Nav bar

Alhamisi, 24 Julai 2025

BI. MEENA AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA UONGOZI WA MRADI WA C - SDTP JIJINI DODOMA

Na. Hamis Hussein

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agnes Meena ameongoza Kikao cha kamati ya uongozi wa mradi wa mageuzi katika tasnia ya maziwa kwa kuzingatia mabadiliko ya tabia nchi leo Julai 22, 2025 katika hoteli ya Rafiki jijini Dodoma.

Kikao hicho kimelenga Kutambulisha mradi huo wa mageuzi ya tasnia ya maziwa  kwa kuzingatia mabadiliko ya tabia ya nchi kwa kamati ya uongozi ili kamati iweze kupitia na kuuidhinisha mpango kazi wa mradi na manunuzi kwa mwaka 2025/ 2026.







Hakuna maoni:

Chapisha Maoni