Nav bar

Jumanne, 26 Januari 2021

MHE. NDAKI ATEMBELEA SHAMBA LA MFUGAJI JOSAM NTANGEKI LILILOPO KWENYE RANCHI YA KIKURURA WILAYANI KARANGWE, MKOA WA KAGERA.

 

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki (katikati) akitoa maelekezo mara baada ya kufika kwenye shamba la Mfugaji anayefahamika kwa jina Josam Ntangeki lililopo kwenye ranchi ya Kikukurura wilayani Karagwe Mkoa wa Kagera jana (19.01.2021). Wengine pichani ni Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel (wa kwanza kushoto) na Kaimu Msajili wa Bodi ya Maziwa Bw. Noeli Byamungu (wa kwanza kulia).
Kaimu Msajili wa Bodi ya Maziwa nchini (TDB) Bw. Noely Byamungu (katikati) akimweleza Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki (wa pili kutoka kulia) juu ya namna Bodi inavyompa ushirikiano Mmoja wa wawekezaji wa Ng'ombe wa Maziwa waliopo kwenye ranchi ya Kikulula Bw. Josam Ntangeki (wa pili kutoka kushoto), baada ya Mhe. Mashimba kutembelea ranchi hiyo jana (19.01.2021).

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki (kulia) na katibu Mkuu wa wizara hiyo (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel wakikagua moja ya ng'ombe waliopo kwenye kitalu cha Mwekezaji Josam Ntangeki muda mfupi baada ya kufika kwenye ranchi ya Kikulula iliyopo Wilayani Karagwe mkoa wa Kagera jana (19.01.2021)

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Elisante Ole Gabriel (kushoto) akifafanua jambo kwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki (kulia) muda mfupi baada ya kufika kwenye shamba la mwekezaji wa ndani Bw. Josam Ntangeki lililopo kwenye Ranchi ya Kikurura wilayani Karagwe Mkoa wa Kagera jana (19.01.2021)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni