Nav bar

Jumanne, 5 Desemba 2017


WAZIRI MPINA AUNDA TUME KUCHUNGUZA MKATABA WA KIWANDA CHA NYAMA DODOMA NA SERIKALI.
  • Aagiza Rachi za mifugo kuanza kuchinja mifugo katika kiwanda hicho ifikapo Machi mwakani.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh. Luhaga Mpina ameunda tume ya watu watano  kufanya tathmini ya utekelezaji wa mkataba  wa kiwanda cha nyama cha Dodoma baina ya  Serikali na Kampuni ya nyama Tanzania(TMC) baada ya muda wa mkataba wa miaka mitano kuisha huku uzalishaji wake ukiwa unasuasua.
Mh. Mpina alitoa maelekezo hayo hivi karibuni  kwa Meneja Mkuu wa Kiwanda hicho, bwana Nashon Kalinga  katika ofisi za kiwanda hicho wakati alipokuwa kwenye ziara ya kukagua shughuli mbalimbali za sekta ya mifugo akitokea katika ranchi ya Kongwa.

“Mimi kama Waziri mwenye dhamana ya Mifugo naelekeza kwamba Tume ipitie Mkataba  huu  ambao ushaisha muda wake na ikibainika kuwa wameshindwa kutekeleza nitaamuru kuvunjwa mara moja ili  kiwanda kifanye kazi kama ilivyokusudiwa” alisisitiza Mpina

Alisema Tume hiyo itawashirikisha wataalam kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Ofisi ya  Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Msajili wa Hazina na Ranchi za Taifa za Mifugo.

Katika hatua nyingine, Mh. Waziri amesitisha mkutano wa Bodi ya Kiwanda hicho uliotakiwa kufanyika tarehe 8 Disemba mwaka huu hadi Tume hiyo itakapowasilisha ripoti ya tathmini ya utekelezaji wa mkataba ulioisha wa miaka mitano.

Hata hivyo Mpina amesema  Serikali haiwezi kuruhusu kiwanda kufanya kazi  chini ya kiwango wakati kuna wawekezaji wengi ambao wana nia ya dhati ya kufanya kazi na kwamba Tanzania  bado ina soko kubwa  katika mazao ya mifugo duniani kote.

“Ni bahati mbaya sana tunaona kiwanda kinageuka  machinga badala ya kufanya kazi na kuleta tija katikakuelekea uchumi wa kati wa viwanda hapa nchini. Sisi kama Serikali hatukubaliani na hili” aliongeza Mh.Waziri.

Aidha amesema imefika wakati mwafaka sasa kwa Serikali  kwa Ranchi zote za mifugo kuzalisha  katika kiwango cha juu ili kiwanda hicho cha nyama (TMC) kiwe kinachinja mifugo kutoka Ranchi hizo na  kwa kuanzia amesema  ranchi ya Ruvu na Kongwa  lazima ziendelezwe  mara moja ili kutoa mifugo ya kutosha  na kuchinjwa katika kiwanda hicho. Katika uwekezaji huo Serikali ina hisa ya asilimia 41 wakati muwekezaji ana hisa ya asilimia 51.

“Nasema kuanziamwezi Machi mwakani nataka  tuwe tunachinja mifugo kutoka katika ranchi zetu. Naamini hili linawezekana kabisa, ni lazima tuanze sasa” amesisitiza Mh.Mpina.

Akiwa  katika ranchi ya Kongwa ametoa mwaka mmoja kwa uongozi wa ranchi hiyo kuongeza idadi ya mifugo kutoka 8647 ya sasa hadi kufika 20000 ifikapo Disemba 2018. Eneo la malisho kuwa limesafishwa  kutoka hekta 3000 za sasa hadi kufikia hekta 6000 katika kipindi hicho hicho.

Alisema Wizara itafanya tathmini ya utekelezaji wa maagizo hayo baada ya kipindi cha miezi sita ili kuona utekelezaji wake.Eneo la ranchi ya Kongwa linaukumbwa wa hekta 38000 ambapo ametaka  nusu ya hekta hizo kutumika katika uzalishaji wa malisho na nusu nyingine kwa ajili ya kuhifadhia mifugo hiyo.

Meneja Mkuu wa Ranchi za Mifugo nchini, Profesa Philemoni Wambura amesema Rachi ya Kongwa  uongozi wa rachi hiyo unamalengo ya kuzifanya ranchi zote nchini kuwa  mashamba darasa ya kuwafundishia wananchi namna bora ya uzalishaji wa malisho na mbegu bora  za mifugo.

Aidha amesema  kwa sasa Ranchi ya Kongwa   inayozalisha nyama bora duniani kinachotakiwa ni kuongeza uzalishaji wa nyama hiyo kwa kuwa mahitaji yake ni makubwa.

“Mh. Waziri tumepokea maelekezo yako tunaahidi kuzalisha kwa kiwango cha juu ili tujenge uchumi wetu wa viwanda” ameongeza Profesa.

Profesa amesema  kwa sasa kipaombele cha kwanza ni kuhakikisha kuwa rachi zinazalisha idadi kubwa ya majike  ya mbegu bora na kusambaza kwa wafugaji wote nchini ili kubadili ufugaji asilia na kwenda katika ufugaji wa kisasa wenye tija.

“Kwa kufanya hivyo tutapata mbegu  bora za mifugo wanaokuwa haraka, wanaotoa maziwa mengi na wenye kuhimili magonjwa na hiyo yatakuwa mapinduzi makubwa katika sekta hii nchini”amesisitiza Profesa.

Hata hivyo amesema mpango wa ranchi ni kuangalia namna  bora ya kuziingiza aina nyingine za ng’ombe kutoa kataika mikoa ya singida(Singida White), Sumbawanga(Fipa Type) na Iringa(Iringa Red) ili kuboresha zaidi badala ya kutegemea mbegu kutoka nje ya nchi ambazozina kufa  kwa kiasi kikubwa baada zinashindwa kuhimili hali ya hapa nchini.

Katika hatua nyingine, Mh. Waziri meuagiza uongozi wa rachi kuangalia namna ambavyo wanaweza kupunguza gharama ya kuuza mbegu bora za mifugo, ambapo kwa sasa dume la ngombe aina ya Borani linauzwa kwa milioni mbili hali ambayo inawafanya wafugaji wengi kushindwa kumudu.

Mwakilishi wa Katibu Mkuu aneyesimamia Sekta ya Mifugo katika ziara hiyo, bwana Victor Mwita, amesema kwa sasa Wizara imejipanga kuhakikisha uzalishaji wa malisho bora  unasimamiwa kikamilifu ili mifugo inayozalishwa kuwa  na tija.






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni