwin Mhede, akizungumza na wadau wa Tasnia ya Maziwa, ni katika Warsha ya kutambulisha Mradi wa Mageuzi wa Tasnia ya Maziwa  na Mabadiriko ya Tabia ya nchi, kilichofanyika katika Ukumbi wa Rafiki Hoteli, Machi 17, 2025, Dodoma.
Mkurugenzi wa Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Ndg. Stephen Michael, akitoa utangulizi, ni katika Warsha ya kutambulisha Mradi wa Mageuzi wa Tasnia ya Maziwa  na Mabadiriko ya Tabia ya nchi, kilichofanyika katika Ukumbi wa Rafiki Hoteli, Machi 17, 2025, Dodoma
Mkurugenzi wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo Tanzania (IFAD),Bw. Sakphouseth Meng, akizungumza na wadau wa Tasnia ya Maziwa, ni katika Warsha ya kutambulisha Mradi wa Mageuzi wa Tasnia ya Maziwa  na Mabadiriko ya Tabia ya nchi, kilichofanyika katika Ukumbi wa Rafiki Hoteli, Machi 17, 2025, Dodoma
Mkurugenzi wa AFD Tanzania, Bi. Celine Robert, akizungumza na wadau wa Tasnia ya Maziwa, ni katika Warsha ya kutambulisha Mradi wa Mageuzi wa Tasnia ya Maziwa  na Mabadiriko ya Tabia ya nchi, kilichofanyika katika Ukumbi wa Rafiki Hoteli, Machi 17, 2025, Dodoma
Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa  la HEIFER Tanzania, Bw. Mark Tsoxo, akizungumza na wadau wa Tasnia ya Maziwa, ni katika Warsha ya kutambulisha Mradi wa Mageuzi wa Tasnia ya Maziwa  na Mabadiriko ya Tabia ya nchi, kilichofanyika katika Ukumbi wa Rafiki Hoteli, Machi 17, 2025, Dodoma
Mratibu na Kiongozi wa Kiufundi wa Mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa, Ndg. Lazaro Kapella, akitambulisha Mradi huo kwa wadau wa Tasnia ya Maziwa, ni katika Warsha ya kutambulisha Mradi wa Mageuzi wa Tasnia ya Maziwa  na Mabadiriko ya Tabia ya nchi, kilichofanyika katika Ukumbi wa Rafiki Hoteli, Machi 17, 2025, Dodoma

Picha ni baadhi ya wadau wa Tasnia ya Maziwa walioshiriki ni katika Warsha ya kutambulisha Mradi wa Mageuzi wa Tasnia ya Maziwa  na Mabadiriko ya Tabia ya nchi, kilichofanyika katika Ukumbi wa Rafiki Hoteli , Machi 17, 2025, Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo  na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe (katikati waliokaa), akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau wa Tasnia ya Maziwa, ni katika Warsha ya kutambulisha Mradi wa Mageuzi wa Tasnia ya Maziwa  na Mabadiriko ya Tabia ya nchi, kilichofanyika katika Ukumbi wa Rafiki Hoteli , Machi 17, 2025, Dodoma.

















Jumatano, 22 Januari 2025

SERIKALI KUIMARISHA MIKAKATI YA KUKUZA SHUGHULI ZA UKUZAJI VIUMBE MAJI ZIWA TANGANYIKA

Na. Stanley Brayton

Serikali imeendelea kufanya juhudi za kuimarisha na kuweka mikakati bora ya kukuza shughuli za Ukuzaji Viumbe maji kupitia vizimba vya kufugia samaki ambapo njia hii inalenga kuboresha zaidi Uzalishaji  wa Samaki na kukuza shughuli za uchumi kwa wananchi na kufungua fursa za uchumi.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara  ya Mifugo na Uvuvi, leo Januari 22, 2025 mkoani Dodoma katika Mkutano wa kujadili ni namna gani ya kuimarisha Tasnia ya Ukuzaji Viumbe Maji kwa njia ya Vizimba na mashirikiano baina ya Wizara na Shirika la Uhifadhi wa Mazingira "The Nature Conservancy" pamoja na Taasisi zingine, Mkurugenzi wa Idara ya Ukuzaji Viumbe Maji, Dkt. Nazael Madalla amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alielekeza Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuhakikisha inahamasisha na kuendelea Ufugaji Samaki kwa njia ya Vizimba katika maeneno yote yanayofaa kiufugaji.

