Nav bar

Ijumaa, 29 Mei 2020

"WATANZANIA TUNYWE MAZIWA YA HAPA NCHINI"-ULEGA




Watanzania wametakiwa kuwa wazalendo kwa kunywa maziwa yanayotengenezwa hapa nchini ili kuendeleza uchumi wa viwanda na Taifa kwa ujumla.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega wakati akifungua maadhimisho ya 23 ya wiki ya maziwa  Mkoani Dodoma kwa njia ya kielectronic 

"Ninaomba Sana na ninawasisitiza watanzania lazima tuwe na wivu wa maendeleo kwa ajili ya Taifa letu, lazima tuwe na uzalendo wa Taifa letu" Ulega

Pia ameongezea na kusema kuwa Mhe. Raisi wetu Dr John Joseph Pombe Magufuli ametupa Ari kubwa Sana ya uzalendo kwa kupenda vya kwetu.

Imeelezwa kuwa sekta ya Mifugo katika Pato la Taifa hapa nchini inachangia kwa asilimia saba (7%) huku asilimia thelathini (30%) ikitokana na sekta ndogo ya maziwa hivyo asilimia 1.2% ya Pato zima la Taifa inatokana na sekta ya maziwa.

Mhe. Ulega amesema  Katika mwaka 2017/2018 kulikua na jumla ya viwanda (76,) lakini hivi Sasa tunajumla ya viwanda (99) kwa hivyo tunazidi  ongezeko la viwanda vidogo,vya Kati na vikubwa 20 katika Taifa letu.

Naye Kaimu msajili wa bodi ya maziwa Dr Sophia Mlote amesema bodi ya maziwa imefanya jitihada kubwa kwa kushirikiana na mashirika mbalimbali katika kuhakikisha tasnia ya maziwa inakua kwa kiasi kikubwa

Maadhimisho ya wiki ya maziwa yanakwenda sambamba na kauli mbiu isemayo "wiki ya maziwa 2020 chagua viongozi Bora kwa maendeleo ya tasnia ya maziwa"


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.Abdallah Ulega akifungua rasmi Maadhimisho ya Wiki ya Maziwa Kielekitroniki 2020 yaliyofanyika kitaifa Mkoani Dodoma. Maadhimisho haya ni ya 23 kufanyika tangu kuanzishwa kwa Maadhimisho haya mwaka 1997 yakiwa na lengo la kuhamasisha unywaji wa maziwa nchini kutoka wastani wa Lita 49 kwa mtu kwa mwaka hadi kufika Lita 200 kwa mtu kwa mwaka. 


Kaimu msajili wa bodi ya maziwa bi Sophia Mlote akitoa Taarifa ya tasnia ya maziwa katika ufunguzi wa maadhimisho ya wiki ya maziwa, na wadau wakimsikiliza kwa makini,maadhimisho hayo yalifanyika katika ukumbi wa treasure square  tarehe 28/05/2020

Mkurugenzi wa Uzalishaji na Masoko Dkt. Felix Nandonde kwa niaba ya Katibu Mkuu (M) akimkaribisha Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe.Abdallah Ulega kwenye Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Maziwa Kielekitroniki yaliyofanyika kitaifa Mkoani Dodoma. 


Katibu Tawala Mkoa Ndugu, Maduka  Kessy akitoa neno la shukrani kwa Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mh.Abdallah Ulega mara baada ya ufunguzi rasmi wa Maadhimisho ya Wiki ya Maziwa kwa njia ya Kielekitroniki jijini Dodoma,

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni