Nav bar

Jumanne, 22 Aprili 2025

SERIKALI KUENDELEA KUWEZESHA UFUGAJI WA KISASA

Na Hamisi Hussein - WMUV, Mwanza.

⬛️ Mhe. Mnyeti akikabidhi Mitamba 10 ya Maziwa kwa UWAMATA

Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi itaendelea kuwezesha ufugaji wa kisasa ili kuongeza tija katika uzalishaji na kukuza uchumi wa wafugaji nchini.

Hayo yameelezwa leo Aprili 19, 2025 na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alaxender Mnyeti wakati wa kukabidhi ng'ombe 10 wa Maziwa kwa kikundi cha Umoja wa Mapadri Tanzania (UWAMATA) hafla iliyofanyika katika Shamba la Uzalishaji Mifugo lililopo Misungwi mkoani Mwanza.

Mhe. Mnyeti amesema lengo la serikali nikuona inawezesha ufugaji wa kisasa kwa kuhimiza wafugaji kuwa na mifugo michache yenye tija itakayotoa mazao bora yanayokidhi  ushindani wa masoko.

" Mhe. Rais wetu anataka kuona ufugaji wa Kisasa unakuwa na tija kwa wafugaji na sisi Wizara tunaendelea kuhimiza ufugaji wa kisasa ambapo tumekuwa tukihamasisha ulimaji wa malisho ambayo yametajwa na wataalam wetu kuwa yanaprotini nyingi" alisema Mhe. Mnyeti.

Kuhusu ng'ombe wa maziwa (Mitamba) waliotolewa na serikali kwa Kikundi cha Umoja wa Mapadri Tanzania  (UWAMATA) Mhe. Naibu Waziri Mnyeti amesema zoezi la upandikizaji wa ng'ombe hao limefanywa na Wataalam wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ili kuwa na uhakika wa uzalishaji wa ng'ombe hao.

Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa Mapadri Tanzania (UWAMATA) Padri George Nzungu ameishukuru serikali kwa kuwapatia ng'ombe hao kwani wataleta tija ya uzalishaji wa maziwa na kuahidi kuwa balozi wa ufugaji wa kisasa kwa wananchi wanaozunguka eneo lao.

Aidha Mkurugenzi Msaidi wa Idara ya Uzalishaji na Masoko Dkt . Yeremia Sanka amesema ng'ombe hao waliopatikana kutokana na upandikizaji wa mbegu za madume halisi ya maziwa (Friesian) na majike ya kienyeji aina ya Boran na  watazalisha kati ya lita 8  hadi 12 kwa siku tofauti na ng'ombe wa asili ambaye anatoa maziwa lita 1.5 hadi 3 tu kwa siku.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti (Mwenye Fimbo) akiwa Kwenye Picha ya Pamoja  na Mapadri wakati wa Makabidhiano ya Majike 10 ya maziwa kwenye Shamba la uzalishaji Mifugo Mabuki, Mwanza Aprili 19, 2025.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti  akizungumza na Mapadri waliopo kwenye Umoja wa Mapadri Tanzania (UWAMATA) wakati wa makabidhiano ya Majike 10  ya maziwa yenye mimba kwenye Shamba la uzalishaji Mifugo Mabuki, Mwanza Aprili 19, 2025.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti (Kulia) akimkabidhi Mwongozo wa ufugaji wa ng'ombe wa Maziwa Padri Samweli Massawe(Katikati) wakati wa Makabidhiano ya Majike 10 ya maziwa kwenye Shamba la uzalishaji Mifugo Mabuki, Mwanza Aprili 19, 2025.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti (Kulia) akimkabidhi Boski la Dawa ya kuongeshea ng'ombe wa Maziwa Padri Samweli Massawe wakati wa Makabidhiano ya Majike 10 ya maziwa kwenye Shamba la uzalishaji Mifugo Mabuki, Mwanza Aprili 19, 2025.

Mitamba ya Maziwa ilitokana na madume halisi ya maziwa (Friesian) na Majike ya asili aina ya Boran ikichunga katika Shamba la Mifugo Mabuki kabla la hafla ya makabidhiano baina ya Naibu Waziri  wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti  na Umoja wa Mapadri Tanzania UWAMATA hafla iliyofanyika Shamba la uzalishaji Mifugo Mabuki lililopo Misungwi, Mwanza Aprili 19, 2025.



 




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni