Na. Stanley Brayton, WMUV
Dodoma
Agosti 20, 2025
⬛ Yaipiga Ardhi kipigo cha goli 3-1 bila huruma
⬛ Kamba Wanaume yawatoa povu Ardhi, yashinda mivuto yote miwili, huku wanawake washinda kwa mvuto moja
⬛ Mpira wa Pete wanawake washinda kwa goli 16-7
Wizara ya Mifugo na Uvuvi yaibuka kidedea Maandalizi ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali Tanzania (SHIMIWI) kwa kuipiga Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi goli 3-1, mechi ambayo imechezwa katika Viwanja vya Kilimani, leo Agosti 23, 2025.
Ambapo magoli ya upande wa Mifugo na Uvuvi yalifungwa na wachezaji Hema Mugenyo (1), Joseph Onesmo (2) kwa kipindi cha kwanza, na kwa upande wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kipindi cha kwanza goli lilifungwa na mchezaji Cleophace Simon.
Aidha, Mifugo na Uvuvi imeibuka kidedea mbele ya Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kwa Wanaume kushinda mivutano yote miwili na wanawake kushinda kwa mvuto mmoja huku mvuto mmoja watoshana nguvu.
Vilevile, kwa upande wa Mpira wa Pete, wanawake Wizara ya Mifugo na Uvuvi yaishinda Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi goli 16-7.




Hakuna maoni:
Chapisha Maoni