Nav bar

Jumatatu, 19 Januari 2026

SERIKALI, IFAD KUENDELEZA MIRADI YA SEKTA ZA MIFUGO NA UVUVI.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (Mb.), amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) ambapo wamejadili kuhusu miradi inayotekelezwa kuendeleza sekta ya mifugo na uvuvi.

Akizungumza katika Kikao hicho kilichofanyika leo Januari 16, 2026, Ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru ameonesha kufurahishwa na ujio wa ujumbe huo ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wa IFAD nchini.

Amesema serikali ya awamu ya sita imeendelea kuimarisha mazingira kuwa rafiki ili kuruhusu wawekezaji na sekta binafsi kushiriki katika kusukuma maendeleo ya wananchi.

Ujumbe huo wa IFAD  umeongozwa na Mkurugenzi wa Nchi na Mwakilishi wake nchini Tanzania Bw. Seth Meng pamoja na Mratibu wa Mpango wa Nchi wa IFAD Bi. Jacqueline Machangu.

Majadiliano hayo yalijikita kujadili mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa na Mabadiliko ya Tabianchi (C-SDTP) na Mradi wa Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) inayotekelezwa kati ya sekta ya mifugo na uvuvi.


Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (Wa kwanza, kushoto) akizungumza Ujumbe wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) nchini Tanzania kujadili miradi inayotekelezwa katika sekta ya mifugo na uvuvi, wakati wa Kikao kilichofanyika ofisini kwake leo Januari 16, 2026 Mtumba, Jijini Dodoma.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (Kushoto) akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi  wa Nchi na Mwakilishi wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), Bw. Seth Meng (Katikati) akielezea mpango wa utekelezaji wa miradi ya sekta ya mifugo na uvuvi  Januari 16, 2026 Mtumba, Jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Nchi na Mwakilishi wa IFAD Bw. Seth Meng (Kulia) akimpa maelezo Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa kuhusu utekelezaji wa miradi ya sekta za mifugo na uvuvi wakati wa majadiliano yaliyofanyika Ofisi ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi Januari 16, 2026 Mtumba, Jijini Dodoma.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (Katikati), Mkurugenzi wa Nchi na Mwakilishi wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo, IFAD Bw. Seth Meng (Kushoto) na Mratibu wa Mpango wa Nchi wa IFAD Bi. Jaqueline Machangu (Kulia) wakiwa katika picha ya pamoja baada ya majadiliano yaliyofanyika Ofisi ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi  Januari 16, 2026 Mtumba, Jijini Dodoma.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni