Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2025

DKT. BASHIRU AVUTIWA NA UWEKEZAJI SEKTA ZA MIFUGO NA UVUVI

Picha
◼️Ahimiza Watumishi wa Wizara yake kuwajibika Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amevutiwa na uwekezaji uliofanywa na wadau wa sekta za Mifugo na Uvuvi nchini ambapo amewataka kushirikiana kwa ukaribu na Wizara yake ili kuendelea kuzalisha mazao yanayokidhi viwango stahiki. Mhe. Balozi Dkt. Kakurwa amesema hayo Novemba 27,2025 alipotembelea viwanda vya kusindika nyama (TANCHOICE na UNION MEAT) vyakula vya Mifugo na Samaki (BACKBONE)  na kiwanda cha kuzalisha chanjo (TANCHOICE) vilivyopo mkoani Pwani. “Nipo tayari kuwapa ushirikiano wote mnaohitaji na mimi nimekuja kuomba ushirikiano wenu kwa sababu bila ushirikiano wetu kazi hii haiwezi kwenda inavyotakiwa na kila jambo mnaloona ni la mafanikio mtueleze ili tulidumishe na kila mnaliona ni dosari mtubainishie afu mtoe maoni ya namna ya kuondokana na vikwazo hivyo na kutatua dosari zilizopo kwa uzoefu mlionao” Ameongeza Mhe. Balozi Dkt. Bashiru. Aidha Dkt. Bashiru ametoa wito kwa watumishi wa Wizara yake ...

MRADI WA BBT WA UNENEPESHAJI MBUZI NA KONDOO KUANZA KUTEKELEZWA KONGWA

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi yaanza Rasmi kutekeleza Mradi wa miaka Mitano wa Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT) ya Unenepeshaji wa Mbuzi na Kondoo katika eneo la Kituo cha Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) iliyopo Kongwa, ikiwa na lengo la kuongeza ushiriki wa Vijana na Wanawake katika ujasiliamali wa Biashara ya Mifugo. Akizungumza wakati wa Ziara yake ya kikazi wakati akikagua Miundombinu ya Mradi huo, leo Novemba 27, 2025 Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Meena amesema Mradi huo unatarajiwa kuanza kutoa Mafunzo mapema mwaka huu, na lengo la Mradi huo ni kwa ajili ya kuwapatia Vijana Mafunzo ya Unenepeshaji wa Mbuzi na Kondoo ili waweze kufuga kibiashara. “mradi huu utakuwa na uwezo wa kutoa Mafunzo kwa vijana 200 kwa mwaka na vijana Takribani 1750 wataweza kupata Mafunzo hayo kwa miaka Mitano.” amesema Bi. Meena Aidha, Bi. Meena amesema Mradi huo una eneo la heka 2000 kwa ajili ya kupanda M...

DKT. BASHIRU AANZA KUWAPA ‘TABASAMU’ WAFUGAJI NCHINI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa na Naibu wake Mhe. Ng’wasi Damas Kamani wameanza ziara ya kukagua shughuli mbalimbali za sekta ya Mifugo mkoani Morogoro ambapo wametembelea shamba la Mifugo na mfugaji Maloloi Kibangashi lililopo Wilayani Movemero. Akizungumza mara baada ya kufika kwenye shamba la Bw. Maloloi Balozi Dkt. Bashiru mbali na kuvutiwa na kasi ya mabadiliko ya mfumo wa ufugaji aliyonayo mfugaji huyo kutoka kwenye ufugaji wa asili na kugeukia wa kisasa ambapo alitoa rai kwa wafugaji wengine kote nchini kuiga mfano huo. “Wewe ni mmoja wa wafugaji wa kisasa ambao eneo lako limepangwa, limepimwa,limelindwa kisheria, lina maji, lina malisho na lina umeme na nimeambiwa ulianza kama mfugaji wa asili wa kawaida hivyo nimekuja kukuhakikishia wewe na wafugaji wote nchi nzima kwamba Wizara yangu itakuwa na ushirikiano na wafugaji wote na mimi pia nawaomba ushirikiano” Amesema Mhe. Balozi Dkt. Bashiru. Mhe. Dkt. Bashiru ameongeza kuwa Serikali kupitia Wiza...

SERIKALI INATAMBUA MCHANGO WA WAVUVI KATIKA KUKUZA UCHUMI NCHINI - MHE. LIJUALIKALI

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV Mkuu wa Wilaya ya Nkasi, Mhe. Peter Lijualikali amesema Serikali inatambua mchango wa wavuvi katika kukuza uchumi nchini na ndio maana inaendelea kuboresha Miundombinu na maisha yao kwa kutoa mikopo ya boti za kisasa, vizimba na vitendea kazi vingine vitakavyowasaidia wavuvi kuongeza uzalishaji wa mazao hayo ya uvuvi. Akizungumza katika Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mvuvi Duniani, leo Novemba 21, 2025 katika Kijiji cha Kalungu kilichopo Wilayani Nkasi Mkoani Rukwa, Mhe. Lijualikali amesema kuwa Maadhimisho hayo ni matokeo ya Dira na maono  thabiti ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha Sekta ya Uvuvi inachangia ipasavyo kwenye uchumi wa Taifa na kuinua kipato cha wananchi, hususan wavuvi wadogo na wakuzaji viumbe maji. "Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, anaendelea kuzipa kipaumbele Sekta za uzalishaji, ikiwemo Sekta ya Uvuvi." alisema Mhe. Lijualikali Aidha, Mhe. Lijualikali amebainis...

MAUZO YA SAMAKI YAPAA NJE YA NCHI

Picha
Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Kisaka Meena, Novemba 21, 2025, alipokuwa akihitimisha maadhimisho ya Siku ya Mvuvi Duniani jijini Dar es Salaam katika fukwe za Kawe Beach kwa lengo la kuhamasisha dhana ya Uchumi wa Buluu, ulaji wa samaki na mazao yake, pamoja na kuimarisha shughuli za uhifadhi wa mazingira na rasilimali za uvuvi yaliyofanyika kwa muda wa siku 2 kuanzia tarehe 20 hadi 21 Novemba 2025. Akizungumza wakati wa hotuba yake, Bi. Meena alisema kuwa uuzaji wa samaki nje ya nchi umeongezeka kutoka tani 42,000 zenye thamani ya shilingi bilioni 509.9 hadi tani 59,000 zenye thamani ya shilingi bilioni 755. Sambamba na hilo, idadi ya wavuvi imeongezeka kutoka 198,475 mwaka 2023 hadi 201,661 mwaka 2024. Idadi ya viwanda vya kuchakata mazao ya uvuvi nayo imeongezeka kutoka 21 hadi 64 katika kipindi cha mwaka 2023 hadi 2024. “Sisi sote tunafahamu kuwa Tanzania imebarikiwa kuwa na rasilimali nyingi za maji ikiwemo bahari, mito, mabwawa, maziwa na m...

DKT. BASHIRU AANIKA MWELEKEO WA SEKTA YA MIFUGO KWA WAFUGAJI

Picha
◼️Ni katika mkutano wake na Chama cha Wafugaji nchini Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amekutana na Sekretarieti ya Chama cha wafugaji nchini ikiwa ni takribani siku mbili tu tangu alipoapishwa kushika wadhifa huo ambapo amewaelekeza kuhakikisha wanalinda mafanikio yaliyopatikana kupitia sekta ya Mifugo. Katika kikao hicho kilichofanyika Novemba 20,2025 kwenye Ofisi za Wizara hiyo zilizopo eneo la Mtumba jijini Dodoma, Balozi Dkt. Bashiru amesema kuwa sekta za uzalishaji ikiwemo Mifugo na Uvuvi ndio nguzo ya kulifanya Taifa lijitegemee kiuchumi na kutekeleza dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Mhe. Dkt. Sami Suluhu Hassan. “Tunategemea sekta ya Ufugaji itoe mchango mkubwa katika uendeshaji na ukuzaji wa uchumi wetu na kuboresha maisha ya watu wetu” Ameongeza Balozi Dkt. Bashiru. Aidha Balozi Dkt. Bashiru ameelekeza kutoanzishwa kwa miradi mipya Wizarani hapo hadi itakapokamilishwa ile iliyoanzishwa awali na kuanza kufanya kazi iliyokusudiwa....

MRADI WA UZALISHAJI MBEGU BORA ZA NG’OMBE WA MAZIWA MBIONI KUTEKELEZWA NCHINI

Picha
◼️Utagharimu takribani Shilingi Bil. 7 ◼️ Umefadhiliwa na Shirika la kimataifa la Ushirikiano wa Maendeleo la Korea (KOICA) Nchi ya Tanzania kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Chuo kikuu cha Kilimo cha Sokoine na timu ya Watafiti kutoka chuo kikuu cha Jeonbuk nchini Korea inatarajia kutekeleza mradi wa utafiti na uzalishaji wa ng’ombe wa Maziwa kwa kutumia teknolojia za Uhimilishaji na Uhawilishaji wa viini tete. Hayo yamebainishwa na Ujumbe wa Wawakilishi kutoka chuo kikuu cha Jeonbuk nchini Korea Prof.  Hakkyo Lee, Mwondha Faluku na Rais wa Taasisi ya CACOON Bw. HeeJae ulioongozwa na Msajili wa Bodi ya Maziwa nchini Prof. George Msalya ambao walifika ofisini kwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi. Agness Meena kwa ajili ya kutambulisha azma ya utekelezaji wa mradi huo. Akizungumza mara baada ya kupokea ujumbe huo, Bi. Meena amewataka wataalam hao kukaa pamoja na wataalam wa Wizara yake na kuwashirikisha wadau wengine wanaohusika na utekelezaji wa miradi nchini ili k...

TUTATEKELEZA MAONO YA MHESHIMIWA RAIS DKT. SAMIA - BALOZI DKT. BASHIRU

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amewataka watumishi wa Wizara hiyo kufanya kazi kwa juhudi ili kutekeleza maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan juu ya sekta hizo za uzalishaji. Dkt. Kakurwa amesema hayo mara baada ya kupokelewa na Watumishi wa Wizara hiyo Novemba 18,2025  Wizarani hapo ikiwa ni muda mfupi baada ya kuapishwa kushika wadhifa huo. "Sote tumesikia aliyosema Mhe. Rais kupitia hotuba yake ya ufunguzi wa Bunge kuhusu sekta zetu za Mifugo na Uvuvi hivyo ni wajibu wetu kuhakikisha tunatekekeza maono hayo kwa kila mmoja wetu kutimiza wajibu wake kwa nafasi aliyonayo" Amesema Dkt. Bashiru. Aidha Dkt. Bashiru amewataka watumishi hao kutoa ushirikiano wa kutosha kwake na Naibu Waziri Mhe. Ng'wasi Kamani katika kipindi chote cha kuwahudumia wananchi hususan wadau wa sekta za Mifugo na Uvuvi.  Mhe. Balozi Dkt. Bashiru na Naibu wake Mhe. Kamani waliteuliwa na Rais Samia kushika nyadhifa hizo Novemba...

SERIKALI YA AWAMU YA SITA, YADHAMIRIA KUIMARISHA SEKTA ZA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Na. Stanley Brayton - Dodoma ◾ Yaongeza eneo la ufugaji kutoka ekari milioni 3.46 hadi Milioni 6. ◾ Yaahidi kuendeleza chanjo za mifugo, kuboresha kosafu ya mifugo, ujenzi wa majosho na machinjio. ◾ Kujenga bandari ya uvuvi ya Bagamoyo na kukamilisha bandari ya uvuvi ya Kilwa Masoko ambayo itatoa fursa za ajira takriban 30,000. Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imejipanga vyema kuimarisha sekta za mifugo na uvuvi ili kuongeza uzalishaji na kutoa fursa kwa Vijana na wadau wote ili kukuza kipato chao na kipato cha Taifa kiujumla. Akizungumza wakati wa kuhutubia na kufungua rasmi Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye mkutano wa kwanza kikao cha nne cha Bunge hilo, jijini Dodoma )14.11.2025), Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema mikakati ya kukuza sekta ya mifugo katika muhula wa pili wa serikali ya awamu ya sita ni pamoja na kuongeza eneo lililopimwa la shughuli za ufugaji kutoka ekari milioni 3.46 hadi ekari milioni 6 il...