Nav bar

Ijumaa, 22 Mei 2020

WAFUGAJI WAELEZWA UMUHIMU WA UHIMILISHAJI.





Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti na Mafunzo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Hassan Ally Mruttu ameongoza zoezi la utoaji mafunzo ya umuhimu wa uhimilishaji na faida ya zoezi hilo kwa  wafugaji Mkoani Kagera.



Akiongea wakati wa mafunzo elekezi ya uhamasishaji wa umuhimu wa uhimilishaji wa ng'ombe kwenye kijiji cha Kagenyi Wilaya ya Kyerwa Mkoani Kagera Jana (10/05/2020) Dkt. Hassan Mruttu amesema lengo la mafunzo hayo ni kutaka wafugaji kufuga kwa kuongezea thamani ng'ombe wao.



"Ufugaji wa kisasa unawezesha mfugaji kupata ng'ombe wengi na bora wwnaokuwa kwa haraka na kutoa maziwa na nyama kwa wingi kuliko ng'ombe wasioboreshwa." Amesema Dkt. Mruttu.



Aidha ametoa wito kwa wafugaji kusaidiana na kupeana taarifa za upandikizaji wa mbegu bora za ng'ombe (uhimilishaji) ili wafugaji wengi waweze kufikiwa na huduma hiyo.



Naye mtafiti wa Mifugo, Bi. Neema Urassa kutoka Taasisi ya Utafiti wa Mifugo nchini (TALIRI) amewaelekeza  wafugaji kuwa pamoja na uhimilishaji wa ng'ombe kwa kutumia mbegu za ng'ombe walioboreshwa  ni muhimu wafugaji kubadili mtizamo na kukubali  kufuga kibiashara na kuzingatia uvunaji wa ng'ombe kwa msimu unaofaa.





Aliongeza kuwa uzalishaji wa ng'ombe bora na bidhaa zake utachangia katika kukidhi mahitaji ya lishe bora ya kaya na upatikanaji wa malighafi za viwanda.



Kwa upande wake afisa mifugo wa Wilaya ya kyerwa Mkoani Kagera Bw.  Fred Kija amewasihi wafugaji kuendelea kupeana taarifa za uhimilishaji ili kusaidia wafugaji wengi kuweza kufikiwa na kupata huduma iyo



Hata hivyo mwenyekiti wa wafugaji kijiji cha Kaitambuzi Bw. Charles Bwanakunu ameelezea changamoto wanazozipata ikiwa ni pamoja na serikali ya kijiji  kuchukua ardhi yao na kumuomba  Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina na  serikali kwa ujumla kuwasaidia kutatua changamoto hiyo ili wafugaji wa kyerwa waweze kupata haki yao na kufanya kazi zao bila usumbufu.



Aidha ameishukuru serikali kwa kuweza  kuona umuhimu wao kama wafugaji na kuwafikia kwa kuwapa elimu ya ufugaji wa kisasa, uhimilishaji, kuvuna na kufuga kibiashara na kuahidi kufanya kazi maarifa hayo yaliyoyapa.

Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti na Mafunzo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (wa kwanza kulia) Dkt. Ally Hassan Mruttu akitoa elimu ya umuhimu na faida za uhimilishaji kwa wafugaji na wasaidizi wao kwenye shamba la KMC LTD linalosimamiwa na  Bw. Elias Leopold Wilaya ya Kyerwa Mkoani Kagera. (10/05/2020) 

Mtafiti kutoka TALIRI Bi. Neema Urassa (wa pili kutoka kulia) akimuelimisha mfugaji faida ya  kuongeza thamani kwa mifugo,  kufuga kibiashara na kuvuna mifugo yake ili iweze kuwa na tija kwake na kumuongezea kipato jana katika Wilaya ya Kyerwa Mkoani Kagera. (10/05/2020) 

Watafiti  kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakiangalia mifugo iliyotengwa kwa ajili ya  zoezi la uhimilishaji kwenye shamba la KMC LTD wilayani Kyerwa Mkoani Kagera. (10/05/2020) 



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni