Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2025

PROF. SHEMDOE AITAKA FETA KUZALISHA WANAOJIAJIRI NA KUAJIRI WENGINE

Picha
Na. Maria Mtambalike - FETA  Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe ameitaka Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi nchini (FETA) kuandaa wahitimu watakaoweza kujiajiri na kuajiri wengine badala ya kusubiri kuajiriwa kama ilivyo hivi sasa. Prof. Shemdoe ametoa kauli hiyo wakati akifungua kikao kilichokutanisha wadau kujadili rasimu ya mitaala 5 inayohuishwa na mitaala 12 mipya iliyoandaliwa na Wakala hiyo 26 Mei, 2025 Mkoani Morogoro. “Ni lazima tubadilike katika utoaji wetu wa elimu ili kuzingatia mafunzo yanayojikita kwenye ujuzi wa vitendo zaidi ili wahitimu wetu waweze kujiajiri na baadae waajiri wengine” Amesema Prof. Shemdoe. Aidha Prof. Shemdoe ameielekeza Wakala hiyo kutengeneza mitaala itakayozalisha wataalam wanaozingatia mabadiliko ya tabia nchi kwenye utekelezaji wa shughuli za Uvuvi na ukuzaji Viumbe Maji. “Mitaala hii pia izingatie teknolojia za kisasa ikiwa ni pamoja na matumizi ya zana mpya za Uvuvi, Ukuzaji viumbe Maji lakini mwisho mitaala hii ...

BUNGE LAIDHINISHA BAJETI YA TSH. BIL.476.6 WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI

Picha
  BAJETI ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi imewasilishwa bungeni huku mafanikio lukuki yaliyopatikana kwenye  sekta za mifugo na uvuvi ndani ya kipindi cha miaka minne ya serikali ya awamu ya sita  yakibainishwa na hatua kadhaa zikitajwa kuchukuliwa na wizara kwa lengo la kuziwezesha sekta hizo muhimu kuendelea kuwa na mchango zaidi kwenye Pato la Taifa (GDP). Akiwasilisha bajeti hiyo yenye muelekeo wa kuongeza  uzalishaji na kukuza masoko ya mazao ya mifugo na uvuvi,   bungeni jijini Dodoma   Mei 23, 2025, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amebainisha mafanikio kadhaa ambayo sekta za mifugo na uvuvi zimeyapata. Dkt. Kijaji akihutubia bunge hilo alisema kuwa moja ya mafanikio makubwa ambayo wizara yake  imeyapata ndani ya miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ni  ku ongezeka k wa   bajeti ya wizara kutoka  Shilingi  Bilioni 295.5  Mwaka 2023/2024 hadi Shilingi...

WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI YAZINDUA RASMI ZOEZI LA KULINDA MAZALIA YA SAMAKI ZIWA VICTORIA

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV ◼️ Maboya 32 yawekwa katika mipaka ya Makulia ya Samaki  ◼️ Vifaranga vya Samaki 10,000 vya pandikizwa kwenye Mwalo wa Shadi Ziwa Victoria.  Nyamagana, Mwanza  Mei 20, 2025 Serikali, kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), imezindua Rasmi zoezi la kulinda Mazalia ya Samaki kwa kuweka maboya 32 kwenye mipaka ya maeneo maalumu yaliotengwa, kama alama ya kubainisha maeneo ya mazalia na makulia ya Samaki ambayo wavuvi wataweza kubaini maeneo hayo ambayo hayaruhusiwi kuvua, ikiwa ni moja ya njia ya kudhibiti Uvuvi haramu kwenye maeneo hayo maalumu yaliotengwa katika Ziwa hilo. Akizungumza katika hafla ya Uzinduzi wa Uwekaji Maboya katika Mazalia na Makulia ya Samaki yaliyotengwa, leo Mei 20, 2025 Wilayani Nyamagana Mkoani Mwanza, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Edwin Mhede amesema swala la kuweka alama katika maeneo mahususi yaliobainishwa kwa ajili ya mazalia na makulia ya samaki ni takwa la kikanuni, na maeneo haya yameb...

FETA YAZINDUA MAFUNZO YA KOZI FUPI KADA YA UJUZI WA UVUVI

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV ◼️ Vifaranga vya Samaki 35,000 vya pandikizwa kwenye vizimba na bwawa  Rorya, Mara  Mei 20, 2025 Wizara ya Mifugo na Uvuvi, kupitia Wakala wa Elimu  na Mafunzo ya Uvuvi (FETA), imezindua Mafunzo ya Kozi fupi za Uvuvi na kuboresha Miundombinu ya Kampasi hiyo ya Gabimori, ikiwa ni pamoja na kujenga Madarasa mawili kwa ajili ya Mafunzo, Miundombinu ya msingi ya vitotoleshi vya Vifaranga vya Samaki, Vizimba viwili vya kufugia Samaki, Recirculating Aquaculture System (RAS), na Birika la kunyweshea Mifugo. Akizungumza wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Miundombinu na Upandikizaji wa vifaranga vya samaki kwa ajili ya kuanza kutoa mafunzo katika Kampasi ya FETA Gabimori, leo Mei 20, 2025 Rorya - Mara, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Edwin Mhede amesema kuwa FETA inaanzisha Rasmi Mafunzo ya Kozi fupi katika Kampasi ya Gabimori ili wananchi waweze kujifunza jinsi ya kufuga Samaki kwa njia ya Vizimba na mabwawa. “Leo tunazindua Program...

WATAALAMU KUTOKA NIGERIA KUJIFUNZA UCHUMI WA BULUU TANZANIA

Picha
Na. Hamisi Hussein - WMUV, Dodoma Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Bw. Abdul Mhinte, amesema kuwa Tanzania inaendelea kutekeleza sera ya kukuza Uchumi wa Buluu kwa kutumia rasilimali zake nyingi ambazo zimekuwa chachu ya maendeleo ya uchumi huo. Bw. Mhinte ameyasema hayo leo, Mei 20, 2025, alipokuwa akiikaribisha kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara, Prof. Riziki Shemdoe,  timu ya wataalamu kutoka Taasisi ya Mafunzo ya Sera na Mipango Kitaifa ya Nigeria (NIPSS), ambayo imewasili nchini kwa ziara ya mafunzo juu ya masuala ya Uchumi wa Buluu. “Nchi yetu ina rasilimali nyingi zinazochochea maendeleo ya Uchumi wa Buluu, zikiwemo bahari, maziwa na mito, ambazo zimekuwa zikitumika kukuza na kuendeleza sekta hii muhimu,” amesema Bw. Mhinte. Ameeleza kuwa sekta ya uvuvi inatoa fursa nyingi, na kusisitiza utayari wa Wizara kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuendeleza sekta hiyo kama sehemu ya mpango mpana wa kukuza Uchumi wa Buluu. Kwa upande wake, Kiongozi wa ms...

BARAZA JIPYA LA WAFANYAKAZI LA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI LAUNDWA

Picha
 Na. Chiku Makwai – WMUV Baraza jipya la wafanyakazi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi limeundwa kwa lengo la kuwashirikisha wafanyakazi wa Wizara hiyo katika utekelezaji wa shughuli za Serikali na ushirikiano, kuishauri Wizara juu ya ufanisi wa kazi na hatua zinazofaa kuchukuliwa ili kuimarisha utoaji huduma. Akizungumza katika mkutano uliofanyika leo Mei 19, 2025 katika ukumbi wa Mabeyo – Complex jijini Dodoma Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amesema baraza hilo linapaswa kushauri Wizara juu ya mambo muhimu yanayohusu Haki, Wajibu na Maslahi ya wafanyakazi ili kuleta ufanisi na tija katika utekelezaji wa malengo ya Wizara hiyo. “tunapaswa kulitumia baraza hili kama jukwaa muhimu la kutolea maoni, kujadili masuala yanayowahusu wafanyakazi na kutafuta suluhu ya changamoto mbalimbali zinazoikabili Wizara yetu”  Ameongeza kuwa katika mwaka wa Fedha 2025/2026 Wizara imejiwekea vipaumbele ambavyo ni Kuimarisha afya ya mifugo na viumbe maji, mifumo ya utambuzi wa mifugo...

WAFUGAJI WAHIMIZWA KUMTUNZA MNYAMA PUNDA

Picha
Na. Chiku Makwai - WMUV Naibu  Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Bw. Abdul Mhinte amesema ni wajibu wa kila mfugaji punda kumtunza mnyama huyo kwani anahaki kama ilivyo kwa wanyama wengine, ikiwemo haki ya kutolala njaa, kutopata maumivu, kupata maji safi na kuwa huru dhidi ya magonjwa na kazi zinazozidi uwezo wake. Bw. Mhinte ameyasema hayo Mei 17, 2025 kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt Ashatu Kijaji wakati wa maadhimisho ya Siku ya Punda Duniani yaliyofanyika katika Kijiji cha Chambalo, Wilaya ya Chemba, mkoani Dodoma.  Aidha, Bw. Mhinte aliwasisitiza wafugaji kuhusu umuhimu wa kutambua mchango wa mnyama huyo katika maendeleo ya kiuchumi. “Punda ana haki ya kutopata majeraha au mateso wakati wa kazi, kupata mapumziko ya kutosha na kupewa hifadhi stahiki,” alisema Mhinte,  Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Mifugo, Dkt. Benezeth Lutege, amesema biashara ya punda na mazao yake ilisababisha kutoweka kwa wanyama hao barani Afrika...

MAFUNZO YA WATAALAMU WA AFYA YA MIFUGO KIMATAIFA, YAZINDULIWA

Picha
Na. Chiku MAKWAI - WMUV Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imezindua rasmi mradi wa mafunzo kwa wataalamu wa afya ya mifugo, yanayofanyika katika nchi nne za Tanzania, Botswana, Zambia na Malawi. Akizungumza leo (Mei 17, 2025) wakati wa ufunguzi wa mkutano wa mafunzo maalum kwa wataalam hao  uliofanyika katika Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe amesema mafunzo hayo yamelenga kuwapa ujuzi wa kisasa vijana, hususan wahadhiri ili waendane na hali halisi ya sekta ya ufugaji ndani na nje ya nchi. Akizungumzia juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Prof. Shemdoe amesema Serikali iinaanzisha Kampeni ya Chanjo Kitaifa kwa ajili ya magonjwa 13 sugu ya mifugo itakayozinduliwa mwaka huu. “Kampeni hiyo itaanza na magonjwa matatu, ambapo ng’ombe milioni 19, mbuzi na kondoo milioni 17, pamoja na kuku milioni 40 ...