Nav bar

Jumanne, 13 Novemba 2018

MAKATIBU WAKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI WASISITIZA USHIRIKIANO KATI YA WATUMISHI WA SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI.


Kufuatia kikao cha watumishi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, kilichofanyika Leo tar 7/11/2018 katika ukumbi wa VETA DODOMA Katibu Mkuu Mifugo ahamasisha yafuatayo:-

Ushirikiano kati ya watumishi ni jambo la Msingi sana ili kuweza Kufanikisha shughuli zetu za kila siku pia ni lazima tufanye kazi kwa kujituma.

Changamoto siyo sehemu ya maisha ila changamoto ndiyo maisha yenyewe, kwa hiyo tunazitumia hizo changamoto kama fursa.

Wakurugenzi  na  wakuu  wa vitengo  jitahidini sana kuwasikiliza mnaowaongoza ,na  kuwasimamia na kubwa  zaidi kujali maslahi yao.

Nataka Wizara hii iende kwa kasi sana ,Idara ya Uzalishaji na Masoko Ikiwa kama Operating Engine kwa sababu ndiyo yenye activities nyingi sana

Pia napenda kuwataarifu  rasmi  kuwa Dr. Angelo Mwilawa  kuanzia  sasa nimemteua  kuwa Mkurugenzi Rasmi  wa Idara ya Ugani na mafunzo (DRTE) hapo awali alikuwa anakaimu. 

KMU asisitiza Sekta zote mbili kuwa na ushirikiano

KMM akiongea na watumishi ( hawapo pichani) na kusisitiza ushirikiano katika kazi

KMM na KMU wakiteta jambo na Mkurugenzi msaidizi wa Ukuzaji Viumbe kwenye maji




Picha ya pamoja Makatibu Wakuu, Wakurugenzi na Watumishi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi



Makatibu Wakuu, wakiwa naWakuu wa Idara, Vitengo na Tahasisi katika picha ya pamoja

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni