Nav bar

Jumatatu, 26 Januari 2026

SEMINA YA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI YAKAMILIKA

 Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Taasisi zilizopo chini yake imehitimisha Semina ya Mafunzo Elekezi iliyotolewa kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo kuhusu shughuli zinazo ratibiwa na kusimamiwa na Wizara hiyo.

Akizungumza kwenye tamati ya semina, Mwenyekiti  wa Kamati hiyo Mhe. Deudatus Mwanyika aliwapongeza viongozi pamoja na wataalam wa wizara hiyo kwa uwasilishaji mzuri wa semina hiyo ya siku 2 iliyoanza Januari 19, 2026 na kuhitimishwa leo Januari 20, 2026 Bungeni Jijini Dodoma.

Aidha Mhe. Mwanyika amesisitiza wizara kuendelea kuboresha matumizi ya teknolojia za kisasa za kitafiti pamoja na mafunzo yanayoendana na teknolojia hiyo kwa watumishi na wataalamu wa sekta zote ili kuongeza thamani ya mazao ya mifugo na uvuvi.

Akitolea ufafanuzi wa baadhi ya hoja zilizoibuliwa na wajumbe wa kamati hiyo, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amesema Wizara yake inaendelea kuimarisha na kuboresha huduma zinazotolewa na sekta hizo na kuahidi ushirikiano wa dhati na kamati hiyo. 

Aidha aliongeza kuwa yapo mabadiliko mengi yanayoendelea kwenye sekta hiyo yanayolenga kutatua changamoto za wananchi pamoja na wadau wa sekta hiyo ya mifugo na uvuvi.

Semina hiyo ililenga kuliongezea Bunge uelewa kuhusu sekta ya Mifugo na Uvuvi na mabadiliko yanayotarajiwa katika sekta hiyo.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa akizungumza wakati wa semina ya kuipitisha  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo kwenye majukumu na Maendeleo ya Sekta ya Mifugo na Uvuvi iliyokamilika leo Januari 20,2026 Bungeni jijini Dodoma.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo Mhe. Deodatus Mwanyika akitoa maelekezo kwa Viongozi na watendaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi mara baada ya kamati yake kupitishwa kwenye majukumu na maendeleo ya Sekta ya Mifugo na Uvuvi Januari 20, 2026 Bungeni jijini Dodoma.

Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo wakitoa maoni na ushauri mara baada ya kupokea Semina elekezi ya kujengewa uelewa kuhusu shughuli zinazo Simamiwa na Kuratibiwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi iliyokamilika leo Januari 20, 2025 Bungeni jijini Dodoma.

Sehemu ya Watendaji Wakuu wa Taasisi na Wakurugenzi wa Idara mbalimbali kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakiwa kwenye semina elekezi ya kuipitisha kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo kwenye majukumu na Maendeleo ya Sekta ya Mifugo na Uvuvi iliyokamilika leo Januari 20,2026 Bungeni jijini Dodoma.

Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Maabara ya Veterinari nchini (TVLA) Dkt. Stella Bitanyi akiwasilisha taarifa kwa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo kuhusu shughuli zinazosimamiwa na taasisi hiyo wakati wa mafunzo ya Semina elekezi ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi iliyokamilika leo January 20, 2025, Bungeni jijini Dodoma.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni