Nav bar

Alhamisi, 20 Julai 2023

MATUKIO MBALIMBALI WAKATI WA MAONYESHO YA 47 YA KIMATAIFA YA BIASHARA SABASABA

 

Afisa Utafiti wa Mifugo Mkuu kutoka Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) Dkt.  Scholastica Doto (kushoto) akielezea kazi zinazofanywa na Wakala  kwa Balozi wa Uturuki Nchini Tanzania Dkt. Mehmet Gu"lw"ogui (kulia) alipotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya 47 ya kitaifa ya biashara sabasaba jijini Dar es salaam Julai 13,2023


Afisa Masoko kutoka kampuni ya SEAWEED, Bi. Sophia Mang'ena (kulia) akionyesha bidhaa walizonazo kwa   Balozi wa Uturuki Nchini Tanzania Dkt. Mehmet Gu"lw"ogui bidhaa walizonazo ikiwa ni pamoja na pilipili zinazopatikana kwenye kampuni hiyo alipotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya 47 ya kimataifa ya biashara sabasaba jijini Dar es salaam Julai 13,2023

Mkurugenzi wa Kampuni ya NASHA Aquar Fish Bw. Masumbuko Nzingula (kulia) akieleza fursa za uwekezaji kwenye mnyororo wa thamani wa ufugaji samaki kwa Mkurugenzi wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kutoka Keshi la kujenga Taifa (JKT) Makao makuu Dodoma, Kanali Peter Lushika (kushoto) alipotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya 47 ya kimataifa ya biashara yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam Julai 12,2023

Mkufunzi kutoka Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo (LITA) Bi. Aziza Shekalaghe (kulia) akieleza matumizi ya josho linaloamishika  kwa ajili ya kuongeshea mifugo midogo kama vile mbwa, mbuzi, kondoo, na nguruwe kwa Mkurugenzi wa Idara ya  Kilimo, Mifugo na Uvuvi kutoka Jeshi la kujenga Taifa (JKT) makao makuu Dodoma,  Kanali Peter Lushika (wa pili kutoka kushoto) alipotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya 47 ya kimataifa ya biashara yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam Julai 12,2023


Afisa Uvuvi Mwandamizi kutoka Idara ya Uvuvi (DFs) Bi. Neema Respickius (kushoto) akitoa elimu kwa njia  ya machapisho kwa  Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi - Zanzibar Mhe. Suleiman Makame (kulia) wakati alipotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya 47 ya kimataifa ya biashara yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam Julai 11,2023


Sehemu ya wadau wakiangalia kuku kwenye banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati walipotembelea banda hilo kwenye maonesho ya 47 ya kimataifa ya biashara yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam Julai 11, 2023

Afisa Mtafiti Mifugo kutoka Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) Bw. Jovith Kajuna (wa pili kushoto) akitoa elimu ya malisho ya mifugo zikiwemo aina mbalimbali za mikunde pamoja na nyasi  kwa  Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi -Zanzibar Mhe. Suleiman  Makame ( katikati) aliomtembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya kimataifa ya biashara yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es Salaam Julai 11,2023

Afisa Mtafiti Mifugo kutoka Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) Bw. Jovith Kajuna (wa pili kushoto) akitoa maelezo ya kina kuhusu ufanisi wa mizizi ya nyasi aina Cenchrus ciliaris kwa  Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi -Zanzibar Mhe. Suleiman  Makame  (katikati) alipotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya kimataifa ya biashara yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es Salaam Julai 11,2023

Afisa Mifugo Msaidizi Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Reuben Ngailo (kulia) akitoa elimu ya namna ya ulishaji bora wa ng'ombe wa maziwa kwa mdau Bw. Husein Khatibu alipotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya 47 ya kimataifa ya biashara yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam Julai 11,2023.

Mtakwimu Msaidizi kutoka  Mamlaka ya kusimamia Uvuvi wa Bahari Kuu (DSFA) Bw. Venance Nyanda (kulia) akitoa maelezo ya namna wanavyofanya kazi zao kwa Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi - Zanzibar Mhe. Suleiman  Makame (kushoto) alipotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya 47 ya Kimataifa ya biashara yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam Julai 11,2023.

Afisa Masoko wa Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB) Bw. Hamisi Kihimbi, (kulia) akitoa elimu ya namna ya kupima na kutunza maziwa kwa mdau Bi. Agatha Mmary  wakati alipotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye maonesho ya 47 ya  Kimataifa ya biashara sabasaba yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam Julai 11,2023

Mdau wa Sekta ya Mifugo, Bw. Paluku Emmanuel (kushoto) akitoa elimu juu ya umuhimu wa  lishe ya Mifugo  kwa Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi - Zanzibar Mhe. Suleiman Makame (katikati) aliotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya 47 ya Kimataifa ya biashara yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam Julai 11, 2023.

