Nav bar

Jumamosi, 24 Oktoba 2020

PROF. GABRIEL AFUNGA MAFUNZO YA SIKU MBILI YA WAKAGUZI WA VYAKULA VYA MIFUGO

Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Uendelezaji Maeneo ya Malisho na Rasilimali za vyakula vya Mifugo (WMUV), Bw. Rodgers Shengoto akitoa maelezo mafupi kwa Mgeni Rasmi kuhusu mada zilizowasilishwa katika mafunzo hayo ya siku mbili ya wakaguzi wa vyakula vya Mifugo kwa Kanda ya Mashariki na Kati, yaliyofanyika katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) mkoani Morogoro. (23.10.2020)

Washiriki wa mafunzo ya ukaguzi wa vyakula vya Mifugo wakisikiliza kwa makini mgeni rasmi ambaye pia ni Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel (hayupo pichani) wakati akifunga mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA), mkoani Morogoro. (23.10.2020)

Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Maeneo ya Malisho na Rasilimali za Vyakula vya Mifugo (WMUV), Dkt. Asimwe Rwiguza akitoa taarifa fupi kwa mgeni rasmi kuhusu mafunzo ya siku mbili ya wakaguzi wa Vyakula vya Mifugo wakati wa kufunga mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) mkoani Morogoro. (23.10.2020)

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel akitoa hotuba ya kufunga mafunzo ya siku mbili ya wakaguzi wa vyakula vya Mifugo Kanda za Mashariki na Kati, yaliyofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Kilimo Sokoine (SUA) mkoani Morogoro. (23.10.2020)

Mshiriki wa mafunzo ya siku mbili ya wakaguzi wa vyakula vya Mifugo Kanda ya Mashariki na Kati, Bi. Odetha Mchunguzi akitoa neno la shukrani kwa Mgeni Rasmi kwa niaba ya wenzake, wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo, yaliyofanyika katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) mkoani Mororgoro. (23.10.2020)

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel akimvalisha kitambulisho mmoja wa wahitimu wa mafunzo ya siku mbili ya wakaguzi wa Vyakula vya Mifugo kwa Kanda ya Mashariki na Kati yaliyofanyika katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) mkoani Morogoro. (23.10.2020)






 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni