Na. Stanley Brayton, WMUV
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi yaanza Rasmi kutekeleza Mradi wa miaka Mitano wa Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT) ya Unenepeshaji wa Mbuzi na Kondoo katika eneo la Kituo cha Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) iliyopo Kongwa, ikiwa na lengo la kuongeza ushiriki wa Vijana na Wanawake katika ujasiliamali wa Biashara ya Mifugo.
Akizungumza wakati wa Ziara yake ya kikazi wakati akikagua Miundombinu ya Mradi huo, leo Novemba 27, 2025 Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Meena amesema Mradi huo unatarajiwa kuanza kutoa Mafunzo mapema mwaka huu, na lengo la Mradi huo ni kwa ajili ya kuwapatia Vijana Mafunzo ya Unenepeshaji wa Mbuzi na Kondoo ili waweze kufuga kibiashara.
“mradi huu utakuwa na uwezo wa kutoa Mafunzo kwa vijana 200 kwa mwaka na vijana Takribani 1750 wataweza kupata Mafunzo hayo kwa miaka Mitano.” amesema Bi. Meena
Aidha, Bi. Meena amesema Mradi huo una eneo la heka 2000 kwa ajili ya kupanda Malisho ya Mifugo na hautokuwa wa unenepeshaji wa Mbuzi na Kondoo tu, bali utajumuisha kilimo cha Malisho ya Mifugo, uzalishaji wa nyama na vyakula vya Mifugo.
Vilevile, Bi. Meena amewataka Maafisa wa Wizara hiyo, kuboresha sehemu za michezo katika Mradi huo kama sehemu Mpira wa Miguu, Mpira wa Pete na Mpira wa kikapu ili Vijana waweze kufanya mazoezi ili kujenga mwili baada ya shughuli za siku kuisha.





Hakuna maoni:
Chapisha Maoni