Na. Stanley Brayton, WMUV
Dodoma
Agosti 23, 2025
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Bi. Lucy Kabyemera, amewataka wanamichezo wa Wizara wanaoshiriki Michezo ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali Tanzania (SHIMIWI) kuweka kambi mapema ili kuweza kujiandaa vizuri katika michuano hiyo ya SHIMIWI ili kuweza kuleta makombe na Mataji na kuongeza sifa ya Wizara.
Amezungumza hayo leo Agosti 23, 2025, kwenye Uwanja wa Kilimani Mkoani Dodoma, wakati wa BONANZA la kujiandaa na Michuano ya SHIMIWI.
Aidha, Bi.Kabyemera amewataka wanamichezo wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na wanamichezo wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kudumisha Umoja na ushikamano katika kuhakikisha mazoezi yanafanyika vizuri na kwa uweledi ili kuibuka vinara katika michuano hiyo.


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni