Nav bar

Jumatano, 7 Novemba 2018

NEW ZEALAND KUWEKEZA KATIKA SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI




Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb), amekutana na Balozi wa New Zealand Nchini Tanzania Mike Burrell Ofisini kwake leo tarehe 06/11/2018 jijini Dodoma.

Tumekuwa tukishirikiana vyema kati ya Nchi ya Tanzania na New Zealand katika kupata madume bora ya Ng’ombe 6 kule kituo cha Taifa cha Uhimilishaji (NAIC) kilichopo UsaRiver jijini Arusha ambayo yamechangia uzalishaji wa mbegu bora kuongezeka zaidi, alisema Mh. Ulega.

Mh.Ulega alisema tutasaidiana katika upande wa ufugaji wa samaki, ambapo wenzetu wako mbele
zaidi katika masuala ya Ukuzaji viumbe kwenye maji.
“ Our President Dkt. John P. Magufuli is trying so hard to ensure that, our environment in Tanzania is
getting better and better”. Say’s Ulega.

Vilevile Mhe. Ulega alisema kunahitajika watu wa kwenda kusoma katika kada ya Sayansi ambapo kwa sasa bado tunapeleka watu wachache katika fani hiyo.

Kwa upande wake balozi Mike alisema, tunahitaji Ushirikiano na Tanzana katika kuwekeza kwenye
Sekta ya Mifugo na Uvuvi.
“We assure to share information and cooperate with you because the country has a huge potential”.
Say’s Hon. Mike.

Tunahitaji wanasayansi kutoka Tanzania wenye elimu ya juu hasa waliobobea katika masuala ya
Sayansi, “ We love to have Scholars in New Zealand from your country, alisema Hon. Mike.

 We encourage people to come and learn more about aquaculture,say’s Hon. Mike.

Naye Katibu Mkuu Mifugo Prof.Elisante Ole Gabriel alisema, NARCO wanahitaji kunufaika na kupata Wataalamu kutoka New Zealand kuhusina na Mifugo katika Uzalishaji.


Naibu Waziri Mhe. Ulega akiongea jambo na Balozi wa New Zealand Nchini Tanzania Mhe. Mike Burrell

Balozi Mike akisalimiana na Wakurugenzi




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni