Nav bar

Ijumaa, 9 Mei 2025

AZMA YA DKT. SAMIA KWENYE SEKTA ZA UZALISHAJI IMETIMIA-DKT KIJAJI

Na. Omary Mtamike

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amesema kuwa miaka minne ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imetekeleza kwa vitendo dhana ya kuboresha maisha ya Watanzania kupitia sekta za Uzalishaji.

Mhe. Dkt. Kijaji amesema hayo wakati wa hafla ya uzinduzi wa Hosteli ya wasichana na kumbi mbili za mihadhara kwenye Wakala ya Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo nchini (LITA) kampasi ya Mpwapwa Mei 08, 2025 mkoani Dodoma ambapo mbali na kuupongeza uongozi wa Wilaya ya chuo hicho kwa kukamilisha ujenzi wa majengo hayo kwa viwango stahiki amefurahishwa na namna wanafunzi wa chuo hicho walivyoandaliwa kuwa wataalam wazuri wa sekta ya Mifugo.

“Ni wazi kabisa yale ambayo nimejifunza kwa wanafunzi wetu kuanzia kwenye shamba lao la ng’ombe, kitotoleshi cha kuku na hatimaye kwenye kuku wenyewe yametosha kuonesha kazi aliyoamua kuifanya Daktari Samia Suluhu Hassan kwenye upande wa sekta za uzalishaji tangu alipoingia madarakani miaka minne iliyopita ambapo aliamini mbali na kuwawezesha vijana kujiajiri,  sekta hizi zitasaidia kuinua uchumi wa wananchi wote hasa wale wa kipato cha chini” Amesema Mhe. Dkt. Kijaji.

Mhe. Dkt. Kijaji ameeleza kuwa mbali na ujenzi wa majengo hayo na ukarabati wa kampasi mbalimbali za Wakala hiyo zilizogharimu bil.1.9, Serikali imeendelea kujenga na kukarabati miundombinu mingine ya Wakala hiyo ikiwa ni pamoja na kutoa shilingi milioni 168 za ukarabati wa mabweni mawili ya kampasi ya Temeke.

“Aidha kufuatia kukamilika kwa ujenzi wa miundombinu hii tumeongeza kiwango cha udahili kutoka 3574 mwaka 2021 hadi wanafunzi 4921 mwaka huu na tayari  tumepata shilingi bil. 2.05 kwa ajili ya ujenzi wa kumbi 10 za mihadhara katika kampasi za Mabuki, Mpwapwa, Morogoro na Tengeru” Ameongeza Mhe. Dkt. Kijaji.

Mbali na Ujenzi wa Majengo ya Wakala hiyo yaliyozinduliwa leo ambao umegharimu takribani kiasi cha shilingi bil. 1.6, Wakala hiyo imeanza ujenzi wa Kampasi nyingine mkoani Songwe itakayogharimu shilingi bil. 1.2 hadi kukamilika kwake.

Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Mafunzo ya Mifugo nchini (LITA) Dkt. Pius Mwambene (katikati) akimuonesha Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (kushoto) Maeneo zinakohudumia Kampasi mbalimbali za Wakala hiyo muda mfupi kabla hajazindua Hosteli ya Wasichana na kumbi mbili za mihadhara za Wakala hiyo Mei 08, 2025 Mpwapwa, Dodoma.

Mwanafunzi wa chuo cha Mafunzo ya Mifugo nchini (LITA) kampasi ya Mpwapwa Bi. Kisawa Msaye akimpa maelezo mafupi kuhusu ufugaji wa kuku Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (katikati) wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa Hosteli ya wasichana na kumbi mbili za mihadhara za Kampasi hiyo Mei 08, 2025 Mpwapwa, Dodoma. Wengine pichani ni Mtendaji Mkuu wa Wakala hiyo Dkt. Pius Mwambene (kulia), Watendaji na viongozi mbalimbali wa Wizara hiyo na Wilaya ya Mpwapwa.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (wa tatu kutoka kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Wizara hiyo, Wanafunzi na Watendaji wa Wilaya ya Mpwapwa ndani ya moja ya kumbi mbili za mihadhara alizozindua kwenye Wakala ya Mafunzo ya Mifugo nchini (LITA) kampasi ya Mpwapwa Mei 08, 2025, Dodoma.

Pichani ni jengo la hosteli ya Wasichana la “Dkt. Ashatu Kijaji” lililopo kwenye Wakala ya Mafunzo ya Mifugo nchini (LITA) kampasi ya Mpwapwa ambalo limezinduliwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji Mei 08, 2025 Mpwapwa, Dodoma.

Pichani ni jengo lenye kumbi mbili za mihadhara lililopo kwenye Wakala ya Mafunzo ya Mifugo nchini (LITA) kampasi ya Mpwapwa ambalo limezinduliwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji Mei 08, 2025 Mpwapwa, Dodoma.


Alhamisi, 8 Mei 2025

SERIKALI YAIDHINISHA USAMBAZWAJI WA HERENI ZA KIELEKTRONIKI KWA WAFUGAJI NCHINI

Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imesaini mkataba unaoidhinisha usambazwaji wa hereni za kieletroniki zitakazotumika kwenye utambuzi wa Mifugo nchini.

Akizungumza katika hafla hiyo fupi iliyofanyika kwenye Ofisi za Wizara hiyo jijini Dodoma Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe amewataka wasambazaji hao kuhakikisha taarifa zilizopo kwenye hereni hizo zinakuwa msaada kwa mfugaji pindi anapohitaji kufahamu lolote kuhusu Mifugo yake.

“Muwe tayari wakati wote kutoa elimu kwa wafugaji juu ya namna hereni hizo zinavyofanya kazi ili kuwawezesha wafugaji uelewa wa kutosha kuhusu vifaa hivyo,Amesema Prof. Shemdoe.

Aidha Prof. Shemdoe amebainisha kuwa wafugaji hawatatozwa gharama yoyote wakati wa zoezi la uwekaji hereni hizo baada ya Serikali kugharamia zoezi hilo.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo anayeshughulikia sekta ya Mifugo Ndg. Abdul Mhinte amewataka wazabuni hao kuhamasisha wafugaji kuweka hereni kwenye mifugo yao ili uwe utamaduni kwa wafugaji hao kufanya hivyo hata kusipokuwa na msukumo kutoka Serikalini.

Kwa upande wa wazabuni hao wameihakikishia Wizara kuzalisha na kusambaza hereni zenye viwango na sifa stahiki ili ziweze kuwasaidia wafugaji wakati wowote wanapohitaji kupata taarifa za Mifugo yao.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe (katikati) na Wazabuni walioidhinishwa kusambaza hereni za kielektroniki wakisaini mikataba ya usambazaji wa hereni hizo zitakazotumika kwenye zoezi la Utambuzi wa Mifugo nchini leo Mei 2, 2025 jijini Dodoma. Wanaoshuhudia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo anayeshughulikia Mifugo Ndg. Abdul Mhinte (kushoto), Mwanasheria wa Wizara Bi. Cresensia Lubuva (kushoto nyuma) na Mwanasheria wa Kampuni hizo Bw. Nicodemus Msika.


MADAKTARI WATOA HUDUMA YA MATIBABU KWA WANYAMA BURE

◼️ Ni katika kuadhimisha siku ya Veterinari Duniani

Katika sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Veterinari Duniani, Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na chama cha madaktari wa wanyama Tanzania (TVA) wametoa huduma za afya ya wanyama katika Halmashauri za Wilaya na Mji Mbulu, Halmashauri ya Wilaya ya Hanang, Halmashauri za Wilaya na Mji Babati.

Huduma hizo zimeanza leo Aprili 24-26, 2025 ambapo mbali na huduma hiyo ya kukinga wanyama dhidi ya magonjwa  wameendelea kutoa elimu kwa wafugaji hao kuhusu ugonjwa wa kichaa cha mbwa na huduma hizo zote zinatolewa bila malipo katika maeneo mbalimbali yaliyo ainishwa. 

Pamoja na shughuli hizo wataam hao wameandaa maonyesho makubwa yanayo endelea katika viwanja vya Tanzanite Kwaraa mjini Babati.


Ijumaa, 2 Mei 2025

SERIKALI YAKABIDHI GARI LA UBARIDI KWA CHAMA CHA USHIRIKA WA UVUVI BUKASIGA

Na Hamisi Hussein, WMUV - Dodoma.

Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekabidhi gari la ubaridi kwa ajili ya kusafirishia mazao ya uvuvi kwa Chama cha Ushirika wa Uvuvi BUKASIGA Ltd kilichopo  Wilaya ya Ukerewe Jijini Mwanza  ikiwa ni utekelezaji wa Mpango  wa kuboresha usimamizi wa uvuvi, ukuzaji wa viumbe maji, uchumi wa buluu na biashara katika ukanda wa SADC (PROFISHBLUE).

Akikabidhi gari hilo kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, leo Aprili 30, 2025 katika ofisi za Wizara zilizopo Mtumba jijini Dodoma, Naibu Katibu Mkuu (Uvuvi) Dkt. Edwin Mhede amesema serikali inaendelea kuwawezesha wananchi wanaojihusisha na mnyororo wa thamani wa sekta ya uvuvi ikiwemo chama cha  Ushirika wa uvuvi BUKASIGA 

”Serikali imetumia rasilimali zake kuhakikisha BUKASIGA Ltd inasimama, ndio ilisaidiwa na serikali wakati wa kuingia kwenye mchakato shindani wa mradi wa Profishblue ambao unatumia fedha za serikali kupitia  Benki ya Maendeleo ya Africa (ADB) mradi unaolenga kuongeza ubora wa mazao na kupunguza upotevu wa mazao ya uvuvi, kwahiyo gari hili likafanye kazi iliyokusudiwa na likasafirishe Samaki tu”  amesema Dkt. Mhede.

Aidha Dkt. Mhede amemwagiza Kaimu  Mkurugenzi wa Uvuvi Dkt. Baraka Sekadende  kukisaidia Chama cha Ushirika wa Uvuvi BUKASIGA  kufanya usajili gari hilo  pamoja na kuliweka chapa ’branding’ zitakazoonesha usafirishaji wa mazao ya Samaki ili lisitumike kwa matumizi mengine.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi  wa Uvuvi Dkt. Baraka Sekadende akizungumza  kwenye hafla hiyo amesema kuanzia mwaka 2019 wizara imefanikiwa kuanzisha vyama vinne vya ushirika wa uvuvi ikiwemo  cha BUKASIGA Ltd ambacho ndicho kimekabidhiwa  gari hilo litakalopunguza upotevu wa mazao ya uvuvi .

Naye Mwakilishi wa sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza ambaye ni Mrajisi wa Ushirika mkoani humo Bi. Hilda Boniface ameshukuru kwa jitihada zinazofanywa na serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuvisaidia vyama vya ushirika kukua kupitia sekta ya uvuvi na kutoa wito kwa vyama vyote vya ushirika kuchangamkia fursa zinazotolewa na serikali, huku Mwenyekiti wa chama cha Ushirika  BUKASIGA Ltd Bw. Erasto Majura akiishukuru serikali  na kuahidi kulisimamia gari hilo liweze kuwanufaisha wanachama na jamii kwa ujumla.

Gari ya ubaridi iliyokabidhiwa kwa chama cha ushirika wa Uvuvi cha Bukasiga ina thamani ya dola za kimarekani 87,230.99, pia gali hilo linakadiriwa  kuhifadhi  samaki kwa muda wa mwaka mmoja ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa PROFISHBLUE unaotekelezwa na nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika – SADC.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Edwin Mhede ( Kushoto) kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akimkabidhi  Kadi ya Gari la Ubaridi litakalotumika kusafirishia mazao ya Uvuvi ya chama cha Ushirika wa Uvuvi BUKASIGA LTD Mwenyekiti wa Chama hicho Bw. Erasto Majura( Kulia)  wakati wa hafla ya makabidhiano ya Gari la Ubaridi kwenye ofisi za Wizara zilizopo Mtumba Jijini Dodoma, Aprili 30, 2025.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Edwin Mhede ( Wa tatu, kulia) kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi akizungumza na Wanachama wa Ushirika wa Uvuvi BUKASIGA LTD  pamoja na baadhi ya Wataalamu kutoka wizarani wakati wa hafla ya makabidhiano ya Gari la Ubaridi kwenye ofisi za Wizara zilizopo Mtumba Jijini Dodoma, Aprili 30, 2025.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Edwin Mhede ( Kushoto) kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akikagua Gari hilo la Ubaridi litakalotumika kusafirishia mazao ya Uvuvi kabla ya kukabidhi kwa chama cha Ushirika wa Uvuvi BUKASIGA Ltd, hafla iliyofanyika kwenye ofisi za Wizara zilizopo Mtumba Jijini Dodoma, Aprili 30, 2025.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Edwin Mhede ( wa kwanza, kulia) kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akitoa Maelekezo kwa Wataalamu wa Wizara juu ya usajili wa Gari la Ubaridi litakalotumika kusafirishia mazao ya Uvuvi ya chama cha Ushirika wa Uvuvi BUKASIGA LTD wakati wa hafla ya makabidhiano ya Gari la Ubaridi kwenye ofisi za Wizara zilizopo Mtumba Jijini Dodoma, Aprili 30, 2025.

Gari la Ubaridi litakalotumika kusafirishia mazao ya Uvuvi  ya Chama cha Ushirika wa Uvuvi BUKASIGA LTD limekabidhiwa na Naibu Katibu Mkuu( Uvuvi) Dkt. Edwin Mhede Kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji ikiwa ni utekelezaji wa mradi wa PROFISHBLUE hafla ya makabidhiano imefanyika ofisi za Wizara zilizopo Mtumba Jijini Dodoma, Aprili 30, 2025.








Jumanne, 22 Aprili 2025

SERIKALI KUENDELEA KUWEZESHA UFUGAJI WA KISASA

Na Hamisi Hussein - WMUV, Mwanza.

⬛️ Mhe. Mnyeti akikabidhi Mitamba 10 ya Maziwa kwa UWAMATA

Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi itaendelea kuwezesha ufugaji wa kisasa ili kuongeza tija katika uzalishaji na kukuza uchumi wa wafugaji nchini.

Hayo yameelezwa leo Aprili 19, 2025 na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alaxender Mnyeti wakati wa kukabidhi ng'ombe 10 wa Maziwa kwa kikundi cha Umoja wa Mapadri Tanzania (UWAMATA) hafla iliyofanyika katika Shamba la Uzalishaji Mifugo lililopo Misungwi mkoani Mwanza.

Mhe. Mnyeti amesema lengo la serikali nikuona inawezesha ufugaji wa kisasa kwa kuhimiza wafugaji kuwa na mifugo michache yenye tija itakayotoa mazao bora yanayokidhi  ushindani wa masoko.

" Mhe. Rais wetu anataka kuona ufugaji wa Kisasa unakuwa na tija kwa wafugaji na sisi Wizara tunaendelea kuhimiza ufugaji wa kisasa ambapo tumekuwa tukihamasisha ulimaji wa malisho ambayo yametajwa na wataalam wetu kuwa yanaprotini nyingi" alisema Mhe. Mnyeti.

Kuhusu ng'ombe wa maziwa (Mitamba) waliotolewa na serikali kwa Kikundi cha Umoja wa Mapadri Tanzania  (UWAMATA) Mhe. Naibu Waziri Mnyeti amesema zoezi la upandikizaji wa ng'ombe hao limefanywa na Wataalam wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ili kuwa na uhakika wa uzalishaji wa ng'ombe hao.

Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa Mapadri Tanzania (UWAMATA) Padri George Nzungu ameishukuru serikali kwa kuwapatia ng'ombe hao kwani wataleta tija ya uzalishaji wa maziwa na kuahidi kuwa balozi wa ufugaji wa kisasa kwa wananchi wanaozunguka eneo lao.

Aidha Mkurugenzi Msaidi wa Idara ya Uzalishaji na Masoko Dkt . Yeremia Sanka amesema ng'ombe hao waliopatikana kutokana na upandikizaji wa mbegu za madume halisi ya maziwa (Friesian) na majike ya kienyeji aina ya Boran na  watazalisha kati ya lita 8  hadi 12 kwa siku tofauti na ng'ombe wa asili ambaye anatoa maziwa lita 1.5 hadi 3 tu kwa siku.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti (Mwenye Fimbo) akiwa Kwenye Picha ya Pamoja  na Mapadri wakati wa Makabidhiano ya Majike 10 ya maziwa kwenye Shamba la uzalishaji Mifugo Mabuki, Mwanza Aprili 19, 2025.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti  akizungumza na Mapadri waliopo kwenye Umoja wa Mapadri Tanzania (UWAMATA) wakati wa makabidhiano ya Majike 10  ya maziwa yenye mimba kwenye Shamba la uzalishaji Mifugo Mabuki, Mwanza Aprili 19, 2025.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti (Kulia) akimkabidhi Mwongozo wa ufugaji wa ng'ombe wa Maziwa Padri Samweli Massawe(Katikati) wakati wa Makabidhiano ya Majike 10 ya maziwa kwenye Shamba la uzalishaji Mifugo Mabuki, Mwanza Aprili 19, 2025.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti (Kulia) akimkabidhi Boski la Dawa ya kuongeshea ng'ombe wa Maziwa Padri Samweli Massawe wakati wa Makabidhiano ya Majike 10 ya maziwa kwenye Shamba la uzalishaji Mifugo Mabuki, Mwanza Aprili 19, 2025.

Mitamba ya Maziwa ilitokana na madume halisi ya maziwa (Friesian) na Majike ya asili aina ya Boran ikichunga katika Shamba la Mifugo Mabuki kabla la hafla ya makabidhiano baina ya Naibu Waziri  wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti  na Umoja wa Mapadri Tanzania UWAMATA hafla iliyofanyika Shamba la uzalishaji Mifugo Mabuki lililopo Misungwi, Mwanza Aprili 19, 2025.



 




Jumatano, 16 Aprili 2025

TDB YAHIMIZWA KUENDELEA KUSAJILI WADAU WA TASNIA YA MAZIWA

Na. Stanley Brayton, WMUV 

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Ndg. Abdul Mhinte ameihimiza Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB) kuendelea kuwatambua na kuwasajili wadau wa Tasnia ya Maziwa ili kuongeza Uzalishaji wa maziwa nchini.

Ndg. Mhinte amesema hayo wakati akizungumza na Watumishi wa TDB katika Kikao kazi kinachofanyika kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Aprili 16, 2025.

"kama wadau wa Tasnia ya Maziwa hawafahamiki na hawajasajiliwa, ni ngumu sana kufikia Malengo na kuzalisha Maziwa kwa wingi, kwani wanahitaji kutatuliwa changamoto zao, ikiwemo za Masoko ya Maziwa hayo" amesema Ndg. Mhinte 

Vilevile, Ndg. Mhinte amesema kuwa wadau wa Tasnia ya Maziwa wapo sehemu mbalimbali nchini, na ni vyema Vituo vya ukusanyaji Maziwa vikarekebishwa na kuongezwa, ikiwa pamoja na Usimamizi  mzuri ili Maziwa yakusanywe kwa wingi.

Ndg. Mhinte, pia amehimiza Bodi kubuni Miradi mbalimbali kama ya Bar za Maziwa ili kuhakikisha Watumishi wanayapata kiurahisi na kuongeza Pato la Taifa.

Naye, Msajili wa Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB), Prof. George Msalya amesema kuwa leo wamekuwa na Kikao na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi na kujadili Maendeleo ya Taasisi yao hususani Maendeleo ya Tasnia ya Maziwa hapa nchini pamoja na utendaji kiujumla.

"tumepokea maagizo yote tuliopewa na Naibu Katibu Mkuu ambayo yatatujenga na kuongeza hali ya utendaji kazi katika kutekeleza majukumu yetu ya kila siku katika Tasnia ya Maziwa" amesema Prof. Msalya 

Halikadhalika, Prof. Msalya amesema kwa sasa Maziwa yanakusanywa katika vituo 258 maalum vya kukusanyia, na wataendelea kuongeza vituo vingine pamoja na Miradi mingine kama Bar za Maziwa ili kuhakikisha Maziwa yanapatikana kwa wingi nchini.

Prof. Msalya amebainisha kuwa kwa sasa Takwimu zinaonyesha kila Mtanzania mmoja anatumia takribani Lita 67.5 kwa mwaka, ila viwango vilivyowekwa Kimataifa kwa mtu mmoja kunywa Maziwa kwa mwaka ni Lita 200.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Ndg. Abdul Mhinte, akihutubia Watumishi wa Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB), katika Kikao kazi cha Watumishi wa Bodi hiyo, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma (Mkapa House), Aprili 16, 2025, Dodoma

Msajili wa Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB), Prof. George Msalya, akizungumza na watumishi  wa Bodi hiyo, katika Kikao kazi cha Watumishi wa Bodi hiyo, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma (Mkapa House), Aprili 16, 2025, Dodoma

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Utumishi  na Utawala - Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB), Bi. Victoria Masanja, akielezea kuhusu umuhimu wa utoaji Taarifa kwa Utumishi, katika  Kikao kazi cha Watumishi wa Bodi hiyo, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma (Mkapa House), Aprili 16, 2025, Dodoma

Afisa Matekelezo Mkuu - Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Watumishi wa Umma (PSSSF), Bw. Juma Milinga, akielezea jinsi PSSSF inavyofanya kazi na Taratibu za kuomba Mafao kwa Mtumishi, ni katika Kikao kazi cha Watumishi wa Bodi hiyo, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma (Mkapa House), Aprili 16, 2025, Dodoma

Meneja Fedha Utawala na Rasilimali Watu - Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB), Bw. Walter Vasolela, akichangia  hoja katika Kikao kazi cha Watumishi wa Bodi hiyo, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma (Mkapa House), Aprili 16, 2025, Dodoma

Mchumi - Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB), Bw. Davis Wambura, akifanya mapitio ya Mpango Mkakati wa Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB) ya mwaka 2025/26 na kuelezea Utekelezaji wa Bajeti ya Bodi hiyo kwa Mwaka wa Fedha wa 2024/25, katika Kikao kazi cha Watumishi wa Bodi hiyo, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma (Mkapa House), Aprili 16, 2025, Dodoma

Afisa Mteknolojia  wa Chakula - Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB), Bi. Neema Moshi, akielezea umuhimu wa Ushirikishwaji wa Idara ya Sheria katika kuwawajibisha wadau wa Maziwa wanaoshindwa kufuata Taratibu za Kisheria katika Tasnia hiyo na umuhimu wa ushirikiano katika utendaji kazi, ni katika Kikao kazi cha Watumishi wa Bodi hiyo, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma (Mkapa House), Aprili 16, 2025, Dodoma

Afisa Mteknolojia wa Chakula - Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB), Bw. Francisco Juma, akielezea kuhusu umuhimu wa kubuni vyanzo vya Mapato na kuweka Mikakati mizuri ya Ukusanyaji Mapato katika Bodi na swala la ushirikishwaji wa Watumishi katika kupanga Bajeti kwa kukaa pamoja na kujadili kipi Cha kufanya kwa Mwaka wa Fedha ujao, ni katika Kikao kazi cha Watumishi wa Bodi hiyo, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma (Mkapa House), Aprili 16, 2025, Dodoma

Mhasibu - Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB), Bw. Christian Makawa, akielezea umuhimu wa kufungua Kituo cha Taarifa  za Maziwa (Information Center) ili wadau wa Tasnia ya  Maziwa wapate Habari zinazohusu Maziwa, ni katika Kikao kazi cha Watumishi wa Bodi hiyo, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma (Mkapa House), Aprili 16, 2025, Dodoma

Picha ni Watumishi wa Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB), wakiwa katika Kikao kazi, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma (Mkapa House), Aprili 16, 2025, Dodoma

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Ndg. Abdul Mhinte (aliyesimama katikati mstari wa mbele), akiwa kwenye picha ya pamoja na Watumishi wa Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB), baada ya Kikao kazi cha Watumishi wa Bodi hiyo, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma (Mkapa House), Aprili 16, 2025, Dodoma


​KONGAMANO LA KITAIFA LA NGURUWE KUFANYIKA TANZANIA

Na. Chiku Makwai (MUV). Dodoma

Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi ikishirikiana na chama cha wafugaji wa Nguruwe Tanzania (TAPIFA) imepata fursa ya kuwa mwenyeji wa kongamano la kimataifa la ufugaji wa nguruwe litakalo fanyika Septemba 11-13, 2025 jijini Dar es Salaam.

