Nav bar

Jumatatu, 25 Agosti 2025

WADAU WATAKIWA KUSHIRIKIANA KUDHIBITI UVUVI HARAMU ZIWA VICTORIA

Na Hamisi Hussein - Mwanza.

Serikali Kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imesema ulinzi wa rasilimali za uvuvi katika ukanda wa Ziwa Victoria ni suala linalohitaji ushirikiano wa pamoja baina yake na wadau wote wanaohusika kwenye mnyororo wa thamani wa  sekta ya uvuvi.

Akizungumza wakati wa Kufungua Kikao cha kujadili mikakati ya kudhibiti uvuvi haramu na biashara haramu ya mazao ya uvuvi kwa ukanda wa Ziwa Victoria  kilichofanyika Ukumbi wa Nyakahoja  jijini Mwanza Agosti 22, 2025 Naibu  Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Edwin Mhede alisema wadau wa sekta ya uvuvi kwa kushirikiana  na serikali kuhakikisha uvuvi haramu unadhibitiwa kwa kuja na mikakati ya pamoja ikiwemo elimu.

“Ni lazima tuungane na kuwa na mikakati ya pamoja kupiga vita vitendo hivi. Sio jukumu la Serikali Kuu pekee; ni wajibu wa kila mdau wa sekta hii wakiwemo wavuvi, wachakataji, wasafirishaji, wamiliki wa viwanda vya zana  za uvuvi, wauzaji na wasambazaji wa zana za uvuvi pamoja na Serikali za mitaa. Ni ukweli usiopingika kuwa samaki hawa wakitoweka, hakuna hata mmoja atakayesalia katika biashara ya samaki na mazao ya uvuvi” alisema Dkt. Mhede Aliwahimiza.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Uvuvi Tanzania Prof. Mohammed Sheikh amesema Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeanza matumizi ya teknolojia za kulinda rasilimali za Uvuvi ikiwemo mitambo ya  kuhifadhi mazao ya uvuvi.

"Kipindi cha masika asilimia 40 ya mazao ya uvuvi hupotea, kwa sasa tumeanza kuja na mitambo ya kisasa ya kuhifadhi mazao ya Uvuvi yasipotee, pia boti za uvuvi tutaziwekea vifuatilizi kwa ajili ya usalama wa maisha ya wavuvi na rasilimali zake", Alisema Prof. Sheikh.

Kwa upande  wake Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Bw. Peter Kasele alisema mkoa huo unashirikiana na wataalamu wa Wizara kwa kufanya doria pamoja na kutoa elimu .

Baadhi wa wadau wa sekta ya Uvuvi wakiwemo wavuvi, wachakataji, wasafirishaji, wamiliki viwanda vya zana za uvuvi wamesema udhibiti wa uvuvi haramu utafanikiwa iwapo serikali itasimamia sheria za uvuvi pamoja ulimishaji kufanyika kwa njia ya vyombo vya habari ambapo elimu hiyo ianishe jinsi uvuvi haramu utakavyowaathiri  serikali iendelee ujadili mikakati ya pamoja ya kudhibiti uvuvi haramu na biashara haramu ya uvuvi katika ukanda wa Ziwa Victoria .

Aidha kwa Mwaka 2024/2025 jumla ya tani 528,750.09 zenye thamani ya Shilingi Trilioni 3.42 za mazao y Uvuvi zilivunwa kati ya hizo, tani 486,789.21 zenye thamani ya Shilingi trilioni 3.41 zilivunwa kutoka kwenye Maji ya asili na tani 43, 497.95 zenye thamani ya shilingi bilioni 12.25 zilitokana na ukuzaji viumbe maji.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Edwin Mhede akifungua Kikao cha wadau wa sekta ya uvuvi cha kujadili mikakati ya pamoja ya kudhibiti uvuvi haramu ukanda wa ziwa victoria kilichofanyika Ukumbi wa Nyakahoja, Jijini Mwanza Agosti 22, 2025.

Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Bw. Peter Kasele akieleza jinsi mkoa huo unavyoshirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kufanya doria na kutoa elimu kwa wavuvi ili kukabiliana na uvuvi haramu wakati wa kikao cha wadau wa sekta ya uvuvi cha kujadili mikakati ya pamoja ya kudhibiti uvuvi haramu ukanda wa ziwa victoria kilichofanyika Ukumbi wa Nyakahoja, Jijini Mwanza  Agosti 22, 2025.

Mkurugenzi wa Uvuvi Nchini Prof. Mohammed Sheikh akielezea hali ya uzalishaji wa mazao ya uvuvi na jitihada za Wizara ya Mifugo na Uvuvi kudhibiti uvuvi haramu wakati wa kikao cha wadau wa sekta ya uvuvi cha kujadili mikakati ya pamoja ya kudhibiti uvuvi haramu ukanda wa ziwa victoria kilichofanyika Ukumbi wa Nyakahoja, Jijini Mwanza Agosti 22, 2025.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Edwin Mhede (KatiKati, waliokaa) akiwa katika Picha ya Pamoja na Wadau wa sekta ya Uvuvi mara baada ya kumalizika kwa kikao cha wadau wa sekta ya uvuvi cha kujadili mikakati ya pamoja ya kudhibiti uvuvi haramu ukanda wa ziwa victoria kilichofanyika Ukumbi wa Nyakahoja, Jijini Mwanza Agosti 22, 2025.






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni