Nav bar

Jumatatu, 27 Julai 2020

DKT. TAMATAMAH AKISAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah akisaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa Hayati Benjamin William Mkapa, Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Tatu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mara baada ya kuhudhuria ibada ya misa takatifu ya kumuombea Hayati Mkapa katika uwanja wa uhuru jijini Dar es Salaam. (26.07.2020)

KUELEKEA NANENANE 2020


Jumapili, 26 Julai 2020

KUELEKEA NANENANE 2020


BODI YATAKIWA KUWA BUNIFU KUBORESHA HUDUMA ZA LITA


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel ameitaka Bodi Mpya ya Ushauri ya Wakala ya Vyuo vya Mifugo (LITA) kuwa bunifu ili kuboresha huduma na kuleta tofauti katika shughuli zao na kufikia malengo yake.

Prof. Ole Gabriel aliyasema hayo alipokuwa akifungua kikao kazi cha kwanza cha Bodi mpya ya ushauri ya LITA kilichofanyika jijini Dar es Salaam Julai 25, 2020.

Akizungumza katika kikao hicho, Prof. Gabriel aliwahimiza wajumbe wa bodi hiyo kutumia vyema taaluma zao na kuwa wabunifu katika kuhakikisha LITA inaboresha huduma zake na kuleta mabadiliko chanya ya kiutendaji ya Wakala hiyo.

"Nawaomba bodi mfanye kazi yenu vizuri na mfanye maboresho kadri itakavyowezekana, shirikianeni kwa ukaribu na wadau wengine ili kusaidia kuboresha shughuli zenu," alisema Prof. Gabriel.

Sambamba na hilo, Prof. Gabriel ameitaka bodi hiyo kuhakikisha inasimamia vyema rasilimali fedha za taasisi hiyo huku akiwaeleza kuwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Luhaga Mpina wakati wote amekuwa mkali na watu ambao wamekuwa wanatumia vibaya rasilimali za umma.

Aliendelea kueleza kuwa LITA wanaweze kufanikiwa katika shughuli zao endapo wataweka mikakati ya kuboresha eneo la masoko na habari ambalo litasaidia kutangaza na kuhamasisha jamii kupitia vyombo vya habari kutumia huduma zinazotolewa na LITA na kwa njia hiyo wataongeza mapato.

"Hii ni taasisi ya biashara hivyo ni muhimu kuitangaza vya kutosha ili watu waijue LITA ni nini, ipo wapi na inafanya nini, kwa kufanya hivyo kutaivuta jamii kutumia huduma zenu," alifafanua Prof. Gabriel.

"Serikali inayoongozwa na Dkt. John Pombe Joseph Magufuli imefanya kazi kubwa mpaka sasa tumeingia katika uchumi wa kati, hivyo LITA ni lazima muhakikishe mnaenda sambamba na kasi hii ya uchumi wa kati kwa kuboresha huduma zenu ikiwemo kubuni vyanzo vingine vya mapato," aliongeza Prof. Gabriel.

Akiongea mapema katika kikao hicho, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji  Wakala ya Vyuo vya Mifugo (LITA), Dkt. Pius Mwambene alisema kuwa mpaka sasa taasisi hiyo imepata mafanikio kadhaa ikiwemo kuongezeka kwa udahili wa wanafunzi kutoka 798 mwaka 2012/13 hadi kufikia 3642 mwaka 2019/2020 huku akisema kuwa wameshaongeza Kampasi nyingine mbili ambazo ni Mabuki, Mwanza na Kikulula, Kagera.

"Kuanzia Mwaka jana tumeanza kutoa gawio katika mfuko mkuu wa Serikali ambapo tulianza kutoa kiasi cha shilingi milioni 50 mwaka jana na mwaka huu tumetoa milioni 100,"alifafanua Dkt. Mwambene

Naye, Mwenyekiti wa Bodi ya LITA, Prof. Malongo Mlozi alisema kuwa kufuatia kauli hiyo ya Katibu Mkuu watahakikisha kuwa wataweka utaratibu kwa kushirikiana na Menejimenti kuangalia mapato na matumizi ya fedha kila miezi mitatu, huku akieleza kuwa kwa nafasi yao wataendelea kutoa ushauri juu ya matumizi bora ya rasilimali umma.

Kuhusu suala la ubunifu alisema kuwa wataweka mipango mizuri kuhakikisha taasisi hiyo kupitia Kampasi zake inajiendesha kibiashara ili kujiongezea kipato.



Mjumbe wa Bodi ya Ushauri ya Wakala ya Vyuo vya Mifugo (LITA), Bi. Josephine Matiro akipitia Makabrasha katika kikao cha kwanza cha bodi hiyo kilichofanyika jijini Dar es Salaam. (25.07.2020)



Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya Wakala ya Vyuo vya Mifugo (LITA) muda mfupi baada ya kufungua kikao chao cha kwanza kilichofanyika jijini Dar es Salaam. Kulia (waliokaa) ni Mwenyekiti wa Bodi ya LITA, Prof. Malongo Mlozi na Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa LlTA, Dkt. Pius Mwambene. Waliosimama kutoka kulia ni wajumbe wa Bodi hiyo, wa kwanza ni Dkt. Angello Mwilawa, wa pili ni Bi. Josephine Matiro, katikati ni Prof. Zacharia Masanyiwa. Kutoka kushoto (wa kwanza) ni Bw. Mark Tsoso na wa pili ni Bi. Faraja Makafu.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel (kushoto) akifurahia jambo na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala ya Vyuo vya Mifugo (LITA), Dkt. Pius Mwambene muda mfupi baada ya kufungua kikao cha kwanza cha Bodi ya Ushauri ya LITA kilichofanyika jijini Dar es Salaam (25.07.2020)


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel (kulia) akiteta jambo na Kaimu Mkurugenzi wa Wakala ya Vyuo vya Mifugo (LITA), Dkt. Pius Mwambene katika kikao cha kwanza cha Wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya LITA kilichofanyika jijini Dar es Salaam. (25.07.2020)


Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wakala ya Vyuo vya Mifugo (LITA), Prof. Malongo Mlozi (aliyesimama) akiongea na Wajumbe wa bodi hiyo wakati alipokuwa akiongoza kikao chao cha kwanza kilichofanyika jijini Dar es Salaam. (25.07.2020)


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel akiongea na Wajumbe wa Bodi Mpya ya Ushauri ya Wakala ya Vyuo vya Mifugo (LITA) wakati akifungua kikao cha kwanza cha bodi hiyo kilichofanyika jijini Dar es Salaam. (25.07.2020)

Ijumaa, 24 Julai 2020

MAKATIBU WAKUU WAKUTANA KUJADILI MAANDALIZI YA NANE NANE 2020


Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Kusaya leo (24.07.2020) ameongoza kikao cha Makatibu Wakuu wa wizara za kisekta kujadili maandalizi ya Maonesho ya Kilimo Nane nane yatakayofanyika kitaifa mkoani Simiyu kuanzia tarehe 01 Agosti, 2020.

Katika kikao hicho, Bw. Kusaya  alieleza kuwa ni matarajio ya wizara ya kilimo na zile za kisekta kuona maonesho ya Nane nane mwaka huu yanakuwa tofauti katika kuleta mapinduzi ya, ufugaji na uvuvi ili wananchi wapate kuongeza tija na ufanisi kukuza uchumi wa kaya na taifa.

Kikao hicho kimehusisha Makatibu Wakuu ambao ni Prof. Riziki Shemdoe (Viwanda na Biashara), Prof. Elisante Ole Gabriel (Mifugo), Mhandisi Anthony Sanga (Maji) na Dkt. Rashid Tamatamah (Uvuvi) na Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Miriam Mmbaga pamoja na kamati ya maandalizi.

“Tunapenda kuona maonesho ya Nane nane mwaka huu yanakuwa tofauti na yaliyopita katika kuwafanya wakulima, wafugaji na wavuvi  wabadilike kutoka katika  kilimo cha kujikimu kuwa kilimo, ufaguji na uvuvi wa kibiashara kupitia  elimu na teknolojia bora watakayojifunza kutoka kwa wataalam “ alisema Kusaya.

Kikao kimezishauri Wizara, taasisi na wadau wa maonesho ya mwaka huu kujikita katika kuwasaidia wakulima,wavuvi na wafugaji kuongeza tija katika shuguli zao ili baada ya maonesho maisha yao yawe bora zaidi kiuchumi.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel alisema wakulima wanahitaji elimu ya kubadilisha mtizamo hivyo matumizi ya vyombo vya habari kufikisha elimu kwa wakulima, wafugaji na wavuvi ni muhimu sana kwenye maonesho haya.

Naye Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Prof. Riziki Shemdoe alisema ni vema kamati ya uratibu ikaweka utaratibu wa kuwakutanisha wafanyabiashara za mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi pamoja na wakulima kwenye maonesho hayo hususan Simiyu.

“Tuandae maeneo kwa ajili wa wafanyabiashara na wakulima, wafugaji na wavuvi kufanyia mazungumzo ya kukuza upatikanaji wa masoko na kutumia fursa za biashara ikiwemo kuwekeza katika viwanda” alisisitiza Prof. Shemdoe.

Maonesho ya Kilimo Nane nane mwaka huu yana kauli mbiu isemayo “Kwa Maendeleo ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Chagua Viongozi Bora 2020”.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ol Gabriel akizungumza katika kikao cha Makatibu Wakuu wa wizara za kisekta kuhusu maandalizi ya maonesho ya Nane nane 2020 yatakayofanyika kitaifa mkoani Simiyu. Kikao kimefanyika katika mji wa serikali Mtumba katika ukumbi wa Wizara ya Kilimo.  (24.07.2020)

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Kusaya akiongoza kikao cha Makatibu Wakuu wa Wizara za kisekta kuhusu maandalizi ya maonesho ya Nane nane 2020 yatakayofanyika kitaifa mkoani Simiyu. Kikao kimefanyika katika mji wa serikali Mtumba katika ukumbi wa Wizara ya Kilimo.  ( 24.07.2020)

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah akizungumza katika kikao cha Makatibu Wakuu wa wizara za kisekta kuhusu maandalizi ya maonesho ya Nane nane 2020 yatakayofanyika kitaifa mkoani Simiyu. Kikao kimefanyika katika mji wa serikali Mtumba katika ukumbi wa Wizara ya Kilimo. (24.07.2020)

Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Prof. Riziki Shemdoe akizungumza katika kikao cha Makatibu Wakuu wa wizara za kisekta kuhusu maandalizi ya maonesho ya Nane nane 2020 yatakayofanyika kitaifa mkoani Simiyu. Kikao kimefanyika katika mji wa serikali Mtumba katika ukumbi wa Wizara ya Kilimo.  (24.07.2020)

Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Anthony Sanga akizungumza katika kikao cha Makatibu Wakuu wa wizara za kisekta kuhusu maandalizi ya maonesho ya Nane nane 2020 yatakayofanyika kitaifa mkoani Simiyu. Kikao kimefanyika mji wa serikali Mtumba katika ukumbi wa Wizara ya Kilimo. (24.07.2020)

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu Bibi Miriam Mmbaga akizungumza kwenye kikao cha Makatibu Wakuu wa wizara za kisekta kuhusu maandalizi ya ya maonesho ya Nane nane 2020 yatakayofanyika kitaifa mkoani Simiyu. Kikao kimefanyika katika mji wa serikali Mtumba katika ukumbi wa Wizara ya Kilimo  (24.07.2020)

Sehemu ya wajumbe wakifuatilia kikao cha Makatibu Wakuu wa wa wizara za kisekta kuhusu maandalizi ya ya maonesho ya Nane nane 2020 yatakayofanyika kitaifa mkoani Simiyu. Kikao kimefanyika katika mji wa serikali Mtumba katika ukumbi wa Wizara ya Kilimo. ( 24.07.2020)

TANZIA


KUELEKEA NANENANE 2020


Alhamisi, 23 Julai 2020

WARSHA YA KAMATI YA KITAIFA YA MWONGOZO WA HIARI WA KUHAKIKISHA UVUVI MDOGO UNAKUWA ENDELEVU


Picha ya Pamoja ya baadhi ya Washiriki wa warsha ya kutoa maoni juu ya Mwongozo wa Hiari wa kuhakikisha Uvuvi Mdogo unakuwa endelevu iliyofanyika katika Kata ya Kilwa Kivinje,Halmashauri ya Kilwa Masoko. (22.07.2020)



Mratibu wa Mpango wa Mwongozo wa Hiari wa kuendeleza Uvuvi Mdogo, Bi. Lilian Ibengwe (picha ya pili kulia) akikusanya Maoni ya wadau kwenye Warsha ya kutoa Maoni ya Wadau wa Uvuvi Mdogo katika Kata ya Kilwa Kivinje,Halmashauri ya Kilwa Masoko. (22.07.2020)



Mdau wa Uvuvi Mdogo, Bw.Faridu Shaweji wa Kilwa Kivinje akitoa Maoni yake leo kwenye Warsha ya utoaji maoni kwenye Warsha ya kutoa Maoni ya Wadau wa Uvuvi Mdogo katika Kata ya Kilwa Kivinje, Halmashauri ya Kilwa Masoko. (22.07.2020)


Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Mwongozo wa Hiari wa kuhakikisha Uvuvi Mdogo unakuwa endelevu, Bw.Yahaya Mgawe akitoa maelezo kwenye Warsha ya kutoa Maoni ya Wadau wa Uvuvi Mdogo katika Kata ya Kilwa Kivinje, Halmashauri ya Kilwa Masoko. (22.07.2020)

KUELEKEA NANENANE 2020


Jumanne, 21 Julai 2020

NANENANE 2020


NARCO YAMSIMAMISHA KAZI MENEJA WEST KILIMANJARO


Kaimu Meneja Mkuu wa Kampuni ya Ranchi ya Taifa (NARCO), Masele Mipawa amemsimamisha kazi Meneja wa Ranchi ya West Kilimanjaro iliyopo Kilimanjaro, Hezron Kyaruzi kwa tuhuma za kukosa uadilifu kwa mali za Umma na kusababisha upotevu wa Ng’ombe takriban 32.

Akiwa katika ziara ya kutembelea Ranchi hiyo ya West Kilimanjaro Mipawa alisema kuwa waliamua kufanya maamuzi hayo kufuatia changamoto nyingi zinazolikumba shamba hilo ambazo kwa kiasi kikubwa zimechangiwa na uongozi mbovu wa meneja huyo.

“Kutokana na upotevu wa Ngombe, uzembe na ukosefu wa maadili tumeamua kumsimamisha kazi Meneja wa Ranchi na Msaidizi wake na hatua nyingine za kisheria na kinidhamu zitafuata ", alisema Mipawa

Mipawa alisema ziara hiyo aliyoifanya katika Ranchi hiyo ilikuwa na lengo la kufanya ukaguzi kutokana na taarifa walizokuwa wakizipata ambazo zilionesha kuwa katika shamba hilo kumetokea upotevu wa Ng’ombe ambao Kampuni ya NARCO haina taarifa nao.

Ziara hii pia imesaidia kubaini kuwa kuna wizi uliokithiri katika shamba hili ambao umechangiwa na mahusiano mabovu kati ya Meneja na jamii inayolizunguka shamba hilo, ukosefu wa maadili na uadilifu wa Meneja ambao umepelekea  Ngombe 32 kupotea.

Kati ya ngombe hao 32 waliopotea 15 wameshapatikana na wengine 17 hawajapatikana mpaka sasa huku ngombe wengine 27 walichinjwa bila kibali cha makao makuu, alifafanua Mipawa

Kufuatia hali hiyo, Mipawa alisema wameamua pia kumsimamisha kazi Msaidizi wake kwa kuwa alishindwa kumshauri vizuri meneja huyo huku ikidaiwa alikuwa akishirikiana na meneja huyo kwenda kuazima ngombe kwa watu binafsi ili Ranchi hiyo ionekane ina idadi kubwa ya ngombe.

Aidha, Mipawa aliwataka wafanyakazi wengine waliobaki katika shamba hilo kuendelea kufanya kazi kwa bidii, wazingatie nidhamu na uzalendo huku akiwaonya kuwa Serikali ya Awamu ya Tano haitavumilia mtu yeyote anayehujumu rasilimali za Taifa.



Kaimu Meneja Mkuu - NARCO, Bw. Masele Mipawa (aliyevaa suti nyeusi) akiongea na wafanyakazi wa Ranchi ya West Kilimanjaro wakati alipokwenda kuangalia maendeleo ya ranchi hiyo. (18.07.2020)



Kaimu Meneja Mkuu - NARCO, Bw. Masele Mipawa akiwa amepanda farasi ambao wapo katika ranchi ya West-Kilimanjaro wakati alipokwenda kukagua maendeleo ya ranchi hiyo. (18.07.2020)



Kaimu Meneja Mkuu - NARCO, Bw. Masele Mipawa akiongoza kikao cha watumishi wa Ranchi ya West-Kilimanjaro wakati alipokwenda kukagua maendeleo ya ranchi hiyo. (18.07.2020)

Kaimu Meneja Mkuu - NARCO, Bw. Masele Mipawa akiongoza kikao cha watumishi wa Ranchi ya West-Kilimanjaro wakati alipokwenda kukagua maendeleo ya ranchi hiyo. (18.07.2020)

SIJARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI - DKT. TAMATAMAH.


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah hajaridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa Jeongo la Utawala la Ofisi ya Hifadhi ya Bahari na Maeneo Tengefu (MPRU) unaoendelea katika Kisiwa cha Mafia.

Dkt. Tamatamah aliyasema hayo baada ya kukagua kazi za ujenzi zinazoendelea ambapo hakuridhishwa na kasi ya ujenzi kwani haiendani na muda uliotumika kwa mujibu wa mkataba.

"Sijaridhishwa na kasi ya ujenzi niliyoikuta hapa hivyo ninakuagiza mkandarasi kuhakikisha unazingatia ratiba na muda uliopangwa kulingana na mkataba" Alisisitiza Dkt. Tamatamah.

Jengo hilo linasimamiwa na mkandarasi mwelekezi "Y&P architects" linatarajiwa kutumiwa na MPRU kama ofisi mara baada ya kukamilika kwake ambapo litasaidia kuongeza ufanisi wa taasisi hiyo.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah (kushoto), baadhi ya watendaji wa sekta ya Uvuvi na baadhi ya watendaji wa kampuni ya "Y & P Architects" wakiangalia hatua ya ujenzi iliyofikiwa kwenye jengo la Utawala la Ofisi ya Hifadhi ya Bahari na Maeneo Tengefu (MPRU) lililopo kwenye kisiwa cha Mafia jana (18.07.2020).

MSAJILI WA BARAZA LA VETERINARI AKAGUA BAADHI YA MADUKA YA HUDUMA ZA PEMBEJEO ZA MIFUGO - DODOMA


Msajili wa Baraza la Veterinari Tanzania, Dkt. Bedan Masuruli akikagua moja ya Duka la utoaji huduma za Pembejeo za Mifugo la Blessing Agrovet Techical. Kushoto ni Bi.  Upendo Hamisi ambae ni mtoa huduma katika duka hili. (17.07.2020)



Msajili wa Baraza la Veterinari picha ya kwanza (kulia) akifunga Duka la Blessing Agrovet Technical kwa kufuli lake. Wa kwanza kushoto ni mtoa huduma za Mifugo katika duka hilo, Bi. Upendo Hamisi akitii amri ya kufunga duka kwa kufuli kutokana na kushindwa kutimiza baadhi ya masharti muhimu ya utoaji huduma kwa kutokuwa na daktari wa mifugo aliyesajiliwa na kutohuisha jina la mtoa huduma katika Baraza la Vetenari ili awe kuwa na uhalali wa kutoa huduma. (17.07.2020)


Msajili wa Baraza la Veterinari picha ya kwanza (kulia) akifunga Duka la Blessing Agrovet Technical kwa kufuli lake. Wa kwanza kushoto ni mtoa huduma za Mifugo katika duka hilo, Bi. Upendo Hamisi akitii amri ya kufunga duka kwa kufuli kutokana na kushindwa kutimiza baadhi ya masharti muhimu ya utoaji huduma kwa kutokuwa na daktari wa mifugo aliyesajiliwa na kutohuisha jina la mtoa huduma katika Baraza la Vetenari ili awe kuwa na uhalali wa kutoa huduma. (17.07.2020)

Jumapili, 19 Julai 2020

ZIARA YA KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI (MIFUGO) WILAYANI KONGWA


Picha ya pamoja ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo, Prof. Elisante Ole Gabriel, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI), Dkt. Elligy Shirima, uongozi wa taasisi ya PASS, pamoja na wafanyakazi wa TALIRI na vijana wanaopatiwa mafuzo ya ufugaji bora wa mbuzi na PASS. (17.07.2020)



Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel (aliyesimama) akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) Wilaya ya Kongwa pamoja na vijana wanaopatiwa mafunzo ya unenepeshaji wa mbuzi na taasisi ya PASS, ambapo amewataka kuhakikisha mafunzo hayo yanakuwa chanzo cha wao kujiajiri na kuajiri vijana wengine kupitia ufugaji. (17.07.2020)



Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel (akitembelea) jengo la kituo cha mauzo ya nyama ya mbuzi linalojengwa katika kituo cha Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) Wilaya ya Kongwa kwa kushirikiana na taasisi ya PASS ambayo pia inatoa mafunzo kwa vijana namna ya kunenepesha mbuzi na kufanya biashara ya ufugaji kwa tija. (17.07.2020)



Muonekano wa shamba la malisho ya mifugo la Bw. Mnyonaki Saileni lililopo Kijiji cha Msujile Kata ya Sejeli Wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma, ambapo Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel ameridhishwa na ubora wa malisho hayo. (17.07.2020)



Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel (aliyesimama katikati) akikagua moja ya mbegu bora ya mbuzi alipotembelea shamba la mifugo la Bw. Mnyonaki Saileni (wa kwanza kulia) alipofanya ziara katika shamba lake lililopo Kijiji cha Msujile Kata ya Sejeli Wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma. aliyesimama kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI), Dkt. Elligy Shirima. (17.07.2020)



Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel akikagua viwele vya moja ya ng'ombe wa Bw. Mnyonaki Saileni (hayupo pichani) baada ya kutembelea shamba la malisho la mfugaji huyo lililopo Kijiji cha Msujile Kata ya Sejeli wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma ambapo aliridhishwa na ubora wa mifugo yake kutokana na kupatiwa malisho bora. (17.07.2020)



Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel (aliyevaa miwani) akikagua malisho ya mifugo katika shamba la mifugo la Bw. Mnyonaki Saileni (aliyeshika fimbo) alipofanya ziara katika shamba lake lililopo Kijiji cha Msujile Kata ya Sejeli wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma ambapo aliitaka Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) kuongeza wigo kwa wafugaji kuwa na mashamba ya malisho. (17.07.2020)

SAUTI YETU WIKI HII


SAUTI YETU WIKI HII


DKT. NANDONDE ATEMBELEA KIWANDA CHA MOTHER DAIRIES LIMITED


Mkurugenzi wa uzalishaji na Masoko kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Felix Nandonde jana alitembelea kiwanda cha kusindika maziwa cha Mother Dairies Limited kilichopo Wilaya ya Rufiji mkoani Pwani.

Katika ziara hiyo ya kikazi Meneja wa uzalishaji wa kiwanda hicho Bw. Alle Makene alimweleza Dkt. Nandonde kuwa kiwanda kina uwezo wa kusindika lita za maziwa 5000 kwa siku na sasa kinasindika lita 2000 kwa siku sawa na asilimia 40 ya uwezo wa kiwanda hicho.

Kituo kinakusanya maziwa kutoka kwa wafugaji kupitia vituo vitatu (Milk collection centres) ambapo kiwanda kinanunua maziwa kwa bei ya shilingi 900 kwa lita moja kutoka kwa wafugaji.

Kiwanda cha Mother Dairies Limited kinatengeneza maziwa fresh na mtindi ambayo huuzwa katika masoko ya mikoa ya Lindi, Dar es Salaam na Pwani.

Kiwanda hicho kina utaratibu wa kuuza maziwa kabla ya kuwekwa kwenye vifungashio (bulk sale) kwa bei ya shilingi 1200 kwa lita moja ya maziwa fresh na shilingi 1300 kwa maziwa ya mtindi.

Aidha, Bw. Makene alieleza kuwa changamoto za tasnia ya maziwa ni pamoja na;
I. Upatikanaji wa maji baada ya mfumo wa maji wa Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji kuharibika tangu Mwezi Machi, Mwaka 2020 na;
II. Ubovu wa miundombinu ya barabara



Picha ya pamoja ya uongozi wa kiwanda cha kusindika maziwa Mother Dairies Limited ukiwa na Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Mazao ya Mifugo, Usalama wa Chakula na Lishe, Bw. Gabriel Bura (wa kwanza kushoto) na Mkurugenzi wa Uzalishaji na Masoko Dkt. Felix Nandonde wote kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi mara baada ya kufanya ziara ya siku moja katika kiwanda hicho kilichopo wilaya ya Rufiji mkoani Pwani baada ya kukagua uzalishaji wa bidhaa ya maziwa. (16.07.2020)



Kipimo kinachotumika kukagua ubora wa maziwa kabla ya kusindikwa katika kiwanda cha Mother Dairies Limited kilichopo wilaya ya Rufuji mkoani Pwani. (16.07.2020)

Mkurugenzi wa Uzalishaji na Masoko kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Felix Nandonde (wa kwanza kushoto) akipata maelezo ya namna kiwanda cha kusindika maziwa cha Mother Dairies kinavyofanya kazi kutoka kwa meneja uzalishaji wa kiwanda hicho, Bw. Alle Makene. (16.07.2020)


Sehemu ya vifungashio vya maziwa vinavyotumiwa na kiwanda cha kusindika maziwa cha Mother Dairies kilichopo Wilaya ya Rufiji Mkoani Pwani. (16.07.2020)

ZIARA YA KATIBU MKUU UVUVI - FETA & TAFIRI


Mkandarasi kutoka kampuni ya PETRA ENGINEERING, Eng. Basem Abu Ghalyoun akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (wa pili kutoka kulia mbele) wakati wa ziara yake aliyoifanya ya kukagua maendeleo ya ujenzi kwenye taasisi hiyo Dar es Salaam. (16.07.2020)



Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (kushoto) akioneshwa michoro ya jengo la   Taasisi ya Utafiti wa masuala ya Uvuvi (TAFIRI) wakati wa ziara yake aliyoifanya kwenye taasisi hiyo na Chuo cha Uvuvi (FETA). (16.07.2020)



Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (wa nne kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Menejiment ya chuo cha Uvuvi (FETA) wakati wa ziara yake chuoni hapo. (16.07.2020)