Hayo yamesemwa leo Aprili 16, 2025 na Naibu Waziri, Wizara ya Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti Wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari Uliofanyika katika Ukumbi uliopo jengo la NBC jijini Dodoma.

Mhe. Mnyeti amesema kuwa kongamano hilo linatarajiwa kuhudhuriwa na washiriki takribani 2000 kutoka mataifa mbalimbali barani Afrika wakiwemo Viongozi wa Serikali na Wizara za kisekta, Wawekezaji wa ndani na nje ya nchi, Vijana na Wanawake, Wanataaluma, Wadau wa Maendeleo, Wafugaji na Wafanyabiashara katika mnyororo wa thamani wa Nguruwe.

Aidha, ameongeza kuwa kongamano hilo litaambatana na Mafunzo kutoka kwa wataalam na Wadau wa Maendeleo katika tasnia ya Nguruwe, pia washiriki kufanya majadiliano ya kibiashara na kuzitambua fursa zilizopo Kitaifa, Kikanda na Kimataifa pamoja na kutembelea uwandani kwa wadau kujionea namna ufugaji wa kisasa wa Nguruwe unavyofanyika.

Mhe. Mnyeti amebainisha kuwa ufugaji wa Nguruwe unaendana na malengo ya nchi katika kuhimiza maendeleo ya sekta ya mifugo ili kukuza uchumi wa nchi pamoja na kuongeza thamani ya bidhaa zinazotokana na Nguruwe.



Jumanne, 15 Aprili 2025

WAFUGAJI WAHIMIZWA KUPANDA MALISHO YA MIFUGO

Na. Stanley Brayton, WMUV - Dodoma

◼️Waelezewa athari za kulisha Mifugo katika maeneo ya Hifadhi za Misitu.

Naibu Katibu Mkuu Wizara  ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Ndg. Abdul Mhinte, amewataka wafugaji Wilayani Bahi na Chamwino kupanda Malisho kwa ajili ya Mifugo ili kuepukana na changamoto za kukosa Malisho ya Mifugo.

Akizungumza katika Kikao na Wafugaji cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika leo Aprili 15, 2025, Mkoani Dodoma, katika Kitongoji cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji cha Mayamaya, Wilaya ni Bahi, Ndg. Mhinte, amesema yapo maeneo muhimu ya Malisho ambayo yametengwa na Serikali ili kutatua changamoto za Malisho.

"yapo maeneo ambayo yametengwa kwa ajili ya Malisho japo yanapungua kadri Mifugo inavyozidi kuongezeka, na ni muhimu kuhakikisha kila mfugaji anapanda Malisho kwa ajili ya Mifugo yake" amesema Ndg. Mhite 

Vilevile, Ndg. Mhite amebainisha kuwa maeneo ya Malisho yanapungua kadri Mifugo na watu wanavyoongezeka, kiasi cha kwamba kunapelekea Misitu na Malisho kupungua au kutoweka kabisa.

Pia, Ndg. Mhinte ametolea ufafanuzi kuhusu athari za kulisha Mifugo katika maeneo ya Hifadhi ya Misitu, ikiwa ni pamoja na kuharibu Hifadhi hiyo na hatimaye kuamia katika Hifadhi zingine na kuziharibu na mwishowe kukosa Malisho kabisa pamoja na kuharibu Hifadhi hizo.

Ndg. Mhinte amesema kuwa Biashara ya kupanda Malisho imekuwa kama Dhahabu na hii ndio itakayosaidia wafugaji wengi katika kulisha Mifugo yao.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Maeneo ya Malisho na Rasilimali za vyakula za Mifugo. Dkt. Asimwe Rwiguza, amesema kwa sasa Serikali haitegemei Malisho ya asili kwa sababu haitoshelezi idadi ya Mifugo ambayo tunayo hapa nchini.

Dkt. Rwiguza amefafanua kuwa kwa sasa kuna namna ya kukabiliana na changamoto za Malisho, ikiwa ni pamoja na kulima Malisho, na ndio maana Serikali imetoa maeneo maalum kwa ajili ya kupanda Malisho na inaendelea kutoa mbegu hizo za Malisho na kutoa elimu namna ya kupanda hizo mbegu ili kuhakikisha kila mfugaji anakuwa nazo na anapandikiza katika eneo lake.

Akizungumza kwa niaba ya wafugaji wote, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wafugaji Tanzania (CCWT), Bw. Kusundwa Wamalwa amesema zipo changamoto nyingi zinazowakumba wafugaji wengi hususan wa hapa Wilaya ya Bahi na Chamwino, ikiwemo Maji, Malisho na Masoko, kwa hiyo ni vyema Serikali  ikaangalia ni jinsi gani itaweza kutatua changamoto zinazowakabili wafugaji hao 

Naye, Kamanda wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Kanda ya Kati ambaye ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Bw. Mathew Kiondo amesema miaka ya nyuma TFS ilitoa Hekta 2000 kwa wafugaji, ila kutokana na ongezeko la watu limepelekea Mahitaji ya Malisho kuwa makubwa kutokana na idadi kubwa ya watu na Mifugo, kwa hiyo wao kama TFS wataangalia ni jinsi gani wataweza kufanya ili kunasua wafugaji na changamoto ya uhaba wa maji kupitia Mfuko wa Kusaidia Jamii (CSR), ili kuwatengenezea Miundombinu ya maji kutoka kwenye Hifadhi ya Msitu wa Chenene kwenda kwenye maeneo yao ya Ufugaji.

Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Ndg. Abdul  Mhinte, akizungumza na Wafugaji wa Wilaya ya Chamwino na Bahi katika kikao chake na Wafugaji hao cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika katika Kitongoji cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji cha Mayamaya, Wilayani Bahi, Dodoma, Aprili 15, 2025.

Katibu Tawala Msaidizi - Sekta za Uchumi Mkoa wa Dodoma, Bi. Aziza Mumba, akizungumza na Wafugaji na kuelezea umuhimu wa Sekta ya Mifugo katika kuchangia Pato la Taifa, katika Kikao na Wafugaji cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika katika Kitongoji cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji Cha Mayamaya, Aprili 15, 2025, Bahi - Dodoma.

MKurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Maeneo ya Malisho na Rasilimali za vyakula za Mifugo. Dkt. Asimwe Rwiguza, akitoa ufafanuzi kwa wafugaji juu ya umuhimu wa kupanda na Malisho kwa ajili ya Mifugo ili kutatua changamoto zao, katika Kikao na Wafugaji cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika katika Kitongoji cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji Cha Mayamaya, Aprili 15, 2025, Bahi - Dodoma.

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wafugaji Tanzania (CCWT), Bw. Kusundwa Wamalwa, akimuelezea Naibu Katibu  Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), changamoto wanazokumbana nazo wafugaji nchi ikiwemo Maji, Malisho na Masoko, katika Kikao na Wafugaji cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika katika Kitongoji Cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji cha Mayamaya, Aprili 15, 2025, Bahi - Dodoma.

Kamanda wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Kanda ya Kati ambaye ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Bw. Mathew Kiondo, akiwaelezea wafugaji umuhimu wa Hifadhi ya Msitu wa Chenene Mashariki na Magharibi ambao umeingia kwenye Halmashauri zote mbili za Bahi na Chamwino na kubainisha jinsi watakavyozitatua changamoto  za wafugaji katika Malisho na maji, katika Kikao na Wafugaji cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika katika Kitongoji Cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji cha Mayamaya, Aprili 15, 2025, Bahi - Dodoma.

Mfugaji, Bw. Anthony Makaka, akiiomba Serikali kuweka utaratibu wa kupata Malisho ili kutatua changamoto zao ikiwa pamoja na kuwapatia mabwawa kwa ajili ya Mifugo na matumizi yao binafsi, katika Kikao na Wafugaji cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika katika Kitongoji Cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji Cha Mayamaya, Aprili 15, 2025, Bahi - Dodoma.

Mfugaji, Bw. Manimba oloya, akielekeza  jinsi Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) wanavyokamata Mifugo yao wakati wanapoipeleka kwenye Malisho katika Hifadhi ya Msitu wa Chenene kutokana na kutoandaliwa sehemu za Malisho na kuwapatia elimu ya kutosha, katika Kikao na Wafugaji cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika katika Kitongoji Cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji Cha Mayamaya, Aprili 15, 2025, Bahi - Dodoma.

Mfugaji, Bi. Kafutuku Kipara, akielezea changamoto alizokutana nazo za kuchukuliwa maeneo yake ya kufugia, katika Kikao na Wafugaji cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika katika Kitongoji Cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji Cha Mayamaya, Aprili 15, 2025, Bahi - Dodoma.

Mfugaji, Bi. Katarina Garabuu, akielezea changamoto anazokumbana nazo akienda katika Hifadhi ya Msitu wa Chenene katika kutafuta Maji kwa ajili ya Mifugo, katika Kikao na Wafugaji cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika katika Kitongoji Cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji Cha Mayamaya, Aprili 15, 2025, Bahi - Dodoma.
Mfugaji, Bw. Tadayo Sembuche, akilalamikia faini kubwa wanazotozwa na kunyang'anywa Mifugo baada ya kuingia Mifugo hiyo katika Hifadhi ya Msitu wa Chenene, katika Kikao na Wafugaji cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika katika Kitongoji Cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji Cha Mayamaya, Aprili 15, 2025, Bahi - Dodoma.

Picha ni baadhi ya wafugaji, wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Ndg. Abdul  Mhinte (hayupo pichani), akielezea kuhusu, katika Kikao chake na Wafugaji hao cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika Mtungutu Kijiji cha Mayamaya kata ya Zanka, Aprili 15, 2025, Bahi - Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Ndg. Abdul  Mhinte (waliokaa katikati), akiwa kwenye picha ya pamoja na Wafugaji wa Wilaya ya Chamwino na Bahi, baada ya Kikao chake na Wafugaji hao cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika Mtungutu Kijiji cha Mayamaya kata ya Zanka, Aprili 15, 2025, Bahi - Dodoma.






























