Nav bar

Jumatatu, 5 Januari 2026

MRADI WA CHATO BEACH UWANUFAISHE WALENGWA-DKT. BASHIRU

◼️Aagiza kusitishwa kwa mipango ya siri ya ugawaji wa vizimba vya biashara

Waziri wa Mifugo na Uvuvi amewaelekeza wasimamizi wa mradi wa soko la kimataifa la dagaa lililopo Chato maarufu kama “Chato Beach” kuhakikisha vizimba vya soko hilo vinawafikia walengwa waliokusudiwa wakati wa kuanzishwa kwa mradi huo.

Balozi Dkt. Bashiru amesema hayo mara baada ya kukagua hatua za ujenzi wa mradi huo Januari 04,2026 ambapo ameelekeza kuanza kutumika kwa mradi huo mara tu utakapokadhibiwa na mkandarasi Februari 28,2026.

“Ni lazima kuwepo na uwazi kuhusu usimamizi wa soko hili na ugawaji wa vizimba vilivyopo hapa na inawezekana mahitaji yakawa makubwa kuliko nafasi zilizopo lakini tunataka mfumo utakaotumika ukiwa wa wazi na haki hata atakayekosa akiri kukosa kwa sababu ya upungufu na sio mizengwe” Amesema Balozi Dkt. Bashiru.

Aidha Balozi Dkt. Bashiru amewaelekeza wataalam wa Wizara kukaa pamoja na wale wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato ili kupanga utaratibu wa kumpata mwendeshaji wa soko hilo na mtambo wa kuhifadhi ubora wa dagaa kupitia ukaushaji.

“Ni bora mtambo wa kukausha dagaa ukamilike mengine yasubiri kwa sababu taarifa za wataalam zinatueleza kwamba asilimia 30 ya dagaa wanaovunwa wanaharibika kwa sababu hatuna teknolojia ya ukaushaji na tukikausha kwa teknolojia duni ubora wa dagaa zetu unashuka” Amehitimisha Balozi Dkt. Bashiru.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (kushoto) akifafanua jambo kwa Mhandisi wa Wizara hiyo Bw. George Kwandu (kulia) na wataalam wengine wa Wizara hiyo wakati akikagua ujenzi wa Soko la dagaa la Chato Januari 04,2026. Wa pili kutoka kulia ni Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani.


Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (kushoto) akikagua hatua za ujenzi wa soko la dagaa lililopo Chato mkoani Geita Januari 04,2026. Kushoto kwake ni Mhandisi wa Wizara hiyo Bw. George Kwandu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni