◼️Taa za umeme wa jua zawekwa kiporo
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imepiga marufuku matumizi ya nyavu za uvuvi zilizolalamikiwa na Wavuvi kuwa zinachangia kuongezeka kwa Uvuvi haramu.
Marufuku hiyo imetolewa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa wakati wa mkutano wake na wadau mbalimbali wa Uvuvi uliofanyika jijini Mwanza Desemba 24,2025.
“Kwa hiyo ninaelekezea haya mawili moja la Taa naomba zifanyiwe utafiti ndani ya wiki 2 kwa sababu tafiti zipo ni kuzichambua tu kisha ntalitoea maelekezo lakini hili la nyavu haramu za dagaa halina masihara wala msalimie mtume,tutafute nyavu ambazo zinaweza kuturuhusu tuvue uvuvi endelevu na tubaki kazini na nchi yetu ibaki salama” Amesema Balozi Dkt. Bashiru.
Aidha Balozi Dkt. Bashiru ameongeza kuwa kufuatia marufuku hiyo Serikali itaweka vyombo vyake kwenye mipaka yote ili kuzuia nyavu hizo zisiingie nchini.
Awali wakizungumza wakati wa Mkutano huo, baadhi ya Wavuvi walimueleza Balozi Dkt. Bashiru kuwa nyavu hizo za dagaa zimekuwa zikivua mpaka mazalia ya samaki aina ya sangara kwa kiwango kikubwa huku pia wakimlalamikia matumizi ya taa zinazotumia umeme wa jua kuwa mwanga wake ni mkali na unavuta hata samaki wasiotakiwa kuvuliwa.
Kabla ya kuelekea kwenye mkutano huo Balozi Dkt. Bashiru alishiriki kupandikiza samaki katika eneo la Shadi lililopo Wilaya ya Nyamagana mkoani humo ambapo aliwaeleza wakazi wa eneo hilo kuwa Serikali itapeleka vizimba vya kufugia samaki katika eneo hilo ili kuendelea kulinda samaki wa asili waliopo hapo.




Hakuna maoni:
Chapisha Maoni