Nav bar

Jumamosi, 6 Desemba 2025

DKT. BASHIRU AITAKA TVLA KUTOA HUDUMA ZENYE UBORA KWA WAFUGAJI

Na. Daudi Nyingo Dar Es Salaam.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (Mb) amewataka watumishi wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) kutoa huduma zenye ubora, ufanisi pamoja na zinazotolewa kwa kasi inayotosheleza kwa kuzingatia heshima na uwajibikaji.

Dkt. Bashiru ameyasema hayo Desemba 06, 2025 alipotembelea Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) iliyopo Temeke Dar Es Salaam akiongozana na Naibu Waziri Mhe. Ng'wasi Damas Kamani (Mb) pamoja na Katibu Mkuu Bi. Agnes Meena kwa lengo la kujionea shughuli  mbalimbali za kimaabara zinazofanywa na TVLA pamoja na kuongea na watumishi ili kutoa mwelekeo wa malengo ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Muendelee kutoa huduma kwa umma kwa kuzingatia misingi ya haki, heshima, utu, uwajibikaji, kasi pamoja na uzalendo. Nimekuja kuwaahidi utendaji uliotukuka; niko hapa kuwaambia kwamba wizara na uongozi wake wapo tayari kushirikiana nanyi,” alisema Dkt. Bashiru.

“Tupo tayari kumuunga mkono Mhe. Rais ili atakapomaliza muhula wake wa uongozi aache tabasamu la utu kwa Watanzania kupitia wizara ya Mifugo na Uvuvi,” aliongeza.

Sambamba na hayo, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru aliwapongeza watumishi wa TVLA kwa kazi kubwa wanayoifanya kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi, na amewataka kudumisha mazuri yote yaliyopo kabla ya kuanzisha mapya, kwani amekuja kufanya mabadiliko mapya lakini kwa kuanzia na misingi mizuri aliyokuta. Alisema msingi wa maendeleo anayoyataka ili taifa liwe imara, lenye uchumi shirikishi na unaojitegemea, ni kuendeleza rasilimali watu.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng'wasi Damas Kamani (Mb) alisema kuwa vijana wana jukumu la kujiendeleza kwani kwenye kundi kubwa kama la watumishi wa TVLA, ukiona watu wenye elimu ya juu lakini umri wao umekwenda kidogo, maana yake ni kuwa baada ya muda watatoka na vijana wanatakiwa kuchukua nafasi zao.

“Sifa kubwa ya vijana ni ubunifu. Tunategemea TVLA kuwa na watumishi wengi zaidi vijana ili kasi ya kazi na utoaji matokeo iwe kubwa zaidi, kwa njia fupi zaidi, kwa gharama ndogo lakini kwa matokeo makubwa. Tuzingatie uzalendo kwa nchi yetu; tuwe mabalozi wa kazi tunazozifanya, na tuchape kazi kwa moyo ili ifikapo 2030 tuwe tumewaweka wafugaji wote kwenye tabasamu,” alisema Mhe. Kamani.

Akitoa taarifa kwa Waziri, Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) Dkt. Stella Bitanyi alisema kuwa kwa kipindi cha mwaka 2020/2021 hadi 2024/2025 Wakala umeshuhudia mafanikio mengi yakiwemo ongezeko la mapato ya ndani kutoka bilioni 3.072 hadi bilioni 6.522, yaliyosababishwa na juhudi za menejimenti pamoja na watumishi katika kuhakikisha Wakala unasimama na kuwa chombo thabiti na kinachojitegemea.

Dkt. Bitanyi aliongeza kuwa Wakala imeongeza uzalishaji wa chanjo za mifugo kutoka dozi milioni 64.1 mwaka 2020/2021 hadi dozi milioni 82.6 kwa mwaka 2024/2025 ambayo ni hatua kubwa kwa TVLA. Sambamba na hilo, Wakala imeanzisha vituo viwili vya utoaji huduma za mifugo, ambavyo ni Kituo cha Meatu (Simiyu) na Kituo cha Sumbawanga (Rukwa). Aliongeza kuwa fanikio jingine ni kupata ithibati kwa vipimo 10 vya maabara, ambavyo hadi sasa TVLA inaendelea kuishikilia.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (wa pili kutoka kushoto)  akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Maabara Kuu ya Veterinari (CVL), Dkt. Geofrey Omach kuhusina na kazi za uchunguzi zinazofanya na CVL alipotembelea Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) Desemba 06, 2025  kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na TVLA pamoja na kuongea na watumishi ili kutoa mwelekeo wa malengo ya Serikali ya Awamu ya Sita. Kulia kwake ni Naibu Waziri, Mhe. Ng'wasi Kamani

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (wa tatu kutoka kushoto)  akisalimiana na watumishi wa Wakala ya Maabara ya Veterinari (TVLA) Desemba 06, 2025alipotemblea TVLA  kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa pamoja na kuongea na watumishi ili kutoa mwelekeo wa malengo ya Serikali ya Awamu ya Sita. Kutoka Kulia ni Katibu Mkuu, Bi. Agnes Meena na Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA), Dkt. Stella Bitanyi.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (kushoto), akipata maelezo kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA), Dkt. Stella Bitanyi, kuhusiana na shughuli za kimaabara zinazofanywa na Wakala, alipotembelea TVLA  Desemba 06, 2025 kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na TVLA pamoja na kuongea na watumishi ili kutoa mwelekeo wa malengo ya Serikali ya Awamu ya Sita. Katikati ni Naibu Waziri, Mhe. Ng'wasi Kamani, na kushoto kwake ni Katibu Mkuu, Bi. Agnes Meena.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (wa pili kutoka kushoto)  akipata maelezo kutoka kwa Meneja, Kituo cha Magonjwa ambukizi na Bioteknolojia (CIDB), Dkt. Mathia Mkama kuhusina na kazi zinazofanya na CIDB alipotembelea Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) Desemba 06, 2025 kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na TVLA pamoja na kuongea na watumishi ili kutoa mwelekeo wa malengo ya Serikali ya Awamu ya Sita. Kulia ni Naibu Waziri, Mhe. Ng'wasi Kamani, na kulia kwake ni Katibu Mkuu, Bi. Agnes Meena.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (kulia waliosimama)  akipata maelezo kutoka kwa Mtalamu wa Maabara Kuu ya Veterinari (CVL) Robert Kamnde kuhusina na kazi za uchunguzi wa manjonjwa ya Bakteria zinazofanya na CVL alipotembelea Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) Desemba 06, 2025  kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na TVLA pamoja na kuongea na watumishi ili kutoa mwelekeo wa malengo ya Serikali ya Awamu ya Sita. Kulia kwake ni Naibu Waziri, Mhe. Ng'wasi Kamani

NI JUKUMU LA KILA MTANZANIA KULINDA RASILIMALI ZA UVUVI

 ◼️Apiga marufuku matumizi ya maneno “Uvuvi haramu”

◼️Asisitiza ni Uvuvi usiozingatia sheria na wanaofanya hivyo ni wahalifu

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally amepiga marufuku matumizi ya maneno “Uvuvi haramu” ambapo badala yake ametaka vitendo hivyo sasa vitambulike kama Uvuvi usiozingatia sheria na watu wanaofanya hivyo watambulike kama wahalifu.

Mhe. Balozi Dkt. Bashiru ameyasema hayo wakati akizungumza na watendaji na watumishi wa kitengo cha Uhifadhi wa Maeneo Tengefu alipofika kukagua utekelezaji wa shughuli mbalimbali za kitengo hicho Disemba 06,2025 jijini Dar-es-salaam.

“Hakuna Uvuvi haramu, suala la uharamu na uhalali ni suala la Mwenyezi Mungu sasa mtu haramu maana yake aende motoni na sisi hapa duniani na Serikalini hatuna moto wa kupeleka watu wanaovua uvuvi haramu” Amesisitiza Mhe. Balozi Dkt. Bashiru

Mhe. Balozi Dkt. Bashiru ameongeza kuwa vitendo vya Uvuvi usiozingatia sheria vinatokana na kukosekana kwa utawala wa sheria katika sekta ya Uvuvi suala ambalo amesisitiza kuwa linapaswa kutekelezwa na kila Mtanzania.

“Kwa hiyo mimi sitakuwa na msamiati wa Uvuvi haramu kwa sababu Rais hajateua masheikh, mapadri, wachungaji au mitume bali ameteua Watanzania kusimamia sheria na kama sheria ni dhaifu bunge lipo na mimi ndo ninaiwakilisha sekta ya Uvuvi na Mifugo bungeni kwa hiyo tuimarishe sheria zetu” Amesema Mhe. Balozi Dkt. Bashiru.

Aidha Mhe. Balozi Dkt. Bashiru ametoa kwa Watanzania popote walipo pindi wanaposhuhudia vitendo vinavyoashiria Uvuvi usiozingatia sheria wahakikishe wanawachukulia hatua za kisheria watu hao.

“We unamuona mtu ana nyavu za kihalifu, anavua kihalifu, wasimamizi wa sheria wanamlinda mhalifu afu wewe mwenye wajibu wa kusimamia utawala wa sheria unalalamika bila kuchukua hatua kwa hiyo hili ni tatizo letu sote na tutakapoanza kudhurika kutokana na uvuvi wa kihalifu tutaumia wote” Amehitimisha Mhe. Balozi Dkt. Bashiru.


Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa akisalimiana na Kaimu Mkuu wa kitengo cha Uhifadhi wa MaeneoTengefu Bw. Godfrey Ngupula muda mfupi baada ya kufika kwenye ofisi za kitengo hicho Disemba 06,2025 jijini Dar-es-salaam.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani akisaini kitabu cha wageni muda mfupi baada ya kufika kwenye ofisi za kitengo cha Uhifadhi wa Maeneo Tengefu Disemba 06,2025 jijini Dar-es-salaam.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (katikati walioketi) akiwa kwenye picha ya pamoja na Watendaji wa Wizara yake na watumishi wa kitengo cha Uhifadhi wa Maeneo Tengefu muda mfupi baada ya kuzungumza nao Disemba 06,2025 jijini Dar-es-salaam.






DKT. BASHIRU ASISITIZA UMAKINI USHIRIKISHAJI SEKTA BINAFSI

 ◼️Ataka TAFICO liwe Shirika la mfano

◼️Kamani awaita vijana kuchangamkia fursa

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amezitaka mamlaka zilizopo chini ya Wizara yake kwa upande wa sekta ya Uvuvi kuwa makini kwenye ushirikishaji wa sekta binafsi za ndani na zile za nje.

Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amesema hayo wakati wa ziara yake kwenye Ofisi za Shirika la Uvuvi nchini (TAFICO) aliyoifanya Disemba 05,2025 jijini Dar-es-salaam ambapo amelitaka shirika hilo kushirikisha sekta binafsi za ndani kwa mambo ambayo sekta hizo zinaweza kufanya kwenye mchakato wa kufufua shughuli zake unaoendelea hivi sasa.

