Nav bar

Jumamosi, 24 Oktoba 2020

DKT. TAMATAMAH AKABIDHI INJINI ZA BOTI KWA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAVUVI KANDA YA ZIWA VICTORIA.

 

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (kulia) akikabidhi Injini ya Boti kwa Kaimu Mwenyekiti wa Chama cha Ushirika wa Wavuvi Zilagula, Bi. Agness Mbasha katika hafla fupi ya kugawa Injini za Boti kwa Vyama vya Ushirika vya Wavuvi Kanda ya Ziwa Victoria iliyofanyika katika Wilaya ya Muleba, Mkoani Kagera. (23.10.2020)

Pichani ni Injini za Boti (4) aina ya Yamaha ambazo Wizara ya Mifugo na Uvuvi imezikabidhi kwa Vyama vinne (4) vya Ushirika vya Wavuvi Kanda ya Ziwa Victoria katika hafla fupi iliyofanyika Wilayani Muleba, Mkoani Kagera. (23.10.2020)

Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (kulia) akijadiliana jambo na Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Utafiti na Mafunzo ya Uvuvi, Dkt. Erastus Mosha (kushoto) muda mfupi kabla ya kukabidhi Injini za Boti kwa Vyama vya Ushirika vya Wavuvi Kanda ya Ziwa Victoria katika hafla fupi iliyofanyika Wilayani Muleba, Mkoani Kagera. (23.10.2020)

Mkurugenzi Msaidizi, Kitengo cha Huduma za Ugani za Uvuvi, Anthony Dadu akifafanua jambo katika hafla fupi ya kukabidhi Injini za Boti kwa Vyama vya Ushirika vya Wavuvi Kanda ya Ziwa Victoria iliyofanyika Wilayani Muleba, Mkoani Kagera. (23.10.2020)

Mkazi wa Kasenyi, Ikuza, Wilayani Muleba, Mkoani Kagera, Edgar Katunzi akiuliza swali kwa Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (hayupo pichani) katika hafla fupi ya kugawa Injini za Boti kwa Vyama vya Ushirika vya Wavuvi Kanda ya Ziwa Victoria iliyofanyika Wilayani Muleba, Mkoani Kagera. Wengine katika picha ni Sehemu ya Wananchi wanaofanya shughuli za Uvuvi Mkoani humo. (23.10.2020)

Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba, Bw. Omary Mchengule akizungumza katika hafla fupi ya kugawa Injini za Boti kwa Vyama vya Ushirika vya Wavuvi Kanda ya Ziwa Victoria iliyofanyika Wilayani Muleba, Mkoani Kagera. Kulia kwake ni Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah na kushoto kwake ni Kaimu Mkurugenzi, Idara ya Uvuvi, Stephen Lukanga. (23.10.2020)

Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi na Wawakilishi wa Vyama vya Ushirika vya Wavuvi Kanda ya Ziwa Victoria muda mfupi baada ya kukabidhi Injini za Boti kwa Vyama (4) vya Ushirika wa Wavuvi wilayani Muleba, Mkoani Kagera. Kutoka kulia waliokaa ni Mkurugenzi Msaidizi, Kitengo cha Huduma za Ugani za Uvuvi, Anthony Dadu akifuatiwa na Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Utafiti na Mafunzo ya Uvuvi, Dkt. Erastus Mosha. Kutoka kushoto ni Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Muleba, Omary Mchengule akifuatiwa na Kaimu Mwenyekiti Chama cha Ushirika cha Wavuvi Zilagula, Bi. Agness Mbasha. (23.10.2020)



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni