ULEGA AWATAKA WAFUGAJI KUFUGA KIBIASHARA
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amewataka Wafugaji kuachana na tabia ya kufuga kuku kwa mazoea badala yake wafuge kibiashara ili kujikwamua kiuchumi. Naibu waziri amesema hayo Septemba 21 leo, wakati akifungua mafunzo ya siku moja ya wafugaji wa kuku Mkoa wa Dar es Salaam. Wafugaji hao wametoka wilaya za Ilala, Kinondoni, Kigamboni, Temeke na Ubungo. Alieleza Ulega ni watu wachache wanaofuga kuku kibiashara, lakini waliobaki wanafanya shughuli kama sehemu ya maisha yao, hali inayosababisha kutofanikisha malengo ya kukuza uchumi. “Nataka mfuge kibiashara, hatutaki mfuge kuku kimazoea. Watu watambue ufugaji kuku ni biashara kama zingine na ni fursa ya kujikwamua kimaisha,”amesema Ulega Amesema ufugaji wa kuku sehemu mojawapo itakayowakomboa wanawake na vijana kuondokana na changamoto ya ajira ambayo imekuwa kilio kwa watu mbalimbali. Ulega amesema nyama ya kuku inapendwa kila mahali na kila mtu...