Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amewataka watumishi wa Wizara hiyo kufanya kazi kwa juhudi ili kutekeleza maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan juu ya sekta hizo za uzalishaji.
Dkt. Kakurwa amesema hayo mara baada ya kupokelewa na Watumishi wa Wizara hiyo Novemba 18,2025 Wizarani hapo ikiwa ni muda mfupi baada ya kuapishwa kushika wadhifa huo.
"Sote tumesikia aliyosema Mhe. Rais kupitia hotuba yake ya ufunguzi wa Bunge kuhusu sekta zetu za Mifugo na Uvuvi hivyo ni wajibu wetu kuhakikisha tunatekekeza maono hayo kwa kila mmoja wetu kutimiza wajibu wake kwa nafasi aliyonayo" Amesema Dkt. Bashiru.
Aidha Dkt. Bashiru amewataka watumishi hao kutoa ushirikiano wa kutosha kwake na Naibu Waziri Mhe. Ng'wasi Kamani katika kipindi chote cha kuwahudumia wananchi hususan wadau wa sekta za Mifugo na Uvuvi.
Mhe. Balozi Dkt. Bashiru na Naibu wake Mhe. Kamani waliteuliwa na Rais Samia kushika nyadhifa hizo Novemba 17,2025.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agnes Meena akimkabidhi Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa nyaraka za utendaji wa ofisi yake Makao makuu ya Wizara hiyo Novemba 18,2025 Mtumba jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agnes Meena akimkabidhi Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng'wasi Kamani nyaraka za utendaji wa ofisi yake Makao makuu ya Wizara hiyo yaliyopo eneo la Mtumba jijini Dodoma Novemba 18,2025.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agnes Meena akimuongoza ofisini kwake Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng'wasi Kamani muda mfupi baada ya kuwasili makao makuu ya Wizara hiyo yaliyopo eneo la Mtumba jijini Dodoma Novemba 18,2025.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa akisaini kitabu cha wageni muda mfupi baada ya kuwasili na kupokelewa Makao Makuu ya Wizara hiyo yaliyopo eneo la Mtumba jijini Dodoma Novemba 18,2025.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng'wasi Kamani akisaini kitabu cha wageni muda mfupi baada ya kuwasili na kupokelewa Makao Makuu ya Wizara hiyo yaliyopo eneo la Mtumba jijini Dodoma Novemba 18,2025.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa akila kiapo cha kutumikia nafasi hiyo Novemba 18,2025 Ikulu jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng'wasi Kamani akila kiapo cha kutumikia nafasi hiyo Novemba 18,2025 Ikulu jijini Dodoma.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni