Nav bar

Jumanne, 18 Agosti 2020

HABARI PICHA ZA MAONYESHO YA NANENANE KWENYE MIKOA YA MOROGORO, LINDI, ARUSHA, DODOMA, SIMIYU, MBEYA TAREHE 05/08/2020

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mkoani Dar es Salaam Mhe. Godwin Gondwe (Kushoto) wakikagua bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa kwa kutumia (ukili/ukindu) mara baada ya kutembelea banda la Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani kwenye Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki yanayofanyika katika Viwanja vya Nanenane Mkoani Morogoro. (05.08.2020) 

 


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega akishuhudia chanjo sita za mifugo zinazozalishwa hapa nchini chini ya Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) inayosimamiwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, wakati alipotembelea Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki inayojumuisha mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Pwani na Morogoro, yanayofanyika katika Viwanja vya Nanenane Mkoani Morogoro. Pembeni yake ni Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mkoani Dar es Salaam Mhe. Godwin Gondwe. (05.08.2020) 



Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Wa pili kutoka kulia) akiwa na mwenyeji wake katika Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mkoani Dar es Salaam Mhe. Godwin Gondwe (Wa kwanza kutoka kulia) wakati wakikagua bidhaa mbalimbali zinazozalishwa hapa nchini zinatokana na mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi baada ya Naibu Waziri Ulega kufika katika Viwanja vya Nanenane Mkoani Morogoro kujionea maonesho hayo. (05.08.2020) 


 

Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mkoani Dar es Salaam Mhe. Godwin Gondwe akifurahia kumshika samaki aina ya kambakochi baada ya Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega kumtaarifu namna samaki huyo alivyo na thamani kubwa katika masoko ya kimataifa wakati walipotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki inayojumuisha mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Pwani na Morogoro, yanayofanyika katika Viwanja vya Nanenane Mkoani Morogoro. (05.08.2020) 


LINDI


Mkuu wa Wilaya ya Masasi, Mhe. Selemani Mzee (aliyevaa suti nyeusi) akisaini kitabu cha wageni wakati alipotembelea mabanda ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kusini katika viwanja vya Ngongo - Manispaa ya Lindi. Kulia ni Mtafiti Mkuu wa Mifugo kutoka TALIRI Naliendele, Abel Mtambuki. (05.08.2020) 

 


Mkuu wa Wilaya ya Masasi, Mhe. Selemeni Mzee akiangalia viatu vya ngozi kwa mmoja wa wajasiriamali kutoka Lungwana Shoe Products, Amedeus Thadeus (aliyevaa tisheti nyekundu) wakati alipotembelea mabanda ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kusini katika viwanja vya Ngongo - Manispaa ya Lindi. (05.08.2020) 

 


Afisa Uvuvi Kituo cha Ukuzaji Viumbe Maji Kanda ya Kusini Lindi, Hassan Mchwapi akitoa maelezo kwa Mkuu wa Wilaya ya Masasi, Mhe. Selemani Mzee wakati alipotembelea mabanda ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kusini katika viwanja vya Ngongo - Manispaa ya Lindi. (05.08.2020) 

 

DODOMA


Mgeni rasmi, Kaimu Mkuu wa Mkoa, Dodoma, Mhe. Mwanahamisi Munkunda(kulia) akijadiliana jambo kuhusu bidhaa ya dagaa na Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi(Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel alipotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni, Mkoani Dodoma Agosti 5, 2020. 

 


Mgeni rasmi, Kaimu Mkuu wa Mkoa, Dodoma, Mhe. Mwanahamisi Munkunda (katikati) akiongea na Mkurugenzi wa Kampuni ya Kilimo, Mifugo na Ufugaji Tanzania (TALAS), Felix Filangali (kulia) alipotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni, Dodoma Agosti 5, 2020. Kushoto ni Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Profesa Elisante Ole Gabriel. 

 


Mgeni rasmi, Kaimu Mkuu wa Mkoa, Dodoma, Mhe. Mwanahamisi Munkunda (wa pili kushoto) akiwa ameshika kiatu, moja ya bidhaa inayotengenezwa na Kampuni ya Simons, alipotembelea banda la Mifugo na Uvuvi katika Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Nzuguni, Dodoma Agosti 5, 2020. Wa kwanza kushoto ni Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi(Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel. 

 


Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi(Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel akitoa hotuba fupi kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi kuongea na Wananchi katika Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Nzuguni, Dodoma Agosti 5, 2020. 

 

ARUSHA



Mkuu wa Wilaya ya Longido na Mgeni Rasmi wa siku ya leo  Bw. Frank James Mwaisumbe akipanda farasi mara baada ya mashindano ya mifugo kwenye maonyesho ya nanenane yanayoendelea kwenye kiwanja cha Themi Mkoani Arusha. (05/08/2020) 

 


Daktari wa Mifugo kutoka kituo cha Uhimilishaji NAIC, Bw. Elibariki Njiku akitoa maelezo kwa wadau waliotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye maonyesho ya nanenane yanayoendelea kwenye kiwanja cha Themi Mkoani Arusha (05/08/2020) 


Afisa Uvuvi kanda ya Kaskazini, Bi. Gloria Patiri akitoa maelezo kwa wadau waliotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye maonyesho ya nanenane yanayoendelea kwenye kiwanja cha Themi Mkoani Arusha (05/04/2020) 


SIMIYU


Afisa kutoka Kitengo cha Mazingira, Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Magreth Domick akitoa maelekezo kwa wateja waliofika kwenye banda lao kwa ajili ya kupata huduma (05.08.2020) kwenye viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu. 



Afisa kutoka Kitengo cha Mazingira, Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Omary Mafitah (kushoto) akitoa maelekezo kwa wateja waliofika kwenye banda lao kwa ajili ya kupata huduma  (05.08.2020) kwenye viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu.



MBEYA


Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TARILI)kanda ya nyanda za juu kisini -Uyole,Mbeya, Dr. Edwin Chang'a akiongea na waandishi wa habari kuhamasisha wadau na wananchi wote kutembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye maonyesho ya nanenane yanayoendelea kwenye viwanja vya John Mwakangale Mkoani Mbeya  ( 05/08/2020) 



 Afisa Mifugo kutoka shamba la Mifugo Sao Hill mafinga Mkoa wa Iringa Domitila Barnos akitoa maelezo kuhusu malisho bora kwa mdau aliyetembelea mabanda ya wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye maadhimisho ya maonyesho ya nanenane yanayoendelea kufanyika katika viwanja vya John Mwakangale mkoani Mbeya tarehe 05.08.2020. 

 






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni