"SITACHOKA KUWASEMEA, KUWAPAMBANIA VIJANA WA KITANZANIA" - MHE. NG'WASI
Na, Hamisi Hussein, Singida Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi ambae pia ni Mbunge wa Kundi la Vijana kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Ng'wasi Damas Kamani, amesema ataendelea kulisemea, kulitetea na kulipambania kundi la vijana kupata fursa mbalimbali za kujiinua kiuchumi hususani katika sekta ya mifugo na uvuvi. Mhe. Ng'wasi ameyasema hayo leo Desemba, 24, 2025, Wilayani Iramba Mkoani Singida, alipomwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba katika Kikao cha Baraza la Kawaida la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wilayani humo. "Pamoja na majukumu haya niliyopewa sitachoka kumtetea, kumsemea na kumpambania kijana wa kitanzania, lakini pia hata katika sekta hii ninayoisimamia huku ndio nitaweka nguvu zaidi ili ikiwezekana na sekta zingine ziige kutoka kwetu namna ya kumsaidia kijana wa kitanzania"amesema N'gwasi. Katika hatua nyingine Mhe. Ng'w...