Nav bar

Jumatatu, 25 Agosti 2025

BI. KABYEMERA AWATAKA WANAMICHEZO KUINGIA KAMBINI KABLA YA KWENDA SHIMIWI

Na. Stanley Brayton, WMUV

Dodoma 

Agosti 23, 2025

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Bi. Lucy Kabyemera, amewataka wanamichezo wa Wizara wanaoshiriki Michezo ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali Tanzania (SHIMIWI) kuweka kambi mapema ili kuweza kujiandaa vizuri katika michuano hiyo ya SHIMIWI ili kuweza kuleta makombe na Mataji na kuongeza sifa ya Wizara.

Amezungumza hayo leo Agosti 23, 2025, kwenye Uwanja wa Kilimani Mkoani Dodoma, wakati wa BONANZA la kujiandaa na Michuano ya SHIMIWI.

Aidha, Bi.Kabyemera amewataka wanamichezo wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na wanamichezo wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kudumisha Umoja na ushikamano katika kuhakikisha mazoezi yanafanyika vizuri na kwa uweledi ili kuibuka vinara katika michuano hiyo.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Bi. Lucy Kabyemera, akizungumza na kuwapa nasaha wanamichezo wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na wanamichezo wa Wizara ya Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kabla ya kufanya Ufunguzi wa Bonanza la kujiandaa na Michezo ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali Tanzania (SHIMIWI), yaliyofanyika katika Viwanja vya Kilimani, Agosti 23, 2025 Dodoma.

Wanamichezo wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na wanamichezo wa Wizara ya Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Bi. Lucy Kabyemera, kabla ya kufanya Ufunguzi wa Bonanza la kujiandaa na Michezo ya, yaliyofanyika katika Viwanja vya Kilimani, Agosti 23, 2025 Dodoma.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni