Nav bar

Jumatano, 14 Novemba 2018

KIKAO KAZI CHA WAZIRI MH. LUHAGA MPINA NA WASINDIKAJI WAKUBWA WA MAZIWA NCHINI.




Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh.Luhaga Joelson Mpina (Mb) amekutana na Kampuni kubwa za usindikaji wa maziwa nchini (Tanga Fresh, ASAS,MILCOM NA AZAM) leo tarehe 12/11/2018 jijini Dodoma.

Lengo la kikao kazi hicho ilikuwa ni kujadili mikakati ya uongezaji wa Usindikaji wa maziwa kwenye Kampuni kubwa za Maziwa nchini.

 Nataka Ifikapo tarehe 12/12/2018 mkakati wa ushirikiano uwe umekamilika na kusainiwa kati ya
Kampuni za Wasindikaji wa Maziwa na Dawati la Sekta Binafsi, alisema Mh.Waziri Luhaga Mpina.

Mhe. Mpina aliwaelekeza Wakuu wa Idara na Vitengo kila mtu kwa upande wake kulitumia na
kulisimamia dawati katika kutekeleza Mikakati iliyopangwa.

 Mkakati huu unaenda kuongeza uzalishaji wa maziwa kwa asilimia 84.7 kwa mwaka, alisema Mpina.

Tunazindua mkakati wa dawati tarehe 15/12/2018 na kwenda kuwakabidhi mitamba 350 kwa wafugaji wa Chama Kikuu-Tanga kama shukurani kwa jitihada za wenzetu wa TADB, Mpina.

Serikali imefanya jitihada kubwa katika kuongeza uzalishaji wa maziwa ili kusaidia wasindikaji wa
maziwa kwa kutekeleza yafuatayo:-

·         kuendelea kuboresha vituo vya Uhimilishaji (AI) kwa kutoa mbegu bora.
·         ujenzi wa maabara ya (embro transfer) inayozinduliwa mwezi Januari, 2019 Mpwapwa.
·         Kudhibiti uingizwaji wa maziwa kutoka Nje kwa kuongeza kodi ili kulinda viwanda vya ndani.
·         Serikali imetoa hekta 10,000 Ruvu kwa ajili ya ufugaji ng’ombe wa maziwa.
·         Serikali itasambaza Madume kwa bei ya ruzuku.
·         Tumehamasisha viwanda vya vyakula vya mifugo.

Tutahakikisha katika maeneo ya wafugaji Huduma zote za Ugani zitatolewa na wataalamu wetu na
zitawafikia kwa ajili ya kujua uzalishaji wa Mifugo, alisema Mpina.

Mhe Waziri aliwasisitizia Wawekezaji kuwa, kuna vijana wamemaliza vyuo mbalimbali vya Mifugo na hawana ajira watumieni kuongeza Uzalishaji.

Naye kwa upande wake Mkurugenzi Kampuni ya Tanga Fresh,Bw. Michael Karata alimpongeza Mhe. Waziri Mpina kwa jitihada za kuwaunga mkono alizozichukua katika sekta hiyo mpaka sasa.

Kampuni hiyo ya maziwa ya Tanga Fresh iliahidi kuongeza Usindikaji wa Maziwa kutoka Lita 45,000 hadi 90,000 kwa siku ifikapo Disemba 2018.

Vilevile Mkurugenzi wa ASAS Bw. Fuad Abri alisema,tunashukuru na kuunga mkono Sekta hii ya maziwa na ndoto ya ASAS sio kuuza Tanzania bali kuuza nje ya Tanzania.

 Tutahakikisha tunaachana na maziwa ya unga na kutumia maziwa ghafi alisisitiza Mkurugenzi wa
Mahusiano, Bw. Hussein Ally AZAM.

 Kwa upande wake Meneja wa TADB Kanda ya Kati Bw. George Nyamrunda alisema, watakopesha
wafugaji na wadau katika kuongeza uzalishaji wa maziwa.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Profesa Elisante Ole Gabriel naye alisisitiza,
Wakurugenzi watumie muda wao kulijua kwa undani na kulisaidia dawati la Sekta binafsi ili liweze
kutekeleza majukumu yake ipasavyo.

Aidha Prof.Gabriel alilitaka Dawati hilo kushirikiana kwa karibu na Kitengo cha Mawasiliano ili
kuelimisha umma juu ya utekelezaji wa shughuli zifanywazo na dawati hilo.

Pia Katibu Mkuu Prof.Gabriel aliiomba Benki ya Maendeleo ya Kilimo Nchini (TADB)iangalie uwezekano wa kusaidia ununuzi wa vifaa vya Kitengo cha Mawasiliano ili kufanikisha utekelezwaji wa mkakati wa Mawasiliano wa Wizara.

Mhe. Waziri na KMM wakilikiliza maswali kutoka kwa wadau wa maziwa ( hawapo pichani)

Mhe. Waziri na KMM wakisikiliza kwa makini malengo ya kampuni ya ASAS


Jumanne, 13 Novemba 2018

MAKATIBU WAKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI WASISITIZA USHIRIKIANO KATI YA WATUMISHI WA SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI.


Kufuatia kikao cha watumishi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, kilichofanyika Leo tar 7/11/2018 katika ukumbi wa VETA DODOMA Katibu Mkuu Mifugo ahamasisha yafuatayo:-

Ushirikiano kati ya watumishi ni jambo la Msingi sana ili kuweza Kufanikisha shughuli zetu za kila siku pia ni lazima tufanye kazi kwa kujituma.

Changamoto siyo sehemu ya maisha ila changamoto ndiyo maisha yenyewe, kwa hiyo tunazitumia hizo changamoto kama fursa.

Wakurugenzi  na  wakuu  wa vitengo  jitahidini sana kuwasikiliza mnaowaongoza ,na  kuwasimamia na kubwa  zaidi kujali maslahi yao.

Nataka Wizara hii iende kwa kasi sana ,Idara ya Uzalishaji na Masoko Ikiwa kama Operating Engine kwa sababu ndiyo yenye activities nyingi sana

Pia napenda kuwataarifu  rasmi  kuwa Dr. Angelo Mwilawa  kuanzia  sasa nimemteua  kuwa Mkurugenzi Rasmi  wa Idara ya Ugani na mafunzo (DRTE) hapo awali alikuwa anakaimu. 

KMU asisitiza Sekta zote mbili kuwa na ushirikiano

KMM akiongea na watumishi ( hawapo pichani) na kusisitiza ushirikiano katika kazi

KMM na KMU wakiteta jambo na Mkurugenzi msaidizi wa Ukuzaji Viumbe kwenye maji




Picha ya pamoja Makatibu Wakuu, Wakurugenzi na Watumishi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi



Makatibu Wakuu, wakiwa naWakuu wa Idara, Vitengo na Tahasisi katika picha ya pamoja

Jumatano, 7 Novemba 2018

PROJECT LAUNCHING WORKSHOP, 07 NOVEMBER,2018. AT MORENA HOTEL DODOMA.

Prof. O. Gabriel receives inception report from Hon. Minister of Agriculture Dkt. Charles Tizeba

Ongoing speech from Permanent Secretary

Picture with Minister of Agriculture, Permanent Secretary, AGRA team and ESRF members

NEW ZEALAND KUWEKEZA KATIKA SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI




Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb), amekutana na Balozi wa New Zealand Nchini Tanzania Mike Burrell Ofisini kwake leo tarehe 06/11/2018 jijini Dodoma.

Tumekuwa tukishirikiana vyema kati ya Nchi ya Tanzania na New Zealand katika kupata madume bora ya Ng’ombe 6 kule kituo cha Taifa cha Uhimilishaji (NAIC) kilichopo UsaRiver jijini Arusha ambayo yamechangia uzalishaji wa mbegu bora kuongezeka zaidi, alisema Mh. Ulega.

Mh.Ulega alisema tutasaidiana katika upande wa ufugaji wa samaki, ambapo wenzetu wako mbele
zaidi katika masuala ya Ukuzaji viumbe kwenye maji.
“ Our President Dkt. John P. Magufuli is trying so hard to ensure that, our environment in Tanzania is
getting better and better”. Say’s Ulega.

Vilevile Mhe. Ulega alisema kunahitajika watu wa kwenda kusoma katika kada ya Sayansi ambapo kwa sasa bado tunapeleka watu wachache katika fani hiyo.

Kwa upande wake balozi Mike alisema, tunahitaji Ushirikiano na Tanzana katika kuwekeza kwenye
Sekta ya Mifugo na Uvuvi.
“We assure to share information and cooperate with you because the country has a huge potential”.
Say’s Hon. Mike.

Tunahitaji wanasayansi kutoka Tanzania wenye elimu ya juu hasa waliobobea katika masuala ya
Sayansi, “ We love to have Scholars in New Zealand from your country, alisema Hon. Mike.

 We encourage people to come and learn more about aquaculture,say’s Hon. Mike.

Naye Katibu Mkuu Mifugo Prof.Elisante Ole Gabriel alisema, NARCO wanahitaji kunufaika na kupata Wataalamu kutoka New Zealand kuhusina na Mifugo katika Uzalishaji.


Naibu Waziri Mhe. Ulega akiongea jambo na Balozi wa New Zealand Nchini Tanzania Mhe. Mike Burrell

Balozi Mike akisalimiana na Wakurugenzi




Jumatatu, 5 Novemba 2018

WAKURUGENZI WAPYA WATAMBULISHWA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI



Katibu Mkuu Mifugo Prof. Elisante Ole. Gabriel leo atambulisha Wakurugenzi wapya katika kikao cha Wakuu wa Vitengo na Idara kilichofanyika katika Ukumbi wa NBC Leo.

# Prof. O. Gabriel, alisisitiza Wakurugenzi kujifunza kwa watu na kuwa na Ushirikiano.

#KM aliwataka Wakurugenzi kuwa wabunifu katika kazi zao ili kuinua Sekta.

# Prof. aliwaomba Wakurugenzi kukabiliana na changamoto zilizopo na kuunganisha nguvu kwa pamoja ili kuzitatua.

# Alisisitiza kujenga utamaduni wa Kushirikiana kwa pamoja na kufanya kazi kwa Ushirikiano.

Katibu  Mkuu Mifugo, Profesa Elisante Ole Gabriel ampongeza na kumkaribisha Kaimu Mkuu mpya wa Kitengo cha Mawasiliano  Serikalini Bi. Rehema ,bulalina, leo katika ukumbi wa NBC


KM Mifugo Profesa Elisante Ole Gabriel ampongeza na kumkaribisha Mkurugenzi mpya wa Idara ya Huduma za Mifugo Dkt. H. Nonga, Leo katika ukumbi wa NBC

KM Mifugo Profesa Elisante Ole Gabriel  ampongeza na kumkaribisha Mkurugenzi mpya wa Idara ya Uzalishaji Mifugo na Masoko Dkt. Felix Nandonde




Wakuu wa Idara na Vitengo wakisikiliza maagizo kutoka kwa KM (hayupo pichani)

























Ijumaa, 2 Novemba 2018

KATIBU MKUU ATEMBELEA SOKO LA SAMAKI FERRY KUKAGUA UJENZI WA VYOO:



Leo Katibu Mkuu wa Uvuvi Dkt. Rashid Tamatama alikwenda kuangalia utekelezaji wa ujenzi wa vyoo 24 hiyo ikiwa ni katika hatua za utekelezaji wa ahadi za Mh. Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh. Luhaga Mpina alipotembelea sokoni hapo na kubaini mapungu yaliyopo ikiwemo.

1. Uchakavu wa majengo
2. Upungufu wa vyoo;
3. Kujaa kwa mchanga katika bahari: na
4. Uchakavuwa jokofu la kuhifadhia samaki

Ambapo alisema kuwa Wizara yake itaingilia kwa kuchukua hatua za haraka katika hayo na kuagiza mara moja kwa ujenzi wa vyoo 24 ambavyo vitapunguza msongamano sokoni hapo.

Katibu Mkuu wa Uvuvi, Dkt. Rashidi Tamatamah ametembelea soko la samaki Ferri- Kivukoni kuangalia ujenzi wa vyoo 24 ambavyo vitapunguza msongamano katika soko hilo.

Katibu Mkuu Uvuvi, akielekea eneo la ujenzi akiambatana na Meneja wa soko  Bw. Mkuu Anje

Katibu Mkuu Uvuvi akiwa katika eneo la Ferry 
Katibu Mkuu akiwa na Meneja wa soko hilo akifafanua jambo sokoni hapo


Choo ambacho kinatumika kwa sasa na kutokana na wingi wa watu hakikidhi maitaji yao

Katibu Mkuu akipata maelezo juu ya ujenzi huo unavyoendelea