TANZANIA YAZINDUA RASMI MRADI WA STOSAR II: KUBORESHA USALAMA NA UBORA WA CHAKULA
Tanzania kung’aa masoko ya kimataifa Na Daudi Nyingo-Dar Es Salaam Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Umoja wa Ulaya (EU), na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), imezindua rasmi Mradi wa STOSAR II unaolenga kuimarisha mifumo ya Sanitary and Phytosanitary (SPS) katika ukanda wa SADC ili kuwezesha biashara salama, ushindani na uendelevu wa mazao ya kilimo na vyakula. Akizindua mradi huo tarehe 1 Septemba 2025 katika Hoteli ya Four Points by Sheraton jijini Dar es Salaam, Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Edwin Mhede, alisema mradi huo utashughulikia maeneo muhimu yakiwemo afya ya wanyama, afya ya mimea, lishe na maendeleo ya minyororo ya thamani, hususan katika nyanja za uchunguzi na ufuatiliaji wa magonjwa, udhibiti wa ubora, na upatikanaji wa masoko ya kikanda na kimataifa. “Mkutano huu ni tukio mahususi la kuzindua mradi huu wa kikanda ambao Tanzania ni miongoni mwa wanufai...