Nav bar

Jumanne, 18 Agosti 2020

HABARI PICHA ZA MAONYESHO YA NANENANE KWA MIKOA YA SIMIYU, ARUSHA, KWA TAREHE 06/08/2020

Meneja wa benki ya NMB kanda ya Ziwa Mashariki Bw. Sospeter Magese (katikati) akitoa maelezo kwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina kuhusu kiasi cha Mkopo kilichotolewa na benki hiyo kwa wakulima, wafugaji na wavuvi mpaka sasa ikiwa ni sehemu ya ziara ya Mhe. Mpina aliyoifanya kwenye mabanda mbalimbali yaliyopo kwenye viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu (06.08.2020).

 


Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina (kushoto) akipata maelezo kuhusu sheria na kanuni mbalimbali zinazoongoza sekta za mifugo Uvuvi kutoka kwa Mwanasheria wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Irene Lukindo (kulia) mara tu baada ya kufika kwenye mabanda ya Wizara hiyo ikiwa ni sehemu yake aliyoifanya kwenye mabanda mbalimbali yaliyopo kwenye viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu (06.08.2020).

 


Kutoka kulia Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu Zakariyya Kera ndc na Mkurugenzi wa Ukuzaji viumbe maji Dkt. Nazael Madala wakipata maelezo kwenye banda la Umoja wa wakulima wa mbogamboga na matunda (TAHA) wakati wa Ziara ya Mhe. Mpina kwenye mabanda mbalimbali yaliyopo kwenye viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu (06.08.2020).


 

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel (kushoto) akimpa maelezo Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina (wa tatu kutoka kulia) huku wakielekea yalipo mabanda ya sekta ya Uvuvi wakati wa Ziara ya Mhe. Mpina kwenye mabanda mbalimbali yaliyopo kwenye viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu  (06.08.2020).

 

ARUSHA


Afisa Uvuvi Mwandamizi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Pudensia Panga akitoa maelezo kwa wadau waliotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye maonyesho ya nanenane yanayoendelea kwenye kiwanja cha Themi Mkoani Arusha. (06/08/2020) 

 


Mkufunzi kutoka Wakala ya Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo (LITA), Bw. Ijumaa Bakari akitoa maelezo ya namna wanavyofanya kazi kwa mdau aliyetembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye maonyesho ya nanenane yanayoendelea kwenye kiwanja cha Themi Mkoani Arusha. (06/08/2020) 



Mchumi Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Sophia Mlote akitoa maelezo kwa wadau waliotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye maonyesho ya nanenane yanayoendelea kwenye kiwanja cha Themi Mkoani Arusha. (06/08/2020) 

 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni