Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Julai, 2025

BI. MEENA AWATAKA WAFUGAJI NA WAFANYABIASHARA WA MIFUGO KUPELEKA MIFUGO KARANTINI KABLA YA KUUZA NJE YA NCHI

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV Kibaha, Pwani  Julai 30, 2025 ⬛  Ataka Kituo cha Karantini ya Mifugo Kwala na Kampuni ya NARCO kuweka alama kwenye mipaka ya maeneo yao. ⬛ Ataka Dawati la Ndege Wafugwao kuanzisha Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT) ya Kuku Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Meena amewataka Wafugaji na Wafanyabiashara za Mifugo kupeleka Mifugo yao kwenye kituo cha Karantini ya Mifugo ili kufanyiwa Uchunguzi wa Magonjwa kabla ya kuuza Mifugo hiyo nchi za nje, ikiwa ni njia moja wapo ya kukuza Biashara hiyo Kimataifa. Akizungumza wakati alipotembelea Kituo cha Karantini ya Mifugo Kwala, Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO), Shamba la Kuku la Kampuni ya Tanzania Sunshine na Kampuni ya Mkuza Chicks, leo Julai 30, 2025 Mkoani Pwani, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Meena amesema uwepo wa Kituo cha Karantini ya Mifugo ni fursa ya kimkakati katika kuyafikia masoko ya mifugo na mazao yake ya ndani na nje ya nchi. “Kituo hiki ni muhimu sana, na kimekaa Kim...

DKT. MHEDE: TAASISI ZA FEDHA ZITOE MIKOPO YENYE RIBA NAFUU KWA WAFUGAJI

Picha
Na. Martha Mbena,  Dodoma Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imetoa rai na ushauri kwa taasisi za fedha nchini, hasa benki, kutoa masuluhisho ya kifedha na mikopo yenye riba himilifu kwa wafugaji na wadau wa mnyororo wa thamani wa sekta ya mifugo ili waweze kufanya biashara shindani ya mifugo na mazao yake na kuinua uchumi wao na Taifa kwa ujumla. Rai hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Edwin Mhede, leo Julai 23, 2025 katika Hoteli ya Gerwill Jijini Dodoma wakati akifungua Kongamano la kujadili fursa za sekta ya Mifugo na ngozi ulioandaliwa na Serikali kwa kushirikiana na benki ya Equity Tanzania Ltd. "Watu wetu watakapokuja kukopa nawaomba sana tuzingatie kutokwenda zaidi ya ukomo wa riba uliowekwa na mdhibiti wa sekta ya fedha (Benki Kuu ya Tanzania). Tufanye kama vile ambavyo kiongozi wetu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, alivyothubutu kuweka fedha ya umma kwenye afua mbalimbali ili kuwasaidia wa...

SERIKALI YAANZA KUPANDIKIZA SAMAKI ZIWA HAUBI KONDOA DC

Picha
Na. Hamis Hussein Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Edwin Mhede amezindua rasmi upandikizaji wa vifaranga vya samaki aina sato katika ziwa Haubi lililopo halmashauri ya Wilaya ya Kondoa ili kuongeza aina ya samaki wanaopatika kwenye ziwa hilo. Dkt. Mhede amezindua upandikizaji huo julai 21, 2025 katika kijiji cha Haubi ambapo amesema Wizara ya Mifugo na Uvuvi itatuma wataalam kwa ajili kufanya tathmini ya namna ya kulinda ikolojia ya ziwa hilo ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa wananchi kufanya upandikizaji wa vifaranga vya samaki. Amesema ili kuongeza aina ya samaki wanaopatikana kwenye ziwa hilo  wizara itashirikiana na wananchi wa kijiji hicho ambao ndio wamiliki wa asili wa ziwa hilo na watalam watatoa  elimu ya jinsi ya kupandikiza  samaki aina ya sato tofauti na Kambare wanaopatikana kwa sasa ambao wamesababisha wananchi wa kijiji cha Haubi kuwa na mavuno ya samaki ya msimu. Kwa upande kwake mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Bi. Mwasiti Juma a...

BI. MEENA AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA UONGOZI WA MRADI WA C - SDTP JIJINI DODOMA

Picha
Na. Hamis Hussein Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agnes Meena ameongoza Kikao cha kamati ya uongozi wa mradi wa mageuzi katika tasnia ya maziwa kwa kuzingatia mabadiliko ya tabia nchi leo Julai 22, 2025 katika hoteli ya Rafiki jijini Dodoma. Kikao hicho kimelenga Kutambulisha mradi huo wa mageuzi ya tasnia ya maziwa  kwa kuzingatia mabadiliko ya tabia ya nchi kwa kamati ya uongozi ili kamati iweze kupitia na kuuidhinisha mpango kazi wa mradi na manunuzi kwa mwaka 2025/ 2026.

CHANJO YA MIFUGO ITAONGEZA THAMANI YA MIFUGO YETU - DKT. MHEDE

Picha
Na. Hamisi Hussein, Kondoa Uamuzi wa Serikali wa kuwekeza kwenye sekta ya mifugo kwa kutoa ruzuku ya chanjo na utambuzi wa mifugo utasaidia kupatikana kwa  ithibati kutoka Shirika la Afya ya Wanyama Duniani (WOAH) ya kufanya biashara ya mifugo na mazao yake kwenye masoko ya ndani na ya kimataifa jambo litakaloinua uchumi wa wananchi na taifa kwa ujumla. Hayo yamefahamika wakati Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Edwin Mhede akikagua utekelezaji wa Kampeni ya Chanjo na Utambuzi wa Mifugo  katika kijiji cha Soera wilayani  Kondoa mkoani Dodoma leo Julai 21, 2025.   " Leo tumekabidhi pikipiki 31 kwa maafisa ugani ili waweze kutekeleza kampeni ya chanjo na utambuzi wa mifugo, serikali imetoa ruzuku ya chanjo ya asilimia 50 kwa ng'ombe, mbuzi na kondoo na asilimi 100 (bure) kwa chanjo ya kuku kwahiyo chanjo  hii itaongeza thamani ya mifugo yetu" amesema Dkt. Mhede. Kuhusu utambuzi Dkt. Mhede amesema zoezi la chanjo ya mifugo linaenda sambamba na ...

DKT. MHEDE AZITAKA TAASISI ZINAZOFANYA KAZI MPAKANI NAMANGA KUFANYA KAZI KWA USHIRIKIANO ILI KULETA TIJA

Picha
 Na. Stanley Brayton, WMUV   Longido   Julai 20, 2025  Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Edwin Mhede, amezitaka Taasisi zinazofanya kazi katika mpaka wa Namanga kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuleta tija katika Uzalishaji na kutekeleza majukumu yao na kuleta matokeo chanya.  Akizungumza leo Julai 20, 2025 alipotembelea Kituo cha Ulinzi na Usimamizi wa Rasilimali za Uvuvi (FRP), Mnada wa Upili na Idara ya Huduma za Mifugo vilivyoko katika mpaka wa Namanga, Wilaya ya Longido, kwa lengo la kufanya ufuatiliaji wa shughuli za Uvuvi na Mifugo katika eneo hilo na kuongea na Watendaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi walioko katika Kituo hicho ili kubaini changamoto zinazowakabaili maafisa katika kutekeleza majukumu yao, Dkt. Mhede amesema ni muhimu kushirikiana kati ya Taasisi na Taasisi katika kuleta tija na kuongeza uzalishaji pamoja na Maendeleo nchini. Vilevile, Dkt. Mhede amesema ni vyema Wataalam wa Sekta zote kushirikiana na wadau...

UWEZESHAJI WAVUVI WAONGEZA MAVUNO YA SAMAKI KUFIKIA TANI ZAIDI YA LAKI 5 KWA MWAKA

Picha
Na. Hamisi Hussein, Lindi Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imesema Programu ya utoaji wa boti za kisasa za uvuvi pamoja na programu nyingine zimelenga  kuwawezesha wavuvi wadogo kunufaika na shughuli za uvuvi hapa nchini. Akikabidhi boti za kisasa za uvuvi na vifaa vyake awamu ya pili kwa mikoa ya Lindi na Mtwara, hafla iliyofanyika katika Bandari ya Lindi leo Julai 18, 2025,  Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agnes Meena amesema uwezeshwaji wa wavuvi wadogo umeongeza tija katika sekta ya uvuvi ambapo kiwango cha samaki kinachovunwa kwa mwaka kimeongezeka zaidi  baada ya uwezeshaji huo. "Zoezi la ugawaji wa boti za kisasa za uvuvi na Vifaa vyake lililozinduliwa na Mhe. Rais ni sehemu ya juhudi za serikali kuwawezesha wavuvi wadogo kunufaika na sekta ya uvuvi, na juhudi hizi zimeongeza kiwango cha samaki wanaovunwa kutoka tani 387,542.56 zenye thamani ya Shilingi trilioni 1.74 mwaka 2017/2018 hadi kufikia tani 529,668.01 zenye thamani ya Shilingi trili...

DKT. MHEDE AHITIMISHA MKUTANO WA WADAU WA TASNIA YA KUKU

Picha
Na. Hamis Hussein Naibu Katibu Mkuu  Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Edwin Mhede amehitimisha  mkutano wa wadau wa tasnia ya kuku ujulikanao  (National Poultry Delivery Lab), uliofanyika kwa siku mbili katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.  Akizungumza leo Julai 16, 2025 katika hafla ya kufunga Mkutano huo Dkt. Mhede amesisitiza kuundwa haraka kwa kamati ndogo ya kiufundi itakayoratibu na kufuatilia maazimio ya mkutano huo na kuahidi kushirikiana nayo  ili kuhakikisha kuwa  Wizara kwa kushirikiana na wadau, inakamilisha na kuzindua  Mkakati wa Tasnia ya Kuku. Aidha, Dkt. Mhede amewapongeza wadau wa tasnia ya kuku walivyobainisha na kujadili changamoto na fursa za tasnia hiyo na kutoa mikakati ya kuinua tasnia hiyo , ikiwa ni hatua muhimu ya kuanisha masuala ya kuzingatia katika uandaji wa Mkakati wa Kitaifa wa Tasnia ya Kuku Nchini. Katika hatua nyingine Dkt. Mhede amesisitiza kuongeza wigo wa ushiriki wa wadau wengine katika mnyororo wa thamani...

DKT. KIJAJI AKABIDHI BOTI ZA UVUVI ZENYE THAMANI YA BIL.2

Picha
Na. Omary Mtamike ◼️Ni sehemu ya Boti 120 zinazotolewa na Serikali kwenye awamu ya pili ◼️Wavuvi 205 kunufaika Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amekabidhi boti 13 za Uvuvi zenye thamani ya takribani shilingi Bil. 2 kwa Vikundi vya mikoa ya Pwani na Dar-es-salaam ambazo zinatarajiwa kuwanufaisha zaidi ya Wavuvi 205  wa mikoa hiyo. Mhe. Dkt. Kijaji amekabidhi boti hizo Julai 16, 2025 kwenye ufukwe wa Shirika la Uvuvi nchini (TAFICO) ambapo mkoa wa Pwani umekabidhiwa Boti 8 huku mkoa wa Dar-es-Salaam ukikabidhiwa boti 5 zote jumla zikiwa na uretu wa mita 12 na 14 ambazo zinajumuisha vifaa mbalimbali ikiwa ni pamoja na Nyavu, kamba, maboya, nyuzi, kitafuta samaki na boti saidizi maarufu kama dingi. “Boti mlizopokea leo zimefanyiwa maboresho yote yaliyotokana na maoni mliyotoa kutoka kwenye boti za awamu ya kwanza na sisi kama Serikali tunatamani kuona mnaendelea mnafanikiwa kupitia boti hizo” Ameongeza Mhe. Dkt. Kijaji Aidha Mhe. Dkt. Kijaji amebainisha kuwa ugawaji wa...

DKT. MHEDE AFUNGUA MKUTANO WA WADAU WA TASNIA YA KUKU

Picha
Na. Hamis Hussein  Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Edwin Mhede amefungua Mkutano wa tasnia ya Kuku (National Poultry Delivery Lab) unaofanyika  katika Hoteli ya Serena, Jijini Dar-es-salaam kuanzia leo Julai 15-16, 2025.  Mkutano huo umelenga kuwakutanisha wadau wa tasnia ya kuku ili kuchambua, kujadili na kutoa suluhisho ya namna ya kukabiliana na changamoto zinazopunguza ufanisi na ushindani wa tasnia ya Kuku nchini. Akifungua Mkutano huo,  Dkt. Mhede alielezea kuwa tasnia ya kuku  imeajiri asilimia 65 ya vijana na asilimia 51 ya wanawake nchini  "Tasnia ya Kuku inachagiza ukuaji wa sekta nyingine ikiwemo Kilimo kutokana na mahitaji makubwa  ya vyakula vya Kuku vinavyotokana na mahindi na soya  ambayo vimeifanya tasnia hii  ya kuku kuwa ya kimkakati nchini" alisema Dkt. Mhede. Aidha, Dkt Mhede amewahimiza Washiriki wa mkutano huo kutumia jukwaa hilo kuchambua na kuanisha maeneo ya kimkakati ambayo yatatatua changamoto zina...

UTEKELEZAJI KAMPENI YA CHANJO: MIFUGO MILIONI 6 YACHANJWA NDANI YA WIKI 2

Picha
Na. Omary Mtamike ◼️Zoezi sasa kuendelea kwa miezi 2 Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amebainisha kuwa kampeni ya kitaifa ya Chanjo na Utambuzi wa Mifugo imefanyika kwa mafanikio ambapo takribani Mifugo Milioni 6 imechanjwa na kutambuliwa tangu kuanza kwa kampeni hiyo Julai 02,2025 hadi sasa.  Mhe. Dkt. Kijaji asema hayo wakati wa tukio la kuanza kwa kampeni hiyo mkoani Dodoma lililofanyika Wilaya ya Bahi Julai 15, 2025 ambapo ametoa shukrani kwa wafugaji kote nchini kwa namna walivyojitokeza tangu kuanza kwa zoezi hilo ambapo amewaomba kuendelea kufanya hivyo kwa kipindi chote cha miezi miwili ya utekelezaji wake. “Mhe. Rais amedhamiria kutekeleza kampeni hii kwa wafugaji wote bila kumuacha hata mmoja na ndio maana amewawezesha maafisa Mifugo kwenye kata zote pikipiki na mafuta yake ili waweze kuwafikia wafugaji wote hivyo sitegemei kuona mtaalam yoyote wa Mifugo akiwa ofisini wakati wa utekelezaji wa kampeni hii” Ameongeza Mhe. Dkt. Kijaji Kwa upande wake mwakili...

CHANJO NA UTAMBUZI NI MAPINDUZI YA SEKTA YA MIFUGO NCHINI-DKT.KIJAJI

Picha
Na. Omary Mtamike ◼️Serikali yadhamiria kuondokana na homa ya Mapafu ya Ng’ombe ifikapo 2030 Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amesema kuwa kampeni ya kitaifa ya Chanjo na Utambuzi wa Mifugo itakuwa ni chachu ya mapinduzi wa sekta ya Mifugo nchini. Mhe. Kijaji amesema hayo wakati wa ziara yake ya Ukaguzi wa utekelezaji wa kampeni hiyo Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro Julai 10, 2025 ambapo amebainisha kuwa kufanyika kwa kampeni hiyo kunaweka ukomo wa kutorosha mifugo katika nchi jirani ambako wafugaji walikuwa wanaenda kutafuta masoko kwenye nchi zilizopata ithibati ya Shirika la kimataifa la Afya ya wanyama (WOAH). “Kwa hivi sasa baada ya kutangaza tu kuanza kwa kampeni hii tayari masoko ya kimataifa yameonesha dhamira ya kuhitaji Mifugo yetu hai na mazao yake na ninatamani itakapomalizika miaka 5 ya utekelezaji wa kampeni hii turejee kwa Mhe. Rais na kumuonesha namna alivyofanikiwa kubadili sekta yetu ya Mifugo” Ameongeza Mhe. Dkt. Kijaji. Akielezea ubora wa hereni za...

PWANI KUCHANJA NA KUTAMBUA MIFUGO YOTE KWA SIKU 30

Picha
Na. Omary Mtamike Uongozi wa mkoa wa Pwani umesema kuwa utatumia siku 30 pekee kuchanja na kutambuaMifugo yake badala ya miezi 2 iliyopangwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kutekeleza zoezi hilo. Ahadi hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Shaib Ndemanga ambaye pia alimwakilisha mkuu wa Mkoa huo kwenye ziara ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji iliyolenga kukagua Utekelezaji wa kampeni ya kitaifa ya Chanjo na Utambuzi wa Mifugo kwenye kwenye kijiji cha Miono Wilaya ya Chalinze. “Tunajua nyie kama Wizara mmepanga kutekeleza awamu ya kwanza ya zoezi hili kwa miezi miwili lakini nikuhakikishie Mhe. Waziri mkoa wa Pwani kwa furaha tuliyonayo na namna tulivyopokea zoezi hili tutahakikisha tunamaliza ndani ya siku 30” Amesema Mhe. Ndemanga. Akizungumza mara baada ya kushuhudia kuanza kwa utekelezaji wa kampeni hiyo mkoani Pwani, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji ameupongeza mkoa huo kwa namna walivyopokea zoezi hilo alilolitaja kama sehemu ya maono ma...