“Hatuwezi kukwepa kabisa kushirikisha sekta binafsi za nje kwa sababu za uzoefu, teknolojia, mitaji na kupata masoko ya nje kwa sababu biashara hii ya mazao ya uvuvi ni kubwa hivyo soko likichangamka masoko ya ndani hayatatosha” Amesisitiza Mhe. Balozi Dkt. Bashiru.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Ng’wasi Kamani amewataka vijana waliopo nje ya mfumo rasmi wa ajira kuchangamkia fursa zilizopo kwenye sekta ya Uvuvi hususan zile zitakazotokana na shughuli za Shirika hilo pindi litakavyoanza kufanya kazi

“Nimefurahi kuona hapa wapo vijana ambao walichangamkia fursa zilizopo kwenye sekta ya Uvuvi mpaka wakaajiriwa hivyo niwaombe nyie muwe mabalozi kwa wenzenu waliopo nyumbani mkawaeleze fursa hizi zilizopo kwani ndio dhamira ya Mhe. Rais ya kuhakikisha vijana wananufaika na sekta hizi za uzalishaji” Amesema Mhe. Kamani.

Mhe. Balozi Dkt. Bashiru na Naibu wake Mhe. Kamani wanatarajiwa kuendelea na ziara yao Disemba 05,2025 ambapo watatembelea Wakala ya Maabara ya Veterinari nchini (TVLA) na Kitengo cha Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu (MPRU).


Kaimu Mkuu wa kitengo cha Uthibiti ubora na Usimamizi wa Mazingira Bw. Mgalula Lyoba (kulia) kutoka Shirika la Uvuvi nchini (TAFICO) akiwaonesha Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, Naibu wake Mhe. Ng’wasi Kamani na watendaji mbalimbali wa Wizara hiyo nyuzi stahili zinazopaswa kutumika kutengenezea nyavu za kuvulia samaki wakati wa Ziara ya viongozi hao Disemba 05,2025 jijini Dar-es-salaam.


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani akisalimiana na wafanyakazi wa Shirika la Uvuvi nchini (TAFICO) muda mfupi baada ya kuwasili kwenye ofisi za Shirika hilo Disemba 05,2025 jijini Dar-es-salaam.


Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa akisalimiana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Uvuvi nchini (TAFICO) CPA. Shaibu Matessa muda mfupi baada ya kuwasili kwenye ofisi za Shirika hilo Disemba 05,2025 jijini Dar-es-salaam.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, Naibu wake Mhe. Ng’wasi Kamani wakiangalia mavazi maalum yanayotumiwa na waendeshaji wa vyombo vya Uvuvi muda mfupi baada ya kuwasili Shirika la Uvuvi nchini (TAFICO) Disemba 05,2025 jijini Dar-es-salaam.


Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, Naibu wake Mhe. Ng’wasi Kamani (kushoto) wakisalimiana na wawakilishi wa Kampuni ya Ogawa Seiki ya nchini Japani iliyotengeneza Meli ya Uvuvi ya Shirika la Uvuvi nchini (TAFICO) na kampuni mbia ya ndani ya Electricool Tanzania Limited inayoshughulikia mifumo ya shirika hilo mara baada ya kufika hapo Disemba 05,2025 jijini Dar-es-salaam.

RAIS SAMIA ANATAKA TUFANYE MAAMUZI YANAYOTOKANA NA UTAFITI-DKT. BASHIRU

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anataka viongozi na watendaji wa Serikali yake kufanya maamuzi yanayotokana na matokeo ya utafiti.

Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amesema hayo Disemba 05,2025 jijini Dar-es-salaam wakati akizungumza na watumishi wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi nchini (TAFIRI) alikofika akiwa pamoja na Naibu Waziri Mhe. Ng’wasi Kamani, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi. Agnes Meena, Naibu Katibu Mkuu Dkt. Edwin Mhede na baadhi ya watendaji wa Wizara   ambapo aliwataka wataalam hao kutambua umuhimu wa Taasisi hiyo kwa maslahi ya Taifa.

“Katika umuhimu wa Taasisi hii na mwelekeo wa Serikali ya awamu ya 6 juu ya kukuza sekta hii ya Uvuvi ili iwe na mchango mkubwa kwenye uchumi wetu, nimetumwa na Mhe. Rais nifanye ziara ya kwanza kwenye kituo hiki ambapo anataka tufanye mambo yanayotokana na ushauri,tusifanye maamuzi kwa mihemko” Amesema Mhe. Balozi Dkt. Bashiru.

Mara baada ya kuhitimisha ziara yake kwenye kituo hicho Mhe. Balozi Dkt. Bashiru na viongozi wengine alioambatana nao walielekea kwenye Shirika la Uvuvi nchini (TAFICO).

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa akitoa maelekezo kwa Watendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi nchini (TAFIRI) mara baada ya kukagua hatua za ujenzi unaoendelea kwenye Taasisi hiyo kanda ya Dar-es-salaam Disemba 05,2025.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (kulia), Naibu Waziri wake Mhe. Ng’wasi Kamani (katikati) na Mkurugenzi wa Uvuvi nchini Prof. Mohammed Sheikh wakifuatilia michango ya wajumbe kwenye kikao cha baina yao na Menejimenti ya Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi nchini (TAFIRI) kilichofanyika Disemba 05,2025 jijini Dar-es-salaam.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (wa pili kutoka kushoto), Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Edwin Mhede (wa pili kutoka kulia), Mkurugenzi wa Uvuvi nchini Prof. Mohammed Sheikh (kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi nchini (TAFIRI) Dkt. Ismail Kimirei wakielekea inapojengwa maabara mpya ya Taasisi hiyo muda mfupi baada ya Mhe. Balozi Dkt. Bashiru kuwasili makao makuu ya Taasisi hiyo jijini Dar-es-salaam Disemba 05,2025.

Kaimu Mkuu wa kituo cha Utafiti wa Uvuvi (TAFIRI) kanda ya Dar-es-salaam Dkt. George Rushingisha (kushoto) akimueleza Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (katikati) huduma zinazotolewa na kituo hicho muda mfupi baada ya Mhe. Dkt. Bashiru kuwasili hapo Disemba 05,2025 jijini Dar-es-salaam.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agnes Meena akifafanua jambo wakati wa ziara ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (kushoto) alipotembelea Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi nchini (TAFIRI) Disemba 05,2025 jijini Dar-es-salaam. Katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo Dkt. Ismail Kimirei.




Alhamisi, 4 Desemba 2025

DKT. BASHIRU AKABIDHI PIKIPIKI 381 KWA MAAFISA UGANI NCHINI

◼️Asisitiza Wafugaji ndio kipimo cha utendaji wao

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amewataka Maafisa ugani nchini kujenga ushirikiano madhubuti baina yao na wafugaji utakaolenga kutoa taarifa sahihi, kuelimisha, kutoa ushauri wa kitaalam, kusambaza teknolojia na kupata mrejesho wa matumizi ya teknolojia hizo.

Mhe. Balozi Dkt. Bashiru ametoa maelekezo hayo wakati wa Hafla fupi ya kukabidhi pikipiki 381 kwa Maafisa ugani wote waliopo kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa iliyofanyika Disemba 04,2025 jijini Dar-es-Salaam ambapo amewataka kutanguliza dhana ya majadiliano zaidi badala ya kufundisha pindi wanapokuwa uwandani.

“Huduma za Ugani ni muhimu na ni kiungo kati ya watafiti na wafugaji ili kupata ufugaji wenye tija hivyo ni vema mkaimarisha mahusiano hayo kwa hiyo niwaombe na nirejee tena kama alivyoelekeza Mhe. Rais twendeni kuwahudumia watu sio kama tunawafundisha kama hawana taaluma au uelewa bali tukajadiliane nao na kuwasikiliza” Amesisitiza Mhe. Balozi Dkt. Bashiru.

Aidha Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amewataka maafisa ugani hao kuhakikisha wanatatua changamoto zote zinazowakabili wafugaji huku akiwataka kutoa taarifa kwa upande wa changamoto zinazopaswa kutatuliwa katika ngazi ya Wizara.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa pikipiki hizo kwa niaba ya Maafisa ugani nchini Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amemhakikishia Mhe. Balozi Dkt. Bashiru kuwa pikipiki hizo zitatunzwa na kufanya kazi iliyokusudiwa.

“Nikuhakikishie Mhe. Waziri hutaziona pikipiki hizi zikitumika kama bodaboda na tutahakikisha kwamba vitendea kazi hivi vinaendelea kutumika kwenye zoezi la Chanjo za Mifugo na Utambuzi linaloendelea nchi nzima” Ameongeza Mhe. Prof. Shemdoe.

Akizungumza kwa Niaba ya Wakuu wa Mikoa Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam Mhe. Albert Chalamila amesema kuwa pikipiki hizo zitasaidia kuchochea ufugaji wa kisasa na kuwafanya wafugaji kukopesheka hatua ambayo itaboresha maisha yao na kuakisi dhana ya “Tabasamu” kupitia Wizara za Mifugo na Uvuvi na ile ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI.

Nao wawakilishi wa Maafisa ugani Bw. Peter Shirima kutoka Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma na Odetha Muchukuzi kutoka mkoani Dar-es-Salaam wameishukuru Serikali kwa kuwapatia nyenzo hizo ambazo wamesema kuwa zitawasaidia kuwahudumia wafugaji kwa urahisi zaidi.

Pikipiki hizo zinaifanya Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuwa imeshagawa jumla ya pikipiki 2581 hadi sasa ambazo zote zimelenga kuwarahisishia maafisa ugani hao kuwafikia wafugaji.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (kushoto) akimkabidhi moja ya  pikipiki 381 za Maafisa Ugani nchi nzima (wawakilishi waliokaa kwenye pikipiki) Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe kwenye hafla fupi iliyofanyika Disemba 04,2025 jijini Dar-es-Salaam. Anayeshuhudia (nyuma) ni Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe (kushoto) akimkabidhi pikipiki za Maafisa Ugani kwa niaba ya wakuu wa mikoa yote, Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam Mhe. Albert Chalamila ikiwa ni muda mfupi baada ya kukabidhiwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa kwenye hafla fupi  iliyofanyika Disemba 04,2025 jijini Dar-es-Salaam.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (wa tatu kutoka kushoto) Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe (wa nne kutoka kulia), Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani (katikati), Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam Mhe. Albert Chalamila (wa tatu kutoka kulia) na watendaji wengine wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi na huo wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa hafla fupi ya kukabidhi pikipiki 381 za Maafisa Ugani iliyofanyika Disemba 04,2025 jijini Dar-es-Salaam.

Sehemu ya pikipiki 381 zilizotolewa na Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa Maafisa Ugani nchini kwenye hafla fupi iliyofanyika Disemba 04,2025 jijini Dar-es-Salaam.






KATIBU MKUU BI. MEENA AZINDUA KIKAO CHA KWANZA CHA USIMAMIZI WA MRADI WA TASFAM

Na Daudi Nyingo Dar Es Salaam

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes K. Meena, ameongoza kikao cha kwanza cha Kamati ya Usimamizi wa Mradi wa Tanzania Scaling-Up Sustainable Marine Fisheries and Aquaculture Management (TASFAM) kilichofanyika tarehe 2 Desemba 2025 katika ukumbi wa TVLA ulipo Temeke Dar es salaam. 

Akizungumza mbele ya Mwenyekiti Mwenza, Wakurugenzi, Wataalam wa Sekta ya Uvuvi na wajumbe mbalimbali, Bi. Meena ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Rais wa Zanzibar, Mhe. Hussein Ali Mwinyi, kwa kutoa kipaumbele kikubwa kwa sekta ya uvuvi na uchumi wa buluu.

“Mradi wa TASFAM una thamani ya Dola za Marekani milioni 117, umeandaliwa tangu mwaka 2021 kwa ushirikiano kati ya Tanzania na Benki ya Dunia, mradi huu utatekelezwa kwa muda wa miaka mitano (2025–2030) na unalenga kuimarisha mnyororo wa thamani wa uvuvi, kupunguza upotevu wa mazao, kulinda mazingira na kuongeza kipato cha wananchi.” 

“mradi utahusisha Halmashauri 16 za pwani ya Tanzania Bara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba, na wanufaika wakuu watakuwa ni wavuvi wadogo, jamii za pembezoni mwa pwani, sekta binafsi na mashirika yasiyo ya kiserikali.” Alisema Bi Meena

Bi. Meena ameyataja baadhi ya maeneo ya kipaumbele kuwa ni pamoja na ujenzi wa miundombinu ya masoko na mialo ya kisasa, kuimarisha kilimo cha mwani, ufugaji wa jongoo bahari na kaa, pamoja na usambazaji wa vyombo vya kisasa vya uvuvi na ununuzi wa meli ya utafiti wa bahari. Zaidi ya vikundi 300 vya wakulima wa mwani na wafugaji wa viumbe baharini vitanufaishwa.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes K. Meena, akiongoza kikao cha kwanza cha Kamati ya Usimamizi wa Mradi wa Tanzania Scaling-Up Sustainable Marine Fisheries and Aquaculture Management (TASFAM) kipindi cha 2025/2026 kilichofanyika tarehe 2 Desemba 2025 katika ukumbi wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) ulipo Temeke, Dar es salaam. Bi. Meena ndiye aliyekuwa Mwenyekiti wa Kikao hicho.

Katibu Mkuu Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi, Zanzibar, Kapt. Hamad B. Hamad (kulia) akichangia mada kwenye kikao cha kwanza cha Kamati ya Usimamizi wa Mradi wa Tanzania Scaling-Up Sustainable Marine Fisheries and Aquaculture Management (TASFAM) kipindi cha 2025/2026 kilichofanyika tarehe 2 Desemba 2025 katika ukumbi wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) ulipo Temeke, Dar es salaam. Kapt. Hamad alikuwa Mwenyekiti Mwenza wa Kikao hicho. kushoto kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes K. Meena

Mratibu wa Mradi wa Tanzania Scaling-Up Sustainable Marine Fisheries and Aquaculture Management (TASFAM) Dkt. Nichrous Mlalila akiwasilisha mada kwenye kikao cha kwanza cha Kamati ya Usimamizi wa Mradi wa Tanzania Scaling-Up Sustainable Marine Fisheries and Aquaculture Management (TASFAM) kipindi cha 2025/2026 kilichofanyika tarehe 2 Desemba 2025 katika ukumbi wa wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) ulipo Temeke, Dar es salaam.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikali, Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Mbaraka Kambona akiwasilisha mada kuhusu usanifu wa Nembo ya Mradi kwenye kikao cha kwanza cha Kamati ya Usimamizi wa Mradi wa Tanzania Scaling-Up Sustainable Marine Fisheries and Aquaculture Management (TASFAM) kipindi cha 2025/2026 kilichofanyika tarehe 2 Desemba 2025 katika ukumbi wa wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) ulipo Temeke, Dar es salaam.

Pichani Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes K. Meena (aliekaa kushoto) na Katibu Mkuu Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi, Zanzibar Kapt. Hamad B. Hamad (aliekaa kulia) wakiwa kwenye picha na Wajumbe wa Kamati ya Usimamizi wa Mradi wa Tanzania Scaling-Up Sustainable Marine Fisheries and Aquaculture Management (TASFAM) kilichofanyika tarehe 2 Desemba 2025 katika ukumbi wa wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) ulipo Temeke, Dar es salaam.

Pichani Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes K. Meena (aliekaa kushoto) na Katibu Mkuu Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi, Zanzibar Kapt. Hamad B. Hamad (aliekaa kulia) wakiwa kwenye picha na kamati tendaji ya Usimamizi wa Mradi wa Tanzania Scaling-Up Sustainable Marine Fisheries and Aquaculture Management (TASFAM) kilichofanyika tarehe 2 Desemba 2025 katika ukumbi wa wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) ulipo Temeke, Dar es salaam.

Pichani Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes K. Meena (aliekaa kushoto) na Katibu Mkuu Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi, Zanzibar Kapt. Hamad B. Hamad (aliekaa kulia) wakiwa kwenye picha na waratibu wa mradi wa Usimamizi wa Mradi wa Tanzania Scaling-Up Sustainable Marine Fisheries and Aquaculture Management (TASFAM) kilichofanyika tarehe 2 Desemba 2025 katika ukumbi wa wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) ulipo Temeke, Dar es salaam.







SERIKALI, WADAU YAANZA KUPITIA MPANGO MKAKATI KUTOKOMEZA UGONJWA WA SOTOKA YA MBUZI NA KONDOO

Serikali ya kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya mifugo imeanza kufanya mapitio ya kutokomeza ugonjwa Sotoka (Peste des Petits Ruminants (PPR) ifikapo mwaka 2030,  hatua itakayoiweka Tanzania katika mstari wa mbele barani Afrika katika mapambano dhidi ya ugonjwa huu unaodhuru mifugo.

Akifungua warsha ya Kitaifa ya Tathmini na Mapitio ya Mkakati wa Kitaifa wa Kupambana na PPR iliyofanyika leo Desemba Mosi, 2025 katika Hoteli ya Peacok jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,  Bi.Agnes Meena amesema Sekta  ya mifugo imekuwa nguzo muhimu ya uchumi wa Tanzania, ikichangia asilimia 6.2 ya Pato la Taifa na kusaidia zaidi ya kaya milioni tano lakini imekuwa ikikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo magonjwa yanayosababisha vifo vya mifugo. 

“Kondoo na mbuzi wanakabiliwa na changamoto ya PPR inayosababisha vifo vingi, hasara za kiuchumi na kukwamisha upatikanaji wa masoko ya kikanda na kimataifa.”

Bi. Meena aliongeza kuwa serikali imetenga zaidi ya shilingi bilioni 200 kwa miaka mitano ijayo ili kuimarisha chanjo, utambuzi na mifumo ya ufuatiliaji wa mifugo, hivyo dhamira ya serikali kutokomeza magonjwa ya mifugo ikiwemo  PPR itafanikiwa.

Hapo awali,  Mwakilishi wa  Shirika la Rasilimali za Mifugo la Umoja wa Africa (AU-IBAR) Dkt. Folorunso Fasina, alibainisha nafasi muhimu ya Tanzania  kutokomeza ugonjwa wa Sotoka ya mbuzi na kondoo kwani ugonjwa huo umeendelea kusababisha hasara ya hadi dola bilioni 2.4 kila mwaka kwa bara la Africa  hivyo kampeni ya kutokomeza PPR ifikapo 2030.

Naye, Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo, Dkt. Benezeth Lutege, alisema warsha hiyo ni tukio la kihistoria kwa sekta ya mifugo nchini Tanzania ikiwa ni sehemu muhimu ya kutokomeza ugonjwa wa Sotoka ya mbuzi na Kondoo kwani unaathiri afya ya mifugo na kukwamisha biashara.

Mwakilishi wa Shirima la Chakula na Kilimo la umoja wa Mataifa (FAO) nchini  Tanzania,  Dkt. Justine Assenga ameipongeza Tanzania kwa hatua muhimu ya kuanisha mkakati wa kitaifa wa kutokomeza ugonjwa wa Sotoka ya mbuzi na Kondoo.

Katibu Mkuu Wizara ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi.Agnes Meena akifungua warsha ya kupitia na kuhakiki mkakati wa kitaifa wa kutokomeza ugonjwa wa sotoka ya mbuzi na kondoo ifikapo 2030, warsha inayofanyika Hoteli ya Peacok jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 1 hadi 2 Desemba  2025.

Mwakilishi wa Shirika la Rasilimali za Mifugo la Umoja wa Africa (AU - IBAR) Dkt. Folorunso Fasina akizungumza kwenye warsha ya kupitia na kuhakiki mkakati wa kitaifa wa kutokomeza ugonjwa wa sotoka ya mbuzi na kondoo ifikapo 2030, warsha inayofanyika Hoteli ya Peacok jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 1 hadi 2 Desemba  2025.

Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo Dkt. Benezeth Lutege akielezea umuhimu wa Mkakati wa Kitaifa wa Kutokomeza Ugonjwa wa Sotoka ya mbuzi na kondoo ifikapo 2030 wakati wa warsha inayofanyika Hoteli ya Peacok jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 1 hadi 2 Desemba  2025.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agnes Meena (Katikati, waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau wa sekta ya mifugo wakati wa warsha ya kupitia na kuhakiki  Mkakati wa Kitaifa wa Kutokomeza Ugonjwa wa Sotoka ya mbuzi na kondoo ifikapo 2030 iliyofanyika Hoteli ya Peacok jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 1 hadi 2 Desemba  2025.




BI. MEENA AMPONGEZA DKT. MRUTTU KWA KUHITIMISHA SAFARI YAKE YA UTUMISHI

Na. Stanley Brayton, WMUV

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Meena amempongeza aliyekuwa Mkurugenzi Msaidizi wa Vyakula vya Mifugo Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Hassan Mruttu kwa kuhitimisha Utumishi wake bora uliotukuka.

Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kumuaga Dkt. Mruttu katika kuhitimisha Utumishi wake, leo Novemba 28, 2025, Jijini Dodoma, Bi. Meena amesema Dkt. Mruttu ni mwalimu mzuri sana, na amekuwa akiwafundisha wengi ili waweze kujifunza na kupata Ujuzi zaidi katika masuala ya Mifugo na lishe.

“ni vyema kuenzi na kufuata ushauri wa kitaalamu ambao Dkt. Mruttu alikuwa anawapatia ili kuleta tija katika Sekta ya Mifugo.” amesema Bi. Meena

Aidha, Bi. Meena amemtakia heri Dkt. Mruttu katika maisha yake mapya nje ya Utumishi wa Umma na kumsisitiza kuwa aendelee kutoa ushauri kwa vijana juu ya ufugaji na kuwataka watumishi wengine wa Wizara hiyo kujifunza kupitia yeye ili kuweza kuleta matokeo chanya kwa Sekta hiyo ya Mifugo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi Utawala, Bw. Samwel Mwashambwa amesema ni furaha sana kuona mtumishi ana hitimisha Utumishi wake akiwa na Afya njema na mwenye furaha.

Vilevile, Bw. Mwashambwa amemuelezea Dkt. Mruttu kama mtu ambaye alikuwa anapenda ukweli na uwazi katika utendaji wake, na kusisisitiza kuwa ni vyema watumishi wengine kuiga mfano wake na kumtumia kama kitabu cha kujifunza katika Utumishi wake.

Naye, aliyekuwa Mkurugenzi Msaidizi wa Vyakula vya Mifugo Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Hassan Mruttu amemshukuru sana Katibu Mkuu wa Wizara hiyo na kusema kuwa amefalijika sana kupata ushirikiano wa kutosha toka anapoanza Utumishi na mpaka anapohitimisha Utumishi wake katika Wizara hiyo.

Dkt. Mruttu amesisitiza kuwa ni vyema viongozi na wakurugenzi kujua asili ya watu wanaofanya nao kazi na tabia zao ili iweze kuwasaidia katika utendaji kazi wao.





Jumatatu, 1 Desemba 2025

TUFANYE UPYA TATHMINI YA FURSA ZITAKAZOTOKANA NA BANDARI YA UVUVI-DKT. BASHIRU

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Bashiru Ally Kakurwa ameelekeza kufanyika upya tathmini ya fursa zitakazotokana na bandari ya Uvuvi inayotarajiwa kukamilika mwishoni mwa Disemba 2025.

Mhe. Dkt. Bashiru amesema hayo wakati wa ziara yake ya kukagua hatua za ujenzi wa bandari hiyo aliyoifanya Novemba 28,2025 Wilayani Kilwa mkoa wa Lindi ambapo ameitaka menejimenti ya Wizara yake na uongozi wa Wilaya ya Kilwa na mkoa huo kutengeneza kamati ya kupitia upya malengo yaliyokuwa yamewekwa awali ili kuangazia fursa mpya zitakazotokana na bandari hiyo.

“Fursa za kibiashara, fursa za wavuvi wakubwa, wakati na wadogo na sisi katika Wizara tuna kazi ya kuzitangaza vizuri ili watu wazielewe zikiwemo fursa za ajira na fursa za uwekezaji katika maeneo mbalimbali” Ameongeza Mhe. Balozi Dkt. Bashiru.

Aidha Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amezialika taasisi zote za kifedha na wadau wote wa sekta binafsi kuanza kuchunguza na kubainisha fursa zilizopo bandarini hapo na kujipanga kuzitumia.

“Jipangeni kuonesha kwamba tupo tayari kuwezesha utekelezaji wa matarajio na malengo ya Mhe. Rais ya kuhakikisha kwamba anapomaliza kipindi chake cha uongozi anaacha tabasamu katika nyuso za Watanzania” Amehitimisha Mhe. Balozi Dkt. Bashiru.

Ujenzi wa bandari hiyo unatarajiwa kukamilika mwisho wa mwezi Disemba 2025 ambapo utagharimu kiasi cha shilingi Bil. 289.5.







Ijumaa, 28 Novemba 2025

DKT. BASHIRU AVUTIWA NA UWEKEZAJI SEKTA ZA MIFUGO NA UVUVI

◼️Ahimiza Watumishi wa Wizara yake kuwajibika

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amevutiwa na uwekezaji uliofanywa na wadau wa sekta za Mifugo na Uvuvi nchini ambapo amewataka kushirikiana kwa ukaribu na Wizara yake ili kuendelea kuzalisha mazao yanayokidhi viwango stahiki.

Mhe. Balozi Dkt. Kakurwa amesema hayo Novemba 27,2025 alipotembelea viwanda vya kusindika nyama (TANCHOICE na UNION MEAT) vyakula vya Mifugo na Samaki (BACKBONE)  na kiwanda cha kuzalisha chanjo (TANCHOICE) vilivyopo mkoani Pwani.

“Nipo tayari kuwapa ushirikiano wote mnaohitaji na mimi nimekuja kuomba ushirikiano wenu kwa sababu bila ushirikiano wetu kazi hii haiwezi kwenda inavyotakiwa na kila jambo mnaloona ni la mafanikio mtueleze ili tulidumishe na kila mnaliona ni dosari mtubainishie afu mtoe maoni ya namna ya kuondokana na vikwazo hivyo na kutatua dosari zilizopo kwa uzoefu mlionao” Ameongeza Mhe. Balozi Dkt. Bashiru.

Aidha Dkt. Bashiru ametoa wito kwa watumishi wa Wizara yake kuwajibika ipasavyo ili kuendelea kutengeneza mazingira rafiki kwa wawekezaji hao kutimiza wajibu wao huku akisisitiza kutosita kuchukua hatua kwa mtendaji yoyote atakayezembea kwenye jambo hilo.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani ameupongeza uongozi wa mkoa huo kwa kuweka mazingira wezeshi yaliyofanikisha uwepo wa Viwanda hivyo ambapo amefafanua kuwa jambo hilo linaakisi dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan iliyolenga kufanya mageuzi ya uchumi wa nchi kupitia sekta za uzalishaji za Kilimo, Mifugo na Uvuvi.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Wafugaji mkoani humo Bw. Ngobere Msamau ameishukuru Serikali kwa kuendelea kuwajengea mazingira wezeshi ya kutekeleza shughuli zao kuwapatia ruzuku kwenye chanjo za Mifugo na kuwezesha uwekezaji wa viwanda cha kusindika nyama ambavyo  vimewafungulia soko la Mifugo yao. 