DKT. MHINA AWATAKA WATUMISHI KUZINGATIA WELEDI, UAMINIFU NA WAJIBU

Na. Chiku Makwai (WMUV). Dodoma

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Mhina amewataka watumishi wa Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB) kuzingatia weledi, uaminifu na wajibu katika kutekeleza majukumu yao.

Ameyasema hayo Aprili 15, 2025 wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha  menejimenti pamoja na watumishi wa bodi hiyo kilichofanyika katika moja ya ukumbi ziliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Dodoma. 

Aidha,  Dkt Mhina ameipongeza TDB kwa kuendelea kupiga hatua katika utoaji huduma zilizo bora na amewasisitiza kuwa ili kupata maendeleo ni wajibu wa kila mtumishi kufanya kazi kwa bidii. 

Kwa upande wake Msajili Mkuu wa TDB Prof. George Msalya amesema kuwa Tasnia ya Maziwa inazidi kukua nchini na mpaka sasa kuna zaidi ya viwanda 152 vya uchakataji maziwa.

Vile vile ameongeza kuwa ipo mipango mbalimbali inayoandaliwa na kuratibiwa na bodi hiyo itakayolenga kuhamasisha unywaji maziwa nchini pamoja na manufaa yake.

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Mhina akizungumza jambo wakati wa kikao kazi cha Menejimenti pamoja na watumishi wote wa Taasisi ya Bodi ya Maziwa Tanzania kilichofanyika Aprili 15, 2025 jijini Dodoma.

Msajili wa Taasisi ya Bodi ya Maziwa nchini Prof. George Msalya akichangia jambo wakati wa kikao kazi hicho kilichofanyika Aprili 15, 2025 jijini Dodoma.

Sehemu ya Watumishi wa Taasisi ya Bodi ya Maziwa nchini walioshiriki katika kikaokazi cha Menejimenti pamoja na watumishi wake kilichofanyika Aprili 15, 2025 jijini Dodoma.






SHEMDOE ABAINISHA FURSA ZA MALISHO YA MIFUGO

Na. Omary Mtamike

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe amewataka wafugaji nchini kuendelea kutenga maeneo ya kuzalisha malisho ya mifugo yao ili waendelee kuboresha afya za wanyama na kujipatia kipato baada ya kuyauza.

Prof. Shemdoe amesema hayo Aprili 14,2025 wakati akifungua kikao cha wataalam wa malisho ya Mifugo kilichofanyika mkoani Morogoro ambapo ametoa rai kwa vijana kuchangamkia fursa hiyo kama wanavyofanya kwenye shughuli nyingine za kiuchumi.

“Tuwawezeshe vijana waanzishe mashamba ya kulima malisho kwa sababu nina uhakika masoko yapo na nina mfano wa mtu mmoja hapa Pwani yeye kila mwaka anauza tani nyingi za malisho na hana biashara nyingine zaidi ya hiyo” Ameongeza Prof. Shemdoe.

Aidha katika hatua ya utekelezaji wa maazimio ya kikao kilichopita cha wataalam hao, Prof. Shemdoe amesema Wizara yake imeendelea kuajiri vijana wengi wanaotokana na shahada ya nyanda za malisho huku pia wakiendelea kutoa elimu kuhusu chakula stahiki kwa mifugo.

Akizungumza awali kabla ya kumkaribisha Prof. Shemdoe, Mwenyekiti wa chama hicho Prof. Ismail Selemani ameishukuru Wizara kwa kufanyia kazi baadhi ya maazimio ya wataalam hao ikiwa ni pamoja na kuboresha sheria ya Maeneo ya Malisho na rasilimali za vyakula vya Mifugo namba 180 ya mwaka 2010 na kuendelea kutenga maeneo ya malisho na uanzishwaji wa mashamba darasa ya malisho hayo.

Akigusia fursa inayotokana na malisho Visiwani Zanzibar, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo visiwani humo Dkt. Abdultwalib Suleiman amesema kuwa wafugaji waliopo huko wamekuwa na changamoto ya uzalishaji wa malisho kutokana na sehemu kubwa ya visiwa hivyo kuzungukwa na majengo na miundombinu mbalimbali hivyo amewataka wazalishaji wa malisho ya Mifugo kuzalisha malisho ya kutosha na kuyapeleka Zanzibar.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe akitoa hotuba ya ufunguzi wa kikao cha Wataalam wa Malisho nchini kilichofanyika Aprili 14, 2025 mkoani Morogoro.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe akimkabidhi zawadi ya cheti cha Andiko bora la biashara ya Mifugo Mwanafunzi Laurian Jackline Josephat kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo wakati wa kikao cha Wataalam wa Malisho ya Mifugo kilichofanyika mkoani Morogoro  Aprili 14, 2025.

Msajili wa Bodi ya Maziwa nchini Prof. George Msalya (kulia) akiratibu kikao cha Wataalam wa malisho ya Mifugo nchini kilichofanyika Aprili 14, 2025 mkoani Morogoro.