"hapa nchini kwetu Ziwa Tanganyika ni moja ya maeneo ambayo kuna fursa ya Ufugaji Samaki kwa njia ya Vizimba, na tumekutana hapa na wadau mbalimbali wa Ufugaji Samaki kwa njia ya Vizimba kutoka ndani ya nchi na nje ya nchi kwa ajili ya kujadili ni namna gani tutawezesha Ufugaji huu kwa jamii inayozunguka Ziwa Tanganyika, na kukubaliana kwa mikakati kuhakikisha kwamba kunakuwa na uwezeshaji pamoja na ulinzi  wa mazingira na utunzaji wa mazingira hayo ili kuleta faida nchini." amesema Dkt. Madalla

Aidha, Dkt. Madalla amesema serikali imekuwa ikifanya juhudi katika kukuza Tasnia ya Ukuzaji Viumbe Maji kwani tayari ilishapeleka Vizimba katika Ziwa Tanganyika na jana Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji alikwenda kutembelea Vizimba hivyo ambavyo vipo katika eneo la Katavi ambavyo wafugaji tayari walishaanza kufuga na Samaki wanaendelea vizuri kiasi cha kuwatia moyo wafugaji hao.

Vilevile Dkt. Madalla amesema Serikali kupitia Wizara inaendelea na zoezi la kutoa mafunzo kwa wavuvi juu ya Ufugaji Samaki kwa njia ya Vizimba, kutoa mikopo ya pembejeo,  kuendeleza maeneo ya Ufugaji,  kuanza Taratibu za kuanzisha Kituo cha Ukuzaji Viumbe Maji katika Ziwa Tanganyika, pamoja na kuhamasisha na kuwezesha Sekta Binafsi ili kuwekeza katika Uzalishaji na usambazaji wa pembejeo za Ufugaji Samaki.

Dkt. Madalla amesema kuwa kwa sasa mwitikio wa wananchi kufuga samaki kwa njia ya vizimba umeanza kuongezeka kutokana na serikali kuweka mazingira rafiki ikiwemo mikopo ambayo imekuwa ikiwanufaisha sana wafugaji wengi na baaadhi ya wadau katika Sekta wameainisha ni kwa namna gani ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba ulivyokuwa na tija kubwa kiuchumi kwani kwa sasa wananufaika sana kutokana na mradi huo.

Naye, Mkurugenzi wa Uvuvi kutoka Mamlaka ya Ziwa Tanganyika (LTA), Bi. Nyakorema Beatrice Marwa, amesema warsha hii inatija kubwa sana kwa sababu imekusanya wadau mbalimbali wa Tasnia ya Ukuzaji Viumbe  Maji toka Taasisi za Serikali na Binafsi na wadau wa Ziwa Tanganyika na lengo kutaka kuanda Mpango wa Utekelezaji kwa pamoja ambao haukizani na Sheria zetu na za nchi nne zinazozunguka Ziwa Tanganyika.

Pia, Meneja wa Mradi wa Ziwa Tanganyika wa Shirika la Uhifadhi wa Mazingira "The Nature Conservancy" (TNC), Bw. Fridolin Nzambimana amesema kuwa TNS wanachokifanya ni kuimarisha mashirikiano baina yao na serikali pamoja na Taasisi nyingine ili kuendeleza na kukuza Tasnia ya Ukuzaji Viumbe maji kwa njia ya kutumia Vizimba na ambayo inalinda rasilimalinza Uvuvi.

Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Ukuzaji Viumbe Maji, Dkt. Nazael Madalla, akielezea kwa kutumia projekta (haipo pichani) Malengo, Sheria, Kanuni na Taratibu za Serikali na Wizara katika Ukuzaji Viumbe Maji kwa njia ya Vizimba, ni katika Mkutano wa kujadili ni namna gani ya kuimarisha Tasnia ya Ukuzaji Viumbe Maji kwa njia ya Vizimba na mashirikiano baina ya Wizara na Taasisi ya Uhifadhi wa Mazingira "The Nature Conservancy" pamoja na Taasisi zingine, kilichofanyika katika Ukumbi wa Morena, Januari 22, 2025, Dodoma.
Mkurugenzi wa Ukuzaji Viumbe Maji Shirika la Uhifadhi wa Mazingira "The Nature Conservancy", Bw. Taylor Voortees, akielezea shughuli zinazofanywa na TNC, ni katika Mkutano wa kujadili ni namna gani ya kuimarisha Tasnia ya Ukuzaji Viumbe Maji kwa njia ya Vizimba na mashirikiano baina ya Wizara na Shirika la Uhifadhi wa Mazingira "The Nature Conservancy" pamoja na Taasisi zingine, kilichofanyika katika Ukumbi wa Morena, Januari 22, 2025, Dodoma.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) Dkt. Ismael Kimirei, akiwasilisha hoja, ni katika Mkutano wa kujadili ni namna gani ya kuimarisha Tasnia ya Ukuzaji Viumbe Maji kwa njia ya Vizimba na mashirikiano baina ya Wizara na Shirika la Uhifadhi wa Mazingira "The Nature Conservancy" pamoja na Taasisi zingine, kilichofanyika katika Ukumbi wa Morena, Januari 22, 2025, Dodoma.
Mratibu wa Ukuzaji Viumbe Maji Ukanda wa Ziwa Tanganyika -Shirika la Uhifadhi wa Mazingira, Dkt. Imani Kapinga ,akiwasilisha hoja, ni katika Mkutano wa kujadili ni namna gani ya kuimarisha Tasnia ya Ukuzaji Viumbe Maji kwa njia ya Vizimba na mashirikiano baina ya Wizara na Shirika la Uhifadhi wa Mazingira "The Nature Conservancy" pamoja na Taasisi zingine, kilichofanyika katika Ukumbi wa Morena, Januari 22, 2025, Dodoma.
Picha ni sehemu ya wadau wa Ukuzaji Viumbe Maji, wakiwa katika Mkutano wa kujadili ni namna gani ya kuendeleza Tasnia ya Ukuzaji Viumbe Maji kwa njia ya Vizimba na mashirikiano baina ya Wizara na Taasisi ya Uhifadhi wa Mazingira "The Nature Conservancy" pamoja na Taasisi zingine, kilichofanyika katika Ukumbi wa Morena, Januari 22, 2025, Dodoma.
Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Ukuzaji Viumbe Maji, Dkt. Nazael Madalla (mstari wa mbele katikati), akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau wa Ukuzaji Viumbe Maji, ni katika Mkutano wa kujadili ni namna gani ya kuendeleza Tasnia ya Ukuzaji Viumbe Maji kwa njia ya Vizimba na mashirikiano baina ya Wizara na Taasisi ya Uhifadhi wa Mazingira "The Nature Conservancy" pamoja na Taasisi zingine, iliyofanyika katika Ukumbi wa Morena, Januari 22, 2025, Dodoma.










Jumanne, 17 Desemba 2024

DKT KIJAJI AIAGIZA NARCO KUZALISHA MBEGU ZA MIFUGO, MALISHO KWA WINGI

◼️Ataka visima 6  vya maji NARCO kukamilishwa Kabla ya  January 5, 2025 

Waziri wa Mifugo na  Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji ameiagiza Kampuni ya Ranchi za Taifa NARCO iliyopo Kongwa Jijini Dodoma Kuongeza wigo wa Uzalishaji wa Mbegu Bora za  Mifugo na Malisho itakayoongeza upatikanaji wa Nyama nchini na Kukuza uchumi wa Wafugaji.

Dkt. Kijaji ametoa maagizo hayo Leo Desemba 17, 2024 Wakati wa Ziara yake kwenye Kambuni ya Ranchi za Taifa NARCO na kuahidi kurudi Januari 5, 2025 ili kuona utekelezaji wa maagizo hayo.

" NARCO Mnajukumu la kuzalisha mbegu bora za aina Mbalimbali, Watanzania wanahitaji mifugo inayouzika kwa urahisi  hapa ndani ya nchi na  Kimataifa tunataka kila mfugaji akiuza Ng'ombe apate Milioni Nne hivyo nawataka Mzalishe mbegu Bora kwaajili wafugaji wetu" amesema Dkt. Kijaji.

Kuhusu uzalishaji wa Mbegu za Malisho Dkt Kijaji amemwagiza Mkurugenzi wa Uzalishaji na Maendeleo ya  Masoko Stephen Michael  kushirikiana na NARCO kukamilisha malipo ya Mkandarasi wa mradi wa visima sita wenye thamani ya milioni 700 ili visima hivyo vianze kutumika kuzalishia malisho.

" Tumetembelea mradi wa Visima hapa Narco ni mradi mkubwa serikali imetoa milioni 700 lakini umekwama kwa sababu ya madai ya Mkandarasi, sasa nataka nitakaporudi hapa Januari 5, 2025 Visima na Mabirika haya ya kunyweshea Ng'ombe  niyakute yameanza  kutumika" alisema  Dkt. Kijaji.

Kwa upande wake  Mwenyekiti wa Bodi ya NARCO Aziz Mrima  amesema bodi hiyo inajukumu la kuifanya kampuni hiyo kuzalisha  mbegu bora za mifugo zitakazoweza kushindana na wafugaji wengine barani afrika hivyo ameahidi kuyatekeleza  maelekezo ya Waziri Dkt. Kijaji.

Naye Mkurugenzi wa Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko Stephen Michael  katika kutekeleza maelekezo hayo idara yake itaendelea kufuatilia ili kukamilika mradi huo ambapo hadi sasa tayari Bilioni 3.2 zimepatikana kwaajili ya Malipo hayo.

                                                                    
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mheshimiwa Dkt. Ashatu Kachwamba Kijaji (aliyonyoosha mkono), akimuuliza Kaimu Meneja wa Ranchi za Taifa (NARCO LTD), Dkt. Nickson Mbise, juu ya aina na sifa ya ng'ombe wanaopatikana katika Ranchi ya Taifa ya Kongwa, mara alipowasili Ranchi ya Kongwa kwa ajili ya Ziara fupi ya Kikazi, Disemba 17, 2024 Kongwa - Dodoma.

 
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mheshimiwa Dkt. Ashatu Kijaji (wa kwanza kushoto), akisalimiana na Mkurugenzi wa Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Ndg. Stephen Michael, mara alipowasili Ranchi ya Kongwa kwa ajili ya Ziara fupi ya Kikazi, Disemba 17, 2024 Kongwa - Dodoma.



Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO LTD), Ndg. Mohammedi Zuberi Mbwana, akitoa Ripoti ya Utendaji kazi wa NARCO, mara alipowasili Ranchi ya Kongwa kwa ajili ya Ziara fupi ya Kikazi, Disemba 17, 2024 Kongwa - Dodoma.



MKurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Maeneo ya Maliso na Rasilimali za vyakula za Mifugo. Dkt. Asimwe Rwiguza (wa tatu kulia), akimuelezea Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mheshimiwa Dkt. Ashatu Kachwamba (wa kwanza kushoto), sifa za malisho ya majani aina ya Juncao, mara alipowasili Ranchi ya Kongwa kwa ajili ya Ziara fupi ya Kikazi, Disemba 17, 2024 Kongwa - Dodoma.