“Wajibu wetu kwa sasa ni kuendelea kuboresha mifugo yetu ili kuhakikisha viwanda hivi vinaendelea kupata malighafi za kutosha” Ameongeza Bw. Msamau.

Ziara ya Mhe. Balozi Dkt. Bashiru na Naibu wake Mhe. Kamani itaendelea Novemba 28 mkoani Lindi ambapo wanatarajiwa kutembelea na kukagua hatua za ujenzi wa bandari ya Uvuvi iliyopo Wilaya ya Kilwa.

Meneja wa Shamba la uzalishaji malisho ya Mifugo la Vikuge Bw. Reuben Ngailo akimueleza Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (katikati) sifa za malisho ya Mifugo aina ya Nepia iliyoboreshwa (JUNCAO) muda mfupi baada ya Mhe. Balozi Dkt. Kakurwa na Naibu  wake Mhe. Ng’wasi Kamani kufika (kushoto) kwenye shamba hilo lililopo mkoani Pwani Novemba 27,2025.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Bashiru Ally Kakurwa na Naibu wake Mhe. Ng’wasi Kamani wakikagua kiwanda cha kusindika nyama cha Union Meat kilichopo eneo la Ruvu mkoani Pwani Novemba 27,2025.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Bashiru Ally Kakurwa na Naibu wake Mhe. Ng’wasi Kamani wakioneshwa namna nyama inavyosindikwa kwenye kiwanda cha Union Meat kilichopo eneo la Ruvu mkoani Pwani Novemba 27,2025.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani akieleza umuhimu wa sekta za uzalishaji kwenye ukuzaji wa uchumi wa nchi wakati wa ziara yao na Mhe. Waziri Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa waliyoifanya mkoani Pwani Novemba 27,2025.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa akisalimiana na Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Pwani ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Mhe. Nickson Simon muda mfupi baada ya kuwasili mkoani humo Novemba 27,2025.




MRADI WA BBT WA UNENEPESHAJI MBUZI NA KONDOO KUANZA KUTEKELEZWA KONGWA

Na. Stanley Brayton, WMUV

Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi yaanza Rasmi kutekeleza Mradi wa miaka Mitano wa Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT) ya Unenepeshaji wa Mbuzi na Kondoo katika eneo la Kituo cha Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) iliyopo Kongwa, ikiwa na lengo la kuongeza ushiriki wa Vijana na Wanawake katika ujasiliamali wa Biashara ya Mifugo.

Akizungumza wakati wa Ziara yake ya kikazi wakati akikagua Miundombinu ya Mradi huo, leo Novemba 27, 2025 Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Meena amesema Mradi huo unatarajiwa kuanza kutoa Mafunzo mapema mwaka huu, na lengo la Mradi huo ni kwa ajili ya kuwapatia Vijana Mafunzo ya Unenepeshaji wa Mbuzi na Kondoo ili waweze kufuga kibiashara.

“mradi huu utakuwa na uwezo wa kutoa Mafunzo kwa vijana 200 kwa mwaka na vijana Takribani 1750 wataweza kupata Mafunzo hayo kwa miaka Mitano.” amesema Bi. Meena

Aidha, Bi. Meena amesema Mradi huo una eneo la heka 2000 kwa ajili ya kupanda Malisho ya Mifugo na hautokuwa wa unenepeshaji wa Mbuzi na Kondoo tu, bali utajumuisha kilimo cha Malisho ya Mifugo, uzalishaji wa nyama na vyakula vya Mifugo.

Vilevile, Bi. Meena amewataka Maafisa wa Wizara hiyo, kuboresha sehemu za michezo katika Mradi huo kama sehemu Mpira wa Miguu, Mpira wa Pete na Mpira wa kikapu ili Vijana waweze kufanya mazoezi ili kujenga mwili baada ya shughuli za siku kuisha.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Meena (wa kwanza kushoto), akiwa katika eneo la mabanda ya Mradi wa BBT ya Mbuzi na Kondoo wakati akifanya ukaguzi wa miundombinu hiyo, wakati wa Ziara  yake katika eneo la Mradi huo uliopo katika Kituo cha Taasisi ya Utafiti wa Mifugo na Uvuvi Tanzania (TALIRI) Kongwa, Novemba 27, 2025 Dodoma, wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bwana. Daudi Mayeji.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Meena (wa pili kushoto), akisikiliza hoja mbalimbali za Maafisa wa Wizara yake, juu ya uzalishaji wa tija na Uboreshaji wa Miundombinu mbalimbali, wakati alipotembelea na kufanya kikao kifupi na Maafisa hao katika Ofisi ya Kituo cha Taasisi ya Utafiti wa Mifugo na Uvuvi Tanzania (TALIRI) Kongwa, Novemba 27, 2025 Dodoma.


Mhandisi Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bw. Gabriel Mligo (aliyenyoosha Mkono), akielezea kwa mifano juu ya Ramani ya Majengo ya Mradi wa BBT uliopo katika Kituo cha Taasisi ya Utafiti wa Mifugo na Uvuvi Tanzania (TALIRI) Kongwa, wakati wa Ziara ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bi. Agnes Meena (hayupo pichani), Novemba 27, 2025 Dodoma.