Nav bar

Jumanne, 19 Juni 2018

TAHARIFA KWA UMMA KUHUSU TAHADHARI YA MLIPUKO WA UGONJWA WA HOMA WA BONDE LA UFA (RVF)



Ugonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa (RVF) ni ugonjwa hatari kwa binadamu na mifugo hususan ng’ombe, mbuzi, kondoo na ngamia ambao husababishwa na virusi jamii ya Bunyaviridae. Wanyama huambukizwa kwa kuumwa na mbu aina ya ‘Aedes”. Binadamu hupata ugonjwa kwa kushika au kula nyama ya mnyama aliyeambukizwa na virusi vya ugonjwa huo

Katika  siku za hivi Mamlaka ya Hali ya Hewa Kenya, Shirika la Afya ya Wanyama Duniani (OIE) na Shirika la Afya  Duniani (WHO) wametoa taarifa za matukio ya ugonjwa wa  Homa ya Bonde la Ufa (RVF) Kaskazini mwa Kenya na Mashariki mwa nchi ya Rwanda. Hata hivyo Ugonjwa huo haupo hapa nchini.

Kutokana na kuwepo kwa ugonjwa huu katika nchi jirani, Wizara inatoa  maelekezo  yafuatayo kwa Halmashauri zote nchini (Idara za Mifugo, Afya na Elimu) na mikoa yote kuzingatia yafuatayo ili kuchukua tahadhari zote zinazotakiwa ili ugonjwa huu usiweze kuingia nchini.


(a)      Halmashauri zianze kutoa taarifa na elimu kwa umma, hasa kwa wadau wote wanaofanya shughuli za Mifugo, Utoaji wa huduma za Afya n.k. juu ya njia za kudhibiti maambukizi au mlipuko wa ugonjwa huu.

(b)     Halmashauri kuhimiza Wafugaji kuogesha mifugo yao mara kwa mara kwa kutumia viuatilifu (vyenye kiini cha pareto/pyrethroids) ili kudhibiti kupe, mbu, mbung’o na visumbufu wengine waenezao magonjwa. 

(c)      Kuwaagiza Wananchi kutoa taarifa haraka kwa Wataalamu wa Mifugo, Vituo vya Huduma za Afya au Vituo vya Uchunguzi wa Magonjwa ya Mifugo mara wanapoona vifo vingi vya ghafla kwa wanyama, kutupa au kuharibu mimba na wengine kuzubaa kwa homa kali.

(d)     Halmashauri kutoa elimu kwa Umma na kuhahakisha wanyama wote wanachinjiwa machinjioni na wapimwe na nyama yao pia ipimwe na Mtaalamu wa Mifugo kabla na baada ya kuchinjwa. Aidha, nyama zinunuliwe kwenye bucha au super-markets zilizoidhinishwa na sio mitaani.

(e)      Kamati za majanga/maafa za Wilaya ziimarishwe na kwa kushirikiana na Wadau wengine wafuatilie mwenendo na matukio ya magonjwa katika Wilaya zao na kutoa taarifa kwa Wizara husika


IMETOLEWA NA:


Dkt. Mary S.H.  Mashingo

KATIBU MKUU (MIFUGO)

WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI










Ijumaa, 8 Juni 2018

ZIARA YA NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI YA KUTEMBELEA WAFUGAJI WA SAMAKI NA WAZALISHAJI WA CHAKULA CHA SAMAKI KATIKA MKOA WA PWANI.