Mtunza Kumbukumbu kutoka Wakala wa Elimu na Mafunzo ya Uvuvi  (FETA) - Mbegani,  Bi. Lucy Kimea (kulia) akitoa elimu ya namna ya kuzalisha vifaranga vya samaki, ulimaji wa zao la mwani na matumizi ya mwani kwa wadau waliomtembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya 47 ya kimataifa ya biashara yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam Julai 11,2023.


Mtaalam kutoka Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania-TVLA Bwana Shukuru Guo akitoa elimu kwa mdau wa Mifugo raia wa kigeni alietembelea banda la TVLA kuhusiana na matumizi sahihi ya chanjo za Mifugo zinazozalishwa na Wakala siku ya tarehe 10/07/2023 kwenye Maonesho ya 47 ya Kimataifa ya Biashara kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba Dar es Salaam.


Mtaalam kutoka Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania-TVLA Dkt. Jelly Chang'a akitoa elimu kwa wadau wa Mifugo waliotembelea banda la TVLA kuhusiana na matumizi sahihi ya chanjo za Mifugo zinazozalishwa na Wakala siku ya tarehe 10/07/2023 kwenye Maonesho ya 47 ya Kimataifa ya Biashara kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba Dar es Salaam.


Nahodha kutoka Wakala wa Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) Bw. Halifa Snapenda  akitoa elimu kwa wadau ya namna ya kufuga samaki kwa njia ya kizimba wakati wa maoneshoya 47  ya Kimataifa ya biashara yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam Julai 10, 2023


Meneja kutoka Wakala ya Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania  (LITA) Temeke,  Bi. Benadetha Kessy (kushoto)  akitoa elimu ya namna ya kutumia josho kwa wadau waliotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya kimataifa ya biashara sabasaba yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam Julai 10,2023


Fundi Sanifu Mwandamizi kutoka Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) Bw. Hiari Chona (kushoto) akitoa elimu kwa wadau waliotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi juu  ya samaki aliyepotea miaka 65 milioni iliyopita na sasa ameanza kuonekana kwenye Pwani ya bahari ya Hindi mwaka 2003 kwenye maeneo ya Songosongo wakati wa  maonesho ya 47 ya kimataifa ya biashara yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam Julai 10,2023.


Mdau wa sekta ya Mifugo Bw. Emmanuel Paluku (kulia) akitoa elimu juu ya umuhimu wa  lishe ya Mifugo  kwa wadau waliotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya 47 ya kimataifa ya biashara yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam Julai 10,2023.


Mdau wa sekta ya Mifugo Bw. Emmanuel Paluku (kulia) akitoa elimu juu ya umuhimu wa  lishe ya Mifugo  kwa wadau waliotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya 47 ya kimataifa ya biashara yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam Julai 10,2023.


Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Agape ya mkoani Dar es Salaam waliotembelea banda la TDB wakipata maelezo juu ya matumizi ya mashine ya kukamulia maziwa toka kwa Mtaalamu wa mifugo wa kampuni ya Bajuta kwenye maonesho ya kimataifa ya kibiashara yanayoendelea katika Viwanja vya Mwl. JK Nyerere jijini Dar es Salaam (10.07.2023)


Mtaalamu wa mifugo toka Kampuni ya Bajuta inayojishughulisha na pembejeo za mifugo Bw. Sifaeli Dalei (kulia) akitoa maelezo ya namna ya matumizi ya mashine ya kukamulia ng'ombe wa maziwa kwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu waliotembelea banda la TDB kwa lengo la kujifunza kwenye maonesho ya Kimataifa ya biashara Sabasaba jijini Dar Es Salaam.(10.07.2023)


Afisa Utafiti kutoka Taasisi ya utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) Bw. Hakimu Matola (kushoto) akitoa elimu ya namna ya kukausha samaki aina ya jodari na dagaa kwa kutumia mwanga wa jua kwa mdau aliyetembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya kimataifa ya biashara yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam Julai 09,2023

Afisa Uvuvi Mkuu kutoka  Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO) Bw. Mgalula Lyoba (katikati) akitoa maelezo kuhusu samaki aina ya jodari kwa  wadau waliotembelea banda lao wakati wa maonesho ya kimataifa ya biashara sabasaba yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam Julai 09,2023


Mdau uvuvi upande wa Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu(MPRU) na Afisa mauzo kutoka kampuni ya Nyota Venture  Bw. Yahya Makuhana akitoa elimu ya matumizi ya nyavu za uvuvi kwa upande na ziwani na baharini  kwa wadau waliotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya kimataifa ya biashara yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam Julai 09,2023


Afisa Utafiti Mifugo kutoka Idara ya Utafiti, Mafunzo na Ugani , Bi Grace Masolwa akitoa elimu ya  ufugaji bora kupia machaposho  wakati wa maonesho ya kimataifa ya biashara yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam Julai 09, 2023


Mkufunzi kutoka Wakala wa Elimu na mafunzo ya Uvuvi (FETA) Bw.  Mashaka Shabani (kulia) akitoa elimu ya ufugaji wa samaki kwa mdau aliyetembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya kimataifa ya biashara yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam Julai 09,2023.


Afisa Uhusiano kutoka Kampuni ya Ranchi za Taifa Tanzania  (NARCO) Bw. Jumanne Mutalemwa, (kushoto)akitoa elimu ya utaratibu wa upatikanaji wa vitalu, na manufaa ya uwepo wa NARCO Tanzania kwa wadau Bw. Hamis  Makunga alipotembelea  banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya Kimataifa ya biashara  yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam,  Julai 09,2023


Mkufunzi kutoka Wakala ya Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA) Bw. Semu Geoffrey (kushoto) akitoa elimu juu ya namna ya kukuza vifaranga vya kuku kwa kutumia kinengunengu au brodder kwa wadau waliotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya kimataifa ya biashara yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam Julai 09,2023


Kaimu Meneja masoko kutoka Bodi ya Nyama Tanzania (TMB) Bw. Nicholai  Chiweka akitoa elimu ya  umuhimu wa usajili wa wadau katika tasnia ya nyama nchini, nyama bora na salama, na  mambo muhimu ya kuzingatia pale mdau anapotaka kuanzisha biashara ya nyama kwa Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu kutoka Wizara ya utamaduni, sanaa na michezo Bi. Emma  Lyimo  alipotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya kimataifa ya biashara yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam Julai 09,2023


Afisa Mtafiti Mifugo kutoka Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) Bw. Jovith Kajuna (kulia) akitoa elimu ya umuhimu wa jiwe lishe ikiwa ni pamoja na kumsaidia ng'ombe kutoa maziwa mengi, ng'ombe kukua vizuri na kuwezesha upatikanaji bora wa nyama kwa wadau waliomtembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya kimataifa ya biashara yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es Salaam Julai 09,2023


Mwanafunzi kutoka Wakala wa Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) Bw. Habibu Ramadhani akitoa elimu juu  ya kilimo cha mwani pamoja na utengenazaji wa bidhaa mbalimbali zitokanazo na mwani kwa wadau waliotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya kimataifa ya biashara yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es Salaam Julai 09,2023


Mtaalam kutoka Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) Bw. Henry chuma, akitoa elimu ya namna ya kuhakiki ubora wa vyakula vya mifugo kwa  mdau aliyetembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa maonesho ya kimataifa ya biashara yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam Julai 09, 2023.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) Prof. Erick Komba (kushoto) akisaini kitabu cha wageni siku ya tarehe 08/07/2023 alipotembelea banda la Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) lililopo Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika maonesho ya 47 ya Kimataifa ya Biashara kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba Dar es Salaam. Waliosimama kulia ni wataalamu kutoka TVLA Dkt. Scholastica Doto pamoja na Bwana Henri Mlundachuma.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) Prof. Erick Komba (kulia) akipata Maelezo kuhusiana na matumizi sahihi ya chanjo ya Homa ya Mapafu ya Mbuzi (CAPRIVAC-CCPP) kutoka kwa Dkt. Richard Mwakapuja mtaalamu kutoka Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania-TVLA siku ya tarehe 08/07/2023 alipotembelea banda la TVLA lililopo Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika maonesho ya 47 ya Kimataifa ya Biashara kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) Prof. Erick Komba (kulia) akitoa elimu kwa wadau wa mifugo kuhusiana na virutubisho asilia vyenye sifa ya kuongeza uzalishaji, ustahimilivu, kuimarisha kinga ya mwili dhidi ya magonjwa na kupunguza matumizi ya madawa ya mifugo  kwa ajili ya kuongeza ukuaji na kiasi cha uzalishaji wa Mifugo na mazao ya Mifugo kama mayai, nyama na maziwa siku ya tarehe 08/07/2023 katika banda la TALIRI lililopo katika eneo la mabanda ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika maonesho ya 47 ya Kimataifa ya Biashara kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba Dar es Salaam.

Mtaalamu kutoka Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) bwana Jovith Kajuna akitoa elimu kwa wadau wa Mifugo kuhusiana na malisho ya Mifugo (nyasi) yenye virutubisho kwa Mifugo na zinazofaa kupandwa kwenye maeneo yao kwa ajili ya ustawi wa Mifugo siku ya tarehe 08/07/2023 banda la TALIRI lililopo Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika maonesho ya 47 ya Kimataifa ya Biashara kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba Dar es Salaam.

Mtalam kutoka LITA bi Aziza Shekalage atoa elimu kwa mfungaji wa kuku namna ya bora ya kufunga vifanga kwa kutumia njia ya kinengunengu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni