Nav bar

Jumanne, 26 Januari 2021

WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI YATOA MAFUNZO KWA WADAU WA UVUVI WA KATA YA MIGOLI MKOANI IRINGA

 

Afisa Uvuvi Mwandamizi (WMUV), Hamidu Njegite (aliyesimama katikati) akiwaeleza wadau wa uvuvi wa kata ya Migoli, halmashauri ya Wilaya ya  Iringa faida za kuunda ushirika wakati wa Mafunzo rejea kwa wadau hao, yaliyokuwa pia na lengo la kuhamasisha uanzishwaji wa vyama vya ushirika vya wavuvi. Mafunzo hayo yanafanyika katika mwalo wa Migoli na Chapuya, kata ya Migoli, Wilaya ya Iringa, mkoani Iringa. (18/01/2021)

Diwani wa kata ya Migoli, Mhe. Benitho Kayugwa (aliyevaa suti nyeusi) akifungua Mafunzo rejea ya wadau wa uvuvi wa kata ya Migoli, halmashauri ya Wilaya ya  Iringa yaliyokuwa pia na lengo la kuhamasisha uanzishwaji wa vyama vya ushirika vya wavuvi. Mafunzo hayo yanafanyika katika mwalo wa Migoli na Chapuya, kata ya Migoli, Wilaya ya Iringa, mkoani Iringa. (18/01/2021)

Mkufunzi Mwandamizi (WMUV), Bi. Kresensia Mtweve (aliyesimama katikati) akiwaeleza wadau wa uvuvi wa kata ya Migoli, halmashauri ya Wilaya ya  Iringa jinsi ya kupunguza upotevu wa mazao ya uvuvi wakati wa Mafunzo rejea kwa wadau hao, yaliyokuwa pia na lengo la kuhamasisha uanzishwaji wa vyama vya ushirika vya wavuvi. Mafunzo hayo yanafanyika Chapuya, kata ya Migoli, Wilaya ya Iringa, mkoani Iringa. (18/01/2021)
Afisa Mfawidhi kutoka Bwawa la Nyumba ya Mungu, Bw. Godbless Msuya (aliyesimama katikati) akiwaeleza wadau wa uvuvi wa kata ya Migoli, halmashauri ya Wilaya ya  Iringa jinsi ya kutunza rasilimali za uvuvi wakati wa Mafunzo rejea kwa wadau hao, yaliyokuwa pia na lengo la kuhamasisha uanzishwaji wa vyama vya ushirika vya wavuvi. Mafunzo hayo yanafanyika katika mwalo wa Migoli na Chapuya, kata ya Migoli, Wilaya ya Iringa, mkoani Iringa. (18/01/2021)

Afisa Ushirika kutoka halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Bi. Neema Lema (aliyesimama katikati) akiwaelimisha wadau wa uvuvi wa kata ya Migoli, halmashauri ya Wilaya ya  Iringa namna ya kuanzisha vyama vya Ushirika wakati wa Mafunzo rejea kwa wadau hao, yaliyokuwa pia na lengo la kuhamasisha uanzishwaji wa vyama vya ushirika vya wavuvi. Mafunzo hayo yanafanyika katika mwalo wa Migoli na Chapuya, kata ya Migoli, Wilaya ya Iringa, mkoani Iringa. (18/01/2021)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni