Watumishi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Sekta ya Uvuvi wamefanya kikao cha Baraza la Wafanyakazi kwa ajili ya kujadili namna walivyotekeleza bajeti ya mwaka 2021/2022 na kujipanga kutekeleza bajeti ya mwaka 2022/2023.
Kikao hicho kimefanyika
(12.04.2022) Mkoani Singida ambapo Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi
anayeshughulikia Sekta ya Uvuvi Dkt. Rashid Tamatamah amewasihi watumishi
kufanya kazi kwa kuzingatia weledi na kuona ni namna gani wanaweza kutatua
changamoto zilizopo ili sekta hiyo iweze kuchangia zaidi kwenye pato la taifa.
Dkt. Tamatamah amesema kikao hicho
ni muhimu kwa watumishi kwa kuwa watumishi wanashirikishwa kwa uwazi kuhusu
namna walivyotekeleza bajeti ya mwaka 2021/2022 na kujipanga kutekeleza bajeti
ya mwaka 2022/2023.
Aidha, amewasihi wajumbe wa
walioshiriki baraza hilo kuhakikisha wanatoa ushauri mzuri ili kuhakikisha
sekta ya uvuvi inakua na kuongeza mchango wake kwenye pato la taifa.
Pia, amewataka watumishi kuendelea
kujilinda na magonjwa yanayoambukiza na yasiyoambukiza na kuwataka watumishi
kufanya mazoezi ili kuendelea kuimarisha afya zao.
Katibu mkuu huyo amewapongeza
wafanyakazi wa Sekta ya Uvuvi kwa kushiriki vyema kwenye mashindano ya
(SHIMIWI), hivyo kuhakikisha wanaendelea kujiandaa ili katika mashindano
yanayofuata wanafanya vizuri zaidi.
Naye Mkurugenzi wa Idara ya
Ukuzaji Viumbe Maji, Dkt. Nazael Madala amesema kikao hicho kimewasaidia kujua
changamoto walizokuwa wanakabiliana nazo katika utekelezaji wa bajeti na hivyo
kuandaa mikakati ya kukabiliana nazo.
Kwa upande wake Mkurugenzi
Msaidizi - Utumishi, Bi. Mary Mwangisa amesema kuwa watumishi wanapata elimu ya
kuwasaidia kwenda kuboresha utendaji kazi wao kwa kuwa watakuwa wameshafahamu
kazi zinazotakiwa kutekelezwa kulingana na bajeti iliyotengwa.




Hakuna maoni:
Chapisha Maoni