Nav bar

Jumamosi, 10 Januari 2026

MHE. KAMANI AHITIMISHA MAFUNZO KWA WAJASIRIAMALI 350 WA SEKTA YA UVUVI

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng'wasi Kamani amewataka wajasiriamali 350 wa sekta ya uvuvi waliopata mafunzo ya kuongeza thamani ya mazao ya uvuvi kutumia ujuzi walioupata kwa ajili ya kuongeza ajira, Kipato na kuchagia Maendeleo ya Taifa.

Akizungumza wakati wa kufunga Mafunzo hayo Leo Januari 9, 2026 katika Ukumbi wa Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) Kampasi ya Nyegezi Mhe. Kamani amesema serikali inaendelea kuunga Mkono wajasiriamali wanaojihusisha na uongezaji wa thamani ya mazao ya uvuvi ili kupanua biashara zao.

"Mafunzo hayo yanaakisi dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwawezesha wananchi kiuchumi, hususan wanawake na vijana, kupitia fursa za Uchumi wa Buluu, leo mnapopewa vyeti mnakabidhiwa dhima ya kwenda kutumia ujuzi wenu kuongeza ajira, kipato na maendeleo ya Taifa” alisema Mhe. Kamani.

Aidha, aliongeza kuwa serikali imetenga kiasi cha shilingi Bilioni moja kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi ili kuongeza ufanisi unaolenga kutoa mafunzo bora ya kukuza sekta ya uvuvi na uchumi wa buluu

Kwa Upande wake, Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) Dkt. Semvua Mzighani amesema mafunzo hayo yaliyofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Ubelgiji la ENABEL kupitia mradi wa Green and Smart Cities (IncluCities) yamelenga kuongeza thamani ya mazao ya uvuvi, ushindani wa bidhaa sokoni na kuongeza kipato cha kaya.

 Awali wawakilishi wa Kundi la Vijana na Kina Mama Wajasiriliamali wakiwasilisha risala yao kwa mgeni rasmi walieleza kuwa mafunzo hayo yataenda kubadilisha mfumo mzima wa uchakataji na uongezaji wa thamani wa mazao ya Uvuvi tofauti na hapo awali walipokuwa wakitumia njia za jadi.

Jumla ya kina mama wajasiriamali 200 wamehitimu mafunzo ya usindikaji wa mazao ya samaki, huku vijana 150 wakipata mafunzo ya utayari kazini katika ukuzaji viumbe maji.

Naibu waziri wa Mifugo Na Uvuvi Mhe. Ng'wasi Kamani( Wa pili, kulia) akitunuku cheti kwa Bi. Joyce Christopher akiwa ni mmoja kati ya washiriki 350 waliohitimu mafunzo ya muda mfupi juu ya ufugaji samaki na ukuzaji viumbe maji FETA Nyegezi wakati wa kuhitimisha mafunzo hayo leo Januari 9, 2026.

Naibu waziri wa Mifugo Na Uvuvi Mhe. Ng'wasi Kamani( Wa kwanza, kulia) akikagua mazao ya uvuvi yalioongezewa thamani na Kina Mama wajasiriamali waliopata mafunzo ya muda mfupi juu ya ufugaji samaki na ukuzaji viumbe maji FETA Nyegezi leo Januari 9, 2026.

Mtendaji Mkuu wa  Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) Dkt. Semvua Mzighani akizungumza wakati wa hafla ya kutunuku vyeti vijana na  kina Mama Wajasiriamali  350 walioshiriki mafunzo ya muda mfupi ya ufugaji samaki na ukuzaji viumbe maji FETA Nyegezi Leo Januari 9, 2026.

Mwakilishi wa Katibu Mkuu, ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Ukuzaji Viumbe Maji Dkt. Nazael Madalla akielezea hali ya sekta ya Uvuvi nchini wakati wa kufunga mafunzo ya muda mfupi juu ya ufugaji samaki na ukuzaji viumbe maji FETA Nyegezi leo Januari 9, 2026.

Naibu waziri wa Mifugo Na Uvuvi Mhe. Ng'wasi Kamani (kati kati, waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja  na washiriki 350 waliohitimu mafunzo ya muda mfupi juu ya ufugaji samaki na ukuzaji viumbe maji FETA Nyegezi wakati wa hafla ya kuhitimisha mafunzo hayo leo Januari 9, 2026.

Naibu waziri wa Mifugo Na Uvuvi Mhe. Ng'wasi Kamani akizungumza na washiriki 350 waliohitimu mafunzo ya muda mfupi juu ya ufugaji samaki na ukuzaji viumbe maji FETA Nyegezi wakati wa hafla ya kuhitimisha mafunzo hayo leo Januari 9, 2026.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni