Nav bar

Jumatano, 19 Agosti 2020

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI, MHE. ABDALLAH ULEGA ATEMBELEA GEREZA LA KARANGA KUJIONEA UJENZI WA KIWANDA CHA BIDHAA ZA NGOZI (KILIMANJARO LEATHER INDUSTRIES CO. LTD






Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega akikagua ramani ya ujenzi wa kiwanda cha bidhaa za ngozi Kilimanjaro Leather Industries Co. Ltd kilichopo katika eneo la Gereza la Karanga Mkoani Kilimanjaro, ambapo ujenzi wa kiwanda hicho utagharimu zaidi ya Shilingi Bilioni 60. Pembeni yake ni Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda hicho Mhandisi Masoud Omary. (08.08.2020) 


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kufika katika ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro akiwa na baadhi ya maafisa kutoka katika wizara hiyo na kukutana na mkuu wa mkoa huo Dkt. Anna Mghwira ambapo wamezungumza mambo mbalimbali ya kuboresha sekta ya mifugo na uvuvi kabla ya kuelekea katika Gereza la Karanga kujionea ujenzi wa kiwanda cha bidhaa za ngozi cha Kilimanjaro Leather Industries Co. Ltd. (08.08.2020) 

 


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega akikagua baadhi ya mitambo itakayofungwa katika kiwanda cha bidhaa za ngozi cha Kilimanjaro Leather Industries Co. Ltd kilichopo katika eneo la Gereza la Karanga Mkoani Kilimanjaro na kusisitiza watanzania kununua bidhaa za ngozi zinazozalishwa hapa nchini ili kuunga mkono jitihada zinazofanywa na wawekezaji pamoja na wajasiriamali. (08.08.2020) 


Muonekano wa maendeleo ya ujenzi wa kiwanda cha bidhaa za ngozi cha Kilimanjaro Leather Industries Co. Ltd kilichopo katika Gereza la Karanga Mkoani Kilimanjaro, ambapo Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amelipongeza Jeshi la Magereza Mkoa wa Kilimanjaro kwa kutumia nguvu kazi ya wafungwa kwa ajili ya ujenzi huo ambapo baadhi ya wafungwa wamepatiwa pia elimu ya ujenzi katika gereza hilo. (08.08.2020) 

 


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega akikagua ubora wa matofali yanayotengenezwa na wafungwa wa Gereza la Karanga kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha bidhaa za ngozi cha Kilimanjaro Leather Industries Co. Ltd kilichopo katika eneo la gereza hilo, ambapo ameridhishwa na ubora wa matofali hayo ambayo ni mchanganyiko wa saruji na vumbi la miamba/mawe. (08.08.2020) 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni