Nav bar

Jumatatu, 5 Septemba 2011

MAONYESHO YA MIFUGO KATIKA VIWANJA VYA NANENANE ZUGHUNI DODOMA 2011



Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda (MB) akisalimia wananchi wakati wa Uzinduzi wa Maonyesho ya kwanza ya paredi ya mifugo. Paredi hiyo ilihusisha ng'ombe wa Maziwa na Nyama katika viwanja vya Nanenane Nzughuni Dodoma  tarehe 05/08/2011


Waziri Mkuu, akiteta jambo na Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt David Mathayo David (MB) wakati wa kuzindua na kuangalia maonyesho ya mifugo. 

Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt David Mathayo David akisoma Hotuba wakati wa Uzinduzi wa Maonyesho ya Mifugo katika viwanja vya Nanenane Nzughuni - Dodoma

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Mhe. Benedict Ole Nangoro (MB) mwenye miwani na pembeni ni Naibu Katibu Mkuu Dkt Yohana Budeba wakifatilia jambo wakati wa maonyesho ya mifugo.

Mhe. Waziri Mkuu akikaribishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe.Eng.  James Nsekela (kushoto kwa Waziri Mkuu) na kulia kwake ni Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. George Huruma Mkuchika

Moja ya ng'ombe wa maziwa aliyeshiriki kweny mashindano , nyuma ni mtumishi aliyemuongoza ng'ombe kwenye paredi.

Ngombe huyu alishiriki kwenye ushindani wa ng'ombe wa maziwa na pembeni wa waongozaji wa ngo'ombe huyo kwenye paredi

Dume la ng'ombe likipita mbale ya Waziri Mkuu na majaji ili kupata maksi za ushindani wa ng'ombe wa Nyama

Ngombe wa Maziwa akiwa kwenye chumba tayari kwa kupelekwa kwenye paredi kupewa alama anazostahili ili kupata washindi.


Mhe. Waziri Mkuu na viongozi aliofatana nao akipata maelezo muhimu ya ng'ombe aliyepo mbele yao kutoka kwa wahusika wa ngombe huyo.