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega lifanya Ziara yake katika Wilaya za Kibaha na Bagamoyo ya kuwatembelea wadau wa Ukuzaji viumbe kwenye maji ambapo walipata fursa ya kueleza shughuli wanazozifanya pamoja na changmoto wanazozikabili, hivyo lengo la ziara hiyo ni kukagua shughuli zilizopo katika Sekta ya Uvuvi.
Naibu Waziri alianza ziara yake kwa kuwatembelea na kuongea na wamiliki pamoja na wafanyakazi wa Shamba la Ufugaji wa Samaki la Ruvu Wilaya ya Kibaha Kata ya Mbwawa ambapo alipata fursa a kusikiliza shughuli zao na changamoto zinazowakabili ikiwemo upatikanaji wa Chakula cha samaki.
Meneja wa Shamba la Ruvu Bw. Kumbo alisema katika taarifa yake tatizo kubwa linalowakabili ni upatikanaji wa chakula cha kuku pamoja na suala la umeme."
"Tunashindwa kumudu gharama za umeme ni kubwa sana kwa mwezi mmoja gharama yake ni milioni 3, vilevile katika chakula cha samaki tunalazimika kuagiza nje ya nchi kwakuwa chakula cha hapa hakina kiwango kinachotakiwa badala yake samaki hutumia muda mrefu  kuvuna".
Aliendelea kusema tunatakiwa kuvuna samaki kwa Mwaka mara 2 , tukitumia chakula cha hapa tunavuna mara 1 kwa mwaka na samaki anachukua muda wa miezi 9 mpaka kukua lakini tukiagiza tunavuna mara mbili, samaki wanatumia miezi  6 mpaka kuku, tunataka tuwekeze katika ufugaji huu lakini formula ndo tatizo letu kubwa alisisitiza
Mhe. Ulega alisema vikwazo vya namna hii tutaviondo, tutaona ni namna gani ya kuweza kupata chakula bora hapa kwetu sio mpaka tuagize, pia suala la umeme kuanzia sasa naagiza Meneje wa Tanesco waje kushughulikia umeme hadi niwe nimepata majibu wamefikia wapi.
Pia Mhe. Ulega alipata fursa ya kuwatembelea na kuongea na Wanachama wa Chama cha Ukulima na Umwagiliaji (CHAURU) kilichopo Ruvu na akapata fursa ya kuongea na wamiliki wa mabwawa ya samaki ambapo kilio chao kikubwa kilikuwa ni namna ya upatikanaji wa vifaranga vya samaki na masoko.
Bi. Anzelina Masawe mmoja wa mmiliki wa mabwawa ya samaki  alisema pia suala la elimu juu ya ufugaji bora wa samaki wamekosa, hivyo aliomba wasaidiwe kupatiwa utaalamu zaidi wa kufuga samaki na pia upatikananji wa vifaranga vya samaki umekuwa ni washida.
"Tunatakiwa kuvuna Tani laki 7 za samaki kwa mwaka lakini uwezo wetu wa Tanzania ni Tani laki 3.5, kwahiyo kuna upungufu wa Tani laki 3.5 ambapo zinahitajika, kwahiyo ni fursa kwetu kuzalisha kwa wingi na kwa upande wa vifaranga wenzetu wa FETA wanavifaranga wanauza shilingi 50 mkachukue kwa ajili ya kufuga alisistiza Mhe. Ulega".
Naibu Waziri alitembelea pia kiwanda cha kuzalisha vyakula vya kuku na samaki inachoitwa Hill group, kilichopo Mapinga Wilaya ya Bagamoyo. Kampuni hiyo inajihusisha na kutengeneza viroba vya kupakia bidhaa za viwanda na vilevile utengenezaji wa vyakula vya mifugo kwa kutumia mashine za kisasa zaidi  ambapo alifurahishwa na kiwanda hicho kwa kuwa na tekinolojia ya juu zaidi
Meneja wa kampuni hiyo Bw. Hillary Shoo alisema wanazalisha Tani 18 kwa saa moja kwa chakula cha mifugo na Tani 1 kwa chakula cha samaki kinachoelea juu ya maji ambapo kinatumia muda wa dakika 15 ili samaki aweze kula.
Aliendelea kusema Meneja kuwa shida inayowakabili ni elimu ya watengenezaji wa vyakula bora (Feed Millers) pia kwenye operesheni zinazoendelea faini imekuwa tatizo kuna viwanda vimefungwa, imeathiri wenye mitaji midogo ambapo wanatakiwa kulipa faini ndani ya masaa 24 kitu ambacho ni kipo nje ya uwezo wao.
"Nafahamu eneo hili la chakula cha mifugo ni nyeti na katika moja ya azimio tuliojiwekea ni eneo la ufugaji samaki na kuku, asilimia 80 ya Watanzania ni wafugaji wa kuku katika Sekta hii ya ufugaji haifanyi vizuri sana, kilio kikubwa ni upatikanaji wa vifaranga bora alisema Naibu Waziri".
Hivyo, sisi tumejipanga vizuri na tumevipa nguvu vituo vyetu vya kuzalisha na kutotolesha vifaranga Naliendele - Mtwara, Kibinzi - Kigoma, Feta - Mbegani na Nyegezi mwanza na ukiacha hivi vikundi pia tunao watu binasi wa kuweza kutusaidia katika Sekta yetu.


 
Mhe. Naibu Waziri akiongea na wafanyakazi wa shamba la ufugaji wa Samaki la Ruvu Kata ya Mbawa Wilaya ya Kibaha alipotembea kuona shughuli zao za uzalishaji

Mhe. Ulega  akiwa na Meneja wa Ruvu Fish Farm Bw. Kumbo akiwa amefuatana na Mkirugenzi Msaidizi Ukuzaji viumbe kwenye maji Bi. Ritha  wakikagua shamba na akipewa maelezo ya shughuli wanazozifanya