Nav bar

MATANGAZO



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI

                               



RUZUKU KWA WAVUVI

TAARIFA KWA UMMA

Serikali  kupitia Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi imetenga kiasi cha fedha katika mwaka 2013/2014 kwa ajili ya kutoa  ruzuku kwa jamii za wavuvi. Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, anawatangazia wananchi kuwa, Serikali itatoa ruzuku kwa vyama vya ushirika wa wavuvi, vikundi vya wavuvi na Vikundi vya Usimamizi Shirikishi wa Rasilimali za Uvuvi (BMUs) vilivyosajiliwa kuanzia mwaka wa fedha 2013/2014.

Vigezo na masharti yatakayotumika kutoa ruzuku ni kama ifuatavyo:-

1.     Ruzuku itatolewa kwa vyama vya ushirika vya wavuvi, vikundi vya wavuvi na Vikundi vya Usimamizi  Shirikishi wa Raslimali za Uvuvi  vilivyosajiliwa kisheria,  na vyenye  kuzingatia jinsia;
2.     Kikundi kiwe kinafanya kazi  za uvuvi kufuatana na Sheria ya Uvuvi Na. 22 ya mwaka 2003 na Kanuni  za Uvuvi  za mwaka 2009 na kuzingatia miongozo mbalimbali;
3.     Kikundi kiwe na Akaunti ya Benki;
4.     Mradi wowote wa uvuvi utakaowasilishwa na kikundi  lazima ukidhi matakwa ya Sheria ya
 Uvuvi Na. 22 ya mwaka 2003 na Kanuni  za Uvuvi za mwaka 2009 na sheria nyingine
za nchi ikiwemo ya Mazingira ya mwaka 2004;
5.     Miradi itakaofadhiliwa ni pamoja na ununuzi wa boti za uvuvi, injini za kupachika, nyavu za dagaa na nyavu za samaki wakubwa ndoana (long line);
6.     Kikundi kithibitishe  kuwa kina uwezo  na kipo tayari  kuchangia asilimia arobaini (40%) ya gharama ya mradi unaoombwa. Serikali itachangia asilimia sitini (60%) ya gharama za zitakazonunuliwa;
7.     Maombi yapitishwe kwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Serikali za Mitaa husika kwa ajili ya kupitia maombi hayo na kuona kama yanakidhi vigezo vilivyowekwa na baada ya hapo kuwasilishwa Wizarani;
8.     Maombi yaambatane na mchanganuo wa gharama za mradi;

Kwa tangazo hili, vikundi husika vinashauriwa kujiandaa kwa ajili ya kutumia fursa hii kwa
kushirikiana na Halmashauri zao. Aidha, Halmashauri zinashauriwa kufuatilia na kuwandaa
walengwa ili hatimaye vipatikane vikundi vyenye sifa ya kupewa ruzuku.

Tangazo limetolewa na:-
Katibu Mkuu,
Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi,
Sanduku La Posta 9152,
DAR ES SALAAM.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni