Nav bar

Ijumaa, 2 Novemba 2018

KATIBU MKUU ATEMBELEA SOKO LA SAMAKI FERRY KUKAGUA UJENZI WA VYOO:



Leo Katibu Mkuu wa Uvuvi Dkt. Rashid Tamatama alikwenda kuangalia utekelezaji wa ujenzi wa vyoo 24 hiyo ikiwa ni katika hatua za utekelezaji wa ahadi za Mh. Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh. Luhaga Mpina alipotembelea sokoni hapo na kubaini mapungu yaliyopo ikiwemo.

1. Uchakavu wa majengo
2. Upungufu wa vyoo;
3. Kujaa kwa mchanga katika bahari: na
4. Uchakavuwa jokofu la kuhifadhia samaki

Ambapo alisema kuwa Wizara yake itaingilia kwa kuchukua hatua za haraka katika hayo na kuagiza mara moja kwa ujenzi wa vyoo 24 ambavyo vitapunguza msongamano sokoni hapo.

Katibu Mkuu wa Uvuvi, Dkt. Rashidi Tamatamah ametembelea soko la samaki Ferri- Kivukoni kuangalia ujenzi wa vyoo 24 ambavyo vitapunguza msongamano katika soko hilo.

Katibu Mkuu Uvuvi, akielekea eneo la ujenzi akiambatana na Meneja wa soko  Bw. Mkuu Anje

Katibu Mkuu Uvuvi akiwa katika eneo la Ferry 
Katibu Mkuu akiwa na Meneja wa soko hilo akifafanua jambo sokoni hapo


Choo ambacho kinatumika kwa sasa na kutokana na wingi wa watu hakikidhi maitaji yao

Katibu Mkuu akipata maelezo juu ya ujenzi huo unavyoendelea


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni