Nav bar

Alhamisi, 24 Julai 2025

SERIKALI YAANZA KUPANDIKIZA SAMAKI ZIWA HAUBI KONDOA DC

Na. Hamis Hussein

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Edwin Mhede amezindua rasmi upandikizaji wa vifaranga vya samaki aina sato katika ziwa Haubi lililopo halmashauri ya Wilaya ya Kondoa ili kuongeza aina ya samaki wanaopatika kwenye ziwa hilo.

Dkt. Mhede amezindua upandikizaji huo julai 21, 2025 katika kijiji cha Haubi ambapo amesema Wizara ya Mifugo na Uvuvi itatuma wataalam kwa ajili kufanya tathmini ya namna ya kulinda ikolojia ya ziwa hilo ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa wananchi kufanya upandikizaji wa vifaranga vya samaki.

Amesema ili kuongeza aina ya samaki wanaopatikana kwenye ziwa hilo  wizara itashirikiana na wananchi wa kijiji hicho ambao ndio wamiliki wa asili wa ziwa hilo na watalam watatoa  elimu ya jinsi ya kupandikiza  samaki aina ya sato tofauti na Kambare wanaopatikana kwa sasa ambao wamesababisha wananchi wa kijiji cha Haubi kuwa na mavuno ya samaki ya msimu.

Kwa upande kwake mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Bi. Mwasiti Juma amesema ziwa hilo  limekuwa likitumika kuwapatia wananchi mahitaji ya madogo madogo ya nyumbani hususani protini kutokana na samaki lakini changamoto ni uwepo wa samaki aina moja  jambo linalosababisha kuwa na mavuno kidogo na ya msimu.






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni