Nav bar

Alhamisi, 4 Desemba 2025

SERIKALI, WADAU YAANZA KUPITIA MPANGO MKAKATI KUTOKOMEZA UGONJWA WA SOTOKA YA MBUZI NA KONDOO

Serikali ya kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya mifugo imeanza kufanya mapitio ya kutokomeza ugonjwa Sotoka (Peste des Petits Ruminants (PPR) ifikapo mwaka 2030,  hatua itakayoiweka Tanzania katika mstari wa mbele barani Afrika katika mapambano dhidi ya ugonjwa huu unaodhuru mifugo.

Akifungua warsha ya Kitaifa ya Tathmini na Mapitio ya Mkakati wa Kitaifa wa Kupambana na PPR iliyofanyika leo Desemba Mosi, 2025 katika Hoteli ya Peacok jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,  Bi.Agnes Meena amesema Sekta  ya mifugo imekuwa nguzo muhimu ya uchumi wa Tanzania, ikichangia asilimia 6.2 ya Pato la Taifa na kusaidia zaidi ya kaya milioni tano lakini imekuwa ikikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo magonjwa yanayosababisha vifo vya mifugo. 

“Kondoo na mbuzi wanakabiliwa na changamoto ya PPR inayosababisha vifo vingi, hasara za kiuchumi na kukwamisha upatikanaji wa masoko ya kikanda na kimataifa.”

Bi. Meena aliongeza kuwa serikali imetenga zaidi ya shilingi bilioni 200 kwa miaka mitano ijayo ili kuimarisha chanjo, utambuzi na mifumo ya ufuatiliaji wa mifugo, hivyo dhamira ya serikali kutokomeza magonjwa ya mifugo ikiwemo  PPR itafanikiwa.

Hapo awali,  Mwakilishi wa  Shirika la Rasilimali za Mifugo la Umoja wa Africa (AU-IBAR) Dkt. Folorunso Fasina, alibainisha nafasi muhimu ya Tanzania  kutokomeza ugonjwa wa Sotoka ya mbuzi na kondoo kwani ugonjwa huo umeendelea kusababisha hasara ya hadi dola bilioni 2.4 kila mwaka kwa bara la Africa  hivyo kampeni ya kutokomeza PPR ifikapo 2030.

Naye, Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo, Dkt. Benezeth Lutege, alisema warsha hiyo ni tukio la kihistoria kwa sekta ya mifugo nchini Tanzania ikiwa ni sehemu muhimu ya kutokomeza ugonjwa wa Sotoka ya mbuzi na Kondoo kwani unaathiri afya ya mifugo na kukwamisha biashara.

Mwakilishi wa Shirima la Chakula na Kilimo la umoja wa Mataifa (FAO) nchini  Tanzania,  Dkt. Justine Assenga ameipongeza Tanzania kwa hatua muhimu ya kuanisha mkakati wa kitaifa wa kutokomeza ugonjwa wa Sotoka ya mbuzi na Kondoo.

Katibu Mkuu Wizara ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi.Agnes Meena akifungua warsha ya kupitia na kuhakiki mkakati wa kitaifa wa kutokomeza ugonjwa wa sotoka ya mbuzi na kondoo ifikapo 2030, warsha inayofanyika Hoteli ya Peacok jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 1 hadi 2 Desemba  2025.

Mwakilishi wa Shirika la Rasilimali za Mifugo la Umoja wa Africa (AU - IBAR) Dkt. Folorunso Fasina akizungumza kwenye warsha ya kupitia na kuhakiki mkakati wa kitaifa wa kutokomeza ugonjwa wa sotoka ya mbuzi na kondoo ifikapo 2030, warsha inayofanyika Hoteli ya Peacok jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 1 hadi 2 Desemba  2025.

Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo Dkt. Benezeth Lutege akielezea umuhimu wa Mkakati wa Kitaifa wa Kutokomeza Ugonjwa wa Sotoka ya mbuzi na kondoo ifikapo 2030 wakati wa warsha inayofanyika Hoteli ya Peacok jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 1 hadi 2 Desemba  2025.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agnes Meena (Katikati, waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau wa sekta ya mifugo wakati wa warsha ya kupitia na kuhakiki  Mkakati wa Kitaifa wa Kutokomeza Ugonjwa wa Sotoka ya mbuzi na kondoo ifikapo 2030 iliyofanyika Hoteli ya Peacok jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 1 hadi 2 Desemba  2025.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni