Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2025

UTAFITI WA WINGI WA SAMAKI ZIWA TANGANYIKA UMEANZA RASMI

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV  Kigoma  Agosti 27, 2025 Nchi zilizopo ukanda wa Ziwa Tanganyika ambazo ni Tanzania, Zambia, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Burundi, zimezindua rasmi zoezi la Utafiti wa wingi na mtawanyiko wa Samaki katika Ziwa Tanganyika, ambao zoezi hilo linalenga kutambua wingi wa mazao ya Uvuvi katika Ziwa hilo. Akizungumza katika Hafla ya Uzinduzi wa Utafiti wa wingi na mtawanyiko wa Samaki Ziwa Tanganyika, leo Agosti 27, 2025 Mkoani Kigoma, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Edwin Mhede amesema Serikali imeelekeza kufanya Tathmini ya wingi wa Samaki waliopo katika Ziwa Tanganyika ili kujua wametawanyikaje na kwenye maeneo yapi, pamoja na kujua Takwimu sahihi za wingi wa Samaki katika Ziwa hilo. “Utafiti huu utahusisha mazao ya Uvuvi aina ya Migebuka, Dagaa au Samaki wanaoelea wa tabaka la juu, ili kusaidia uwekezaji wenye tija kwa takwimu na kuvutia wawekezaji.” ameseama Dkt. Mhede Aidha, Dkt. Mhede ameweka bayana kuwa zoezi hilo halifanywi ...

ELIMU YA ULINZI WA RASILIMALI ZA UVUVI YAFIKA RORYA

Picha
Na, Hamisi Hussein, Rorya - MARA Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Ulinzi na Usimamizi wa Rasilimali za Uvuvi  kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Kimansa  Bugomba amesema ulinzi wa rasilimali za sekta ya uvuvi utasaidia kuongeza upatikanaji wa mazao ya uvuvi  na kuchochea uchumi wa wananchi na  pato la Taifa. Akitoa elimu ya ulinzi na usimamizi wa rasilimali za uvuvi kwa ukanda wa Ziwa Victoria Agosti 26, 2025, kwa Wavuvi na wachakataji wa mazao ya uvuvi katika Mwalo wa Isegere uliopo Halmashauri ya Wilaya ya Rorya Mkoani Mara Bw. Bugomba  amesema wajibu wa kulinda rasilimali za uvuvi ni jambo shirikishi baina ya wadau na serikali kutokana na umuhimu wake kiuchumi. "Wizara yetu kwa mwaka 2025/2026  katika vipaumbele tulivyonavyo ni kuongeza uzalishaji wa mazao ya uvuvi kwa kutumia teknolojia, ulinzi na usimamizi wa rasilimali za uvuvi, kwa hiyo  sisi serikali na nyie wadau wa uvuvi tunawajibika kulinda rasilimali hizo ili sote tunufaike kiuchumi" alise...

ELIMU YA ULINZI WA RASILIMALI ZA UVUVI ZIWA VICTORIA YAANZA KUTOLEWA KWA WAVUVI

Picha
Na. Hamis Hussein Timu ya Watalam wa Udhibiti Ubora na Masoko ya Mazao ya Uvuvi (QC) na Ulinzi na Usimamizi wa Rasilimali za Uvuvi (FRP) kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeanza utoaji wa elimu ya Ulinzi wa Rasilimali za Uvuvi, Uhifadhi bora wa Mazao ya Uvuvi na Umuhimu wa ulaji wa mazao ya Uvuvi  kwa wadau wa sekta ya uvuvi Ukanda wa Ziwa Victoria ili kudhibiti uvuvi haramu na kulinda rasilimali zilizopo ndani ya ziwa hilo. Timu hiyo ilianza utoaji elimu hiyo  kwa wadau hususan  Wavuvi na Wachakataji wa mazao ya uvuvi  Agosti 23, 2025  katika mialo ya Wilaya za Nyamagana na Ilemela mkoani Mwanza mara baada ya kikao kazi cha kujadili mikakati ya pamoja ya kudhibiti uvuvi haramu ukanda wa Ziwa Victoria. Akizungumza katika Mwalo wa Kayenze Kubwa uliopo Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza Afisa Uvuvi Mwandamizi Bw. Hamprey Tilla aliwahimiza wavuvi kufuata sheria za uvuvi na kuuunga mkono jitihada za serikali kwa kuwa mabalozi na wadau muhimu katika kutafuta mikakati ya...

MIFUGO NA UVUVI YAIONESHA UBABE ARDHI

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV Dodoma  Agosti 20, 2025 ⬛  Yaipiga Ardhi kipigo cha goli 3-1 bila huruma  ⬛ Kamba Wanaume yawatoa povu Ardhi, yashinda mivuto yote miwili, huku wanawake washinda kwa mvuto moja  ⬛  Mpira wa Pete wanawake washinda kwa goli 16-7 Wizara ya Mifugo na Uvuvi yaibuka kidedea Maandalizi ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali Tanzania (SHIMIWI) kwa kuipiga Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi goli 3-1, mechi ambayo imechezwa katika Viwanja vya Kilimani, leo Agosti 23, 2025. Ambapo magoli ya upande wa Mifugo na Uvuvi yalifungwa na wachezaji Hema Mugenyo (1), Joseph Onesmo (2) kwa kipindi cha kwanza, na kwa upande wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kipindi cha kwanza goli lilifungwa na mchezaji Cleophace Simon. Aidha, Mifugo na Uvuvi imeibuka kidedea mbele ya Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kwa Wanaume kushinda mivutano yote miwili na wanawake kushinda kwa mvuto mmoja huku mvuto mmoja watosha...

BI. KABYEMERA AWATAKA WANAMICHEZO KUINGIA KAMBINI KABLA YA KWENDA SHIMIWI

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV Dodoma  Agosti 23, 2025 Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Bi. Lucy Kabyemera, amewataka wanamichezo wa Wizara wanaoshiriki Michezo ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali Tanzania (SHIMIWI) kuweka kambi mapema ili kuweza kujiandaa vizuri katika michuano hiyo ya SHIMIWI ili kuweza kuleta makombe na Mataji na kuongeza sifa ya Wizara. Amezungumza hayo leo Agosti 23, 2025, kwenye Uwanja wa Kilimani Mkoani Dodoma, wakati wa BONANZA la kujiandaa na Michuano ya SHIMIWI. Aidha, Bi.Kabyemera amewataka wanamichezo wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na wanamichezo wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kudumisha Umoja na ushikamano katika kuhakikisha mazoezi yanafanyika vizuri na kwa uweledi ili kuibuka vinara katika michuano hiyo. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Bi. Lucy Kabyemera, akizungumza na kuwapa nasaha wanamichezo wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na wanamichezo wa ...

WADAU WATAKIWA KUSHIRIKIANA KUDHIBITI UVUVI HARAMU ZIWA VICTORIA

Picha
Na Hamisi Hussein - Mwanza. Serikali Kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imesema ulinzi wa rasilimali za uvuvi katika ukanda wa Ziwa Victoria ni suala linalohitaji ushirikiano wa pamoja baina yake na wadau wote wanaohusika kwenye mnyororo wa thamani wa  sekta ya uvuvi. Akizungumza wakati wa Kufungua Kikao cha kujadili mikakati ya kudhibiti uvuvi haramu na biashara haramu ya mazao ya uvuvi kwa ukanda wa Ziwa Victoria  kilichofanyika Ukumbi wa Nyakahoja  jijini Mwanza Agosti 22, 2025 Naibu  Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Edwin Mhede alisema wadau wa sekta ya uvuvi kwa kushirikiana  na serikali kuhakikisha uvuvi haramu unadhibitiwa kwa kuja na mikakati ya pamoja ikiwemo elimu. “Ni lazima tuungane na kuwa na mikakati ya pamoja kupiga vita vitendo hivi. Sio jukumu la Serikali Kuu pekee; ni wajibu wa kila mdau wa sekta hii wakiwemo wavuvi, wachakataji, wasafirishaji, wamiliki wa viwanda vya zana  za uvuvi, wauzaji na wasambazaji wa zana za uvuvi pamoja na Serikali...

MHE. DKT. KIJAJI AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA BANDARI YA UVUVI KILWA MASOKO

Picha
Na. Omary Mtamike Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji ametembelea na kukagua hatua mbalimbali za ujenzi wa Bandari ya Uvuvi unaoendelea Kilwa Masoko mkoani Lindi Agosti 21,2025 kama inavyoonekana pichani chiniπŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

CHANJA ZENYE THAMANI YA MILIONI 117 ZATOLEWA KWA WAVUVI KILWA

Picha
Na. Omary Mtamike ◼️ Zina uwezo wa kukausha tani 3.7 za dagaa kwa siku Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi chini ya programu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) imewawezesha wavuvi wa dagaa waliopo eneo la Kilwa Kivinje mkoani Lindi Chanja 40 za kisasa za kuanikia dagaa zenye thamani ya shilingi Mil. 117. Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi chanja hizo iliyofanyika Agosti 21,2025  Wilayani Kilwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amesema kuwa tukio hilo ni sehemu ya mkakati wa Serikali unaolenga kuondokana na changamoto ya upotevu wa mazao ya Uvuvi baada ya kuvunwa na kuhakikisha dagaa zinazovuliwa kwenye eneo hilo zinakaushwa kwenye mazingira yanayozingatia usalama wa chakula. “Natambua kuwa hapo awali dagaa mnaovua hapa walikuwa wakiharibika kutokana na kukaushiwa kwenye miundombinu isiyo rafiki na wakati mwingine walikuwa wakikutwa na mchanga au matope jambo ambalo mbali na kupunguza thamani ya mazao hayo sokoni lili...