Nav bar

Jumatatu, 25 Agosti 2025

MIFUGO NA UVUVI YAIONESHA UBABE ARDHI

Na. Stanley Brayton, WMUV

Dodoma 

Agosti 20, 2025

⬛  Yaipiga Ardhi kipigo cha goli 3-1 bila huruma 

⬛ Kamba Wanaume yawatoa povu Ardhi, yashinda mivuto yote miwili, huku wanawake washinda kwa mvuto moja 

⬛  Mpira wa Pete wanawake washinda kwa goli 16-7


Wizara ya Mifugo na Uvuvi yaibuka kidedea Maandalizi ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali Tanzania (SHIMIWI) kwa kuipiga Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi goli 3-1, mechi ambayo imechezwa katika Viwanja vya Kilimani, leo Agosti 23, 2025.

Ambapo magoli ya upande wa Mifugo na Uvuvi yalifungwa na wachezaji Hema Mugenyo (1), Joseph Onesmo (2) kwa kipindi cha kwanza, na kwa upande wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kipindi cha kwanza goli lilifungwa na mchezaji Cleophace Simon.

Aidha, Mifugo na Uvuvi imeibuka kidedea mbele ya Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kwa Wanaume kushinda mivutano yote miwili na wanawake kushinda kwa mvuto mmoja huku mvuto mmoja watoshana nguvu.

Vilevile, kwa upande wa Mpira wa Pete, wanawake Wizara ya Mifugo na Uvuvi yaishinda Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi goli 16-7.

Picha ni wachezaji wa Kamba wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi  kwa upande wa Wanawake wakiwa kwenye mstari kabla ya kusalimiana na Mgeni Rasmi, wakati wa BONANZA la Maandalizi ya SHIMIWI, yaliofanyika katika Viwanja vya Kilimani, Agosti 23, 2025 Dodoma.

Picha ni wachezaji wa Kamba wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa upande wa Wanaume wakiwa tayari kwa ajili ya kuvuta kamba, wakati wa BONANZA la Maandalizi ya SHIMIWI, yaliofanyika katika Viwanja vya Kilimani, Agosti 23, 2025 Dodoma.

Picha ni wachezaji wa mpira wa miguu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakiwa kwenye picha ya pamoja kabla ya kuanza mechi dhidi ya Wizara ya Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, wakati wa BONANZA la Maandalizi ya SHIMIWI, yaliofanyika katika Viwanja vya Kilimani, Agosti 23, 2025 Dodoma.

Picha ni wachezaji wa Mpira wa Pete Wizara ya Mifugo na Uvuvi upande wa wanawake wakiwa kwenye mchuano dhidi ya Wizara ya Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, wakati wa BONANZA la Maandalizi ya SHIMIWI, yaliofanyika katika Viwanja vya Kilimani, Agosti 23, 2025 Dodoma.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni