Na. Stanley Brayton
◼️Ataka watumishi kuwatumikia vyema wananchi
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, amewataka watumishi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuwa na utumishi wa kizalendo uliotukuka kwa Watanzania ili kuweza kusongambele katika Sekta hizo mbili.
Akizungumza na watumishi wa Wizara hiyo leo Machi 26, 2025 katika Kikao chake na watumishi hao, kilicho jumuisha Wakuu wa Idara, Vitengo na Taasisi za Wizara, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara katika Mji wa Kiserikali Mtumba, Dkt. Kijaji amesema anafurahishwa sana na utendaji mzuri wa watumishi wa Wizara hiyo huku akiwapongeza kwa kazi nzuri wanazozifanya katika kuendeleza sekta za mifugo na uvuvi.
"wizara inaonekana jinsi inavyofanya kazi na inaendelea kufanya kazi vyema kwani tangu tuanze kuzunguka na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, tulikopita kwenye Miradi yetu yote walitupongeza na kusema tumefanya vizuri" amesema Dkt. Kijaji.
Aidha, Dkt. Kijaji amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na kumteua kuwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi.
Vilevile, Dkt. Kijaji amesema matarajio na matumaini ni makubwa katika Sekta za Mifugo na Uvuvi kwa sababu Mheshimiwa Rais tangu aingie madarakani ameamua kuzipa kipaumbele Sekta za uzalishaji ikiwemo Sekta hizi mbili, ambazo ndio Sekta zinazogusa maisha ya kawaida ya Watanzania na hakuna nyumba utakayokwenda ukakosa Mifugo au mvuvi, kila siku ya mungu Sekta hizi mbili lazima ziguswe, na ni Sekta zinazogusa watu wa chini kabisa.
Aidja, Dkt. Kijaji amewaelekeza Watendaji wa Wizara kuhakikisha wanasimamia maeneo yote ya Mifugo na Malisho na kuainisha maeneo hayo pamoja na kuwaita wafugaji kuwaelewesha umuhimu wa kumiliki ardhi na malisho.
Halikadhalika, Dkt. Kijaji watendaji wa wizara kuanza zoezi ra kuwarasimisha wavuvi wote nchi na kuwatambua wapo wangapi na wanafanya nini, ikiwa ni pamoja na kujua kuwa kuna vyombo vingapi vya uvuvi nchini.
"Wakuzaji Viumbe Maji tuwe na tathimini ya maji yote na kuamua kufanya kazi ipasavyo ili ndani ya miaka 5 ijayo pato kubwa la nchi hii litokane na uchumi Buluu, na hilo linawezekana." amesema Dkt. Kijaji
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, akitoa maelekezo kwa watumishi wa Wizara hiyo, katika Kikao chake na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe, akizungumza na watumishi wa Wizara hiyo, katika Kikao cha Waziri wa Mifugo na Uvuvi na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Edwin Mhede, akijibu hoja za watumishi mbalimbali na kuzitolea maelezo hoja hizo, katika Kikao cha Waziri wa Mifugo na Uvuvi na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Ndg. Abdul Mhinte, akijibu hoja za watumishi mbalimbali na kuzitolea maelezo hoja hizo, katika Kikao cha Waziri wa Mifugo na Uvuvi na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma.
Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Mhina, akiahidi mambo mazuri kiutendaji kwa watumishi wote wa Wizara, katika Kikao cha Waziri wa Mifugo na Uvuvi na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (katikati), akisikiliza na kuandika hoja mbalimbali za Watumishi wa Wizara hiyo, katika Kikao chake na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma, wa pili kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe, wa kwanza kushoto ni Naibu Katibu Mkuu (Mifugo), Ndg. Abdul Mhinte, wa pili kulia ni Naibu Katibu Mkuu (Uvuvi), Dkt. Edwin Mhede, na wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Dkt. Charles Mhina.

Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Utafiti na Mafunzo ya Uvuvi, Bi. Emelda Adam, akimuomba Waziri wa Mifugo na Uvuvi (hayupo pichani), kuwajengea watumishi wa Wizara uwezo ili waweze kupata Maarifa zaidi kutokana na Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia, katika Kikao cha Waziri wa Mifugo na Uvuvi na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma.
Mteknolojia wa Samaki Mwandamizi Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bw. Masui Munda, akimuomba Waziri wa Mifugo na Uvuvi (hayupo pichani), kufanyike uchunguzi yakinifu ili kujua mchango wa Sekta ya Uvuvi kwa wavuvi na jamii nzima na kujua Maendeleo yake halisi, katika Kikao cha Waziri wa Mifugo na Uvuvi na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma.
Afisa Mifugo Mkuu, Bw. Emmanuel Kato, akimuomba Waziri wa Mifugo na Uvuvi (hayupo pichani), kuangalia kwa kina swala la Miradi iliyosimama ili kuweza kuendeleza, katika Kikao cha Waziri wa Mifugo na Uvuvi na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma.
Afisa Uvuvi Mkuu, Bw. Nallianiel Mboje, akimuomba Waziri wa Mifugo na Uvuvi (hayupo pichani), kuongeza Watendaji katikati Sekta ya Uvuvi pamoja na kuongeza vitendea kazi vya kuzuia Uvuvi haramu, katika Kikao cha Waziri wa Mifugo na Uvuvi na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma.
Afisa Mifugo Mkuu, Bw. Mussa Mrindoko, akimuomba Waziri wa Mifugo na Uvuvi (hayupo pichani), kuboresha machinjio ya Mifugo ili iendane na machinjio ya kisasa yenye vifaa vya kisasa, katika Kikao cha Waziri wa Mifugo na Uvuvi na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma.
Picha ni watumishi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, wakimsikiliza Waziri wa Mifugo na Uvuvi (hayupo pichani), akitoa maelekezo kwa watumishi hao, katika Kikao cha Waziri wa Mifugo na Uvuvi na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (mstari wa mbele katikati), akiwa kwenye picha ya pamoja na Watumishi wa Wizara hiyo, baada ya Kikao chake na Watumishi wa Wizara pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo vya Wizara hiyo, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo - Mtumba, Machi 26, 2025, Dodoma, wa pili kushoto mstari wa mbele ni Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe, wa kwanza kushoto mstari wa kwanza ni Naibu Katibu Mkuu (Mifugo), Ndg. Abdul Mhinte, wa pili kulia mstari wa mbele ni Naibu Katibu Mkuu (Uvuvi), Dkt. Edwin Mhede, na wa kwanza kulia .stari wa mbele ni Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Dkt. Charles